Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amesema kuwa kasi ya ukuaji wa
sekta ya madini imeongezeka kutoka asilimia 4 mwaka 2015 mpaka asilimia 4.8
mwaka 2018 baada ya marekebisho ya baadhi ya sheria na usimamizi bora katika
sekta hiyo.
Akizungumza leo
katika Mkutano wa Sekta ya Madini uliokutanisha wadau, wachimbaji wadogowadogo
wa madini, wafanyabiashara wa madini pamoja na wafanyakazi wa Wizara ya Madini
uliofanyika Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli alisema kuwa kwa marekebisho ya
sheria ya Madini yam waka 2010 imewezesha rasilimali ya madini kuwa mali ya
watanzania.
Rais Magufuli aliseme
kuwa katika kufanya mageuzi makubwa katika Sekta hiyo Serikali ililzimika
kuunda Wizara ya Madini iliyopewa dhamana ya kulinda rasilimali hiyo mnamo
mwaka 2017 na kuweza kupata mafanikio makubwa kwa miaka miwili iliyopita.
“Marekebisho ya Sheria ya Madini ya Mwaka 2010
ilifanya mambo mengi sana katika sekta ya madini ikiwemo kurudisha umiliki wa
rasilimali madini kwa watanzania na kuwezesha usimamizi na udhibiti wa
utoroshwaji madini huku ikiwezesha ujenzi wa ukuta katika eneo la madini ya
Tanzanite (Mererani) hii iliiwezesha Tanzania kulinda kwa ukaribu madini yetu”,
alisema Rais Magufuli
Rais Magufuli alisema
kuwa sekta hiyo chini ya Wizara ya Madini ilikuwa kwa kasi na kuwezesha utoaji
wa leseni za wachimbaji wadogowadogo 15,209 huku wachimbaji wengine 5303
wakipata mafunzo ya uchimbaji Madini katika mikoa 14 nchini.
Aidha kasi hiyo
ilihusisha Serikali kutoa ruzuku ya fedha za kitanzania bilioni 7.616 ya
uchimbaji madini mbalimbali hapa nchini, huku ikiwezesha uzalishaji wa madini
kuwa mkubwa zaidi ukilinganisha na miaka ya nyuma, takwimu zinasema kuwa katika
mgodi wa almasi Mwadui uzalishaji uliongezeka kwa kuzalisha karati 341,000
mwaka 2018, kiasi ambacho kwa mara ya mwisho kuzalishwa ilikuwa ni mwaka 1977
karati 317,000 zilizalishwa kiwango ambacho kinakaribia kwenye kiwango cha
sasa.
“Mabadiliko makubwa
katika sekta hii sasa tumeanza kuyaona hasa katika uzalishaji wa madini katika
migodi mbalimbali ikiwemo Mgodi wa Almasi Mwadui ambao ulizalisha karati
341,000 mwaka 2018, hiki ni kiasi kikubwa na kwa mara ya kwanza kwa mgodi huu
kuzalisha kiasi kikubwa ilikuwa mwaka 1977 ambapo ulizalisha karati 317,000 kwa
hiyo hii inathibitisha kuwa uzalishaji katika sekta hii ya madini umekuwa kwa
kasi”, alisema Rais Magufuli.
Pia Serikali imeweza
kukusanya na kuvuka malengo ya ukusanyaji mapato ya shilingi bilioni 194 badala
yake kuweza kukusanya shilingi bilioni 301 katika sekta ya madini ikiwa ni
ongezeko la asilimia 53, na katika nusu ya mwaka wa fedha 2018/2019 Serikali
ilipanga kukusanya shilingi bilioni 160 lakini iliweza kuvuka malengo kwa
kupata shilingi bilioni 167.54 sawa na asilimia 8 ya makusanyo.
Rais Magufuli aliongeza
kuwa uzalishaji umeongezeka kwa wachimbaji wadogowadogo wa madini ya Tanzanite
kutoka kilo 147.7 mwaka 2017 na 164.6
mwaka 2016 hadi kilo 781.2 mwaka 2018,
huku wakiweza kuongeza mapato kutoka shilingi milioni 166.094 mwaka 2017 mpaka
bilioni 1.436 mwaka 2018 baada ya udhibiti na usimamizi mzuri katika sekta
hiyo.
Rais Magufuli pia
aliwaagiza watendaji wa Wizara ya Mdaini kufanya kazi kwa kushirikiana na Wadau,
Wachimbaji, Wafanyabiashara wa Madini ili kuiboresha sekta ya madini nchini kuweza
kutoa mapato makubwa kwa Serikali na kusema kuwa anawapongeza Wizara hiyo
pamoja na wadau wenginewa madini kwa mafanikio hayo yaliyopatikana ndani ya
muda mfupi.
No comments:
Post a Comment