NA
K-VIS BLOG/Khalfan Said, Monduli
MRADI
wa umeme wa Kenya-Tanzania Power Interconnection
(KTIPIP)ZTK tayari umeanza kutekelezwa ambapo kazi ya kutengeneza
misingi ya kusimika minara (towers) imeanza, Mratibu wa Mradi huo kutoka
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Peter Kigadye amewaambia wahariri
wa vyombo vya habari waliotembelea kambi ya wakandarasi iliyoko kijiji cha
Nanja kilichoko barabara ya Bababti-Arusha wilayani Munduli leo Januari 22, 2019.
Mradi
huo ni sehemu moja ya mradi mzima wa regional
power connection ambao lengo lake ni kuunganisha mfumo wa umeme wa Tanzania
na Afrika Mashariki (East Africa Power Pool) kwa upande wa Kaskazini, na
baadaye utekelezaji wa sehemu nyingine ya tatu ambayo itakuwa inaunganisha
mifumo ya nxchi Kusini mwa Afrika, kupitia chombo kinachoitwa Southern Africa
Power Pool (SAPP)
“Tanzaania
tumebarikiwa tutakuwa na sehemu tatu ya kwanza ni mradi wa Backborn ambao
umejengwa katikati ya nchi yetu na ulikuwa na kilomita 670 inaanzia Shinyanga
hadi Iringa, sehemu ya pili ni kuunga kutoka Singida hadi mpakani na Kenya kuna
kituo kimoja kinaitwa Isinya, jumla hapo kuna kilomita 510.7 na hizo ndio
kilomita za mradi tunazoanza kuutekeleza hivi sasa.” Alisema Mhandisi Kigadye.“Baada
ya hapo sehemu ya tatu ni kuanzia Iringa kwenda Kusini ambapo kuna mradi
utakaoitwa Zambia Interconector ambako kuna kilomita nyingine 624 kwahiyo
Tanzania tutakuwa tumekamilisha ule mkongo wa msongo wa kilovoti 400.” Alisema
Mhandisi Kigadye.Akielezea
zaidi kuhusu kuunganiushwa kwa umeme kwenye nchi za Ukanda wa Mashariki na
Kusini Mhandisi Kigadye alisema, “ Lengo ni kuunganisha nchi yetu na ukanda
nchi za Kikanda kuanzia Kaskazini kuungana na Kenya na Kusini kuungana na
Zambia.”
Alisema
mradi wa Kenya-Tanzania Power Interconnection
(KTIPIP)ZTK, utakamilika Aprili 2020, wakati ule Zambia Connector utakamilika
mwaka 2022 tutakuwa tumemaliza mikongo hii mitatu (3)na nchi yetu itakuwa
tayari kushiriki kwenye biashara ya umeme Kikanda.
Akifafanua
zaidi kuhusu mradi huo wa Kenya-Tanzania Power Interconnection (KTIPIP)ZTK Mhandisi
Kigadye alisema sehemu ya kwanza itahusu ujenzi wa njia za kusafirisha umeme
(transmission lines) na ujenzi wa vituo vya kupozea umeme.
Mradi
mzima una urefu wa kilomita 510 na umegawanyika kwenye sehemu nne, ambazo ni
Isinya Kenya hadi Namanga Kilomita kilomita 96, sehemu ya pili unahusu
Namanga-Arusha Kilomita 114, sehemu ya tatu Arusha-Babati kilomita 150, na
Bababti-Singida kilomita 150.
Kwa
upande wake, Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayehusika na Miradi, Mhandisi
Emmanuel G. Manirabona, alisema tayari vifaa vya kutekeleza ujenzi wa mradi huo
vimewasili kwa kiasi kikubwa cha kazi kuanza.
Akieleza
zaidi Mhandisi Manirabona alibainisha kuwa kila kitu kiko sawa na wananchi wote
ambao wako kwenye sehemu mradi unakopita, tayari Serikali imeshawalipa fidia na
ndiyo maana mkandarasi anaendelea na kazi.
Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayehusika na Miradi, Mhandisi
Emmanuel G. Manirabona, akifafanua mambo mbalimbali yahusuyo utekelezaji wa mradi huo leo Januari 22, 2019
Mratibu wa Mradi huo kutoka
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Peter Kigadye, akifafanua jambo kwa wahariri eneo la ujenzi wa kituo cha kupoza umeme Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha leo Januari 22, 2019
Vifaa viko site tayari
Vifaa viko site tayari
Zege linamwaga kwenye msingi wa kusimika mnara wa kupitisha nyaya za umeme mkubwa
Eneo la ujenzi wa kituo cha kupoza umeme Kisongo.
Mhandisi Peter Kigadye
Mhandisi Peter Kigadye
Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayehusika na Miradi, Mhandisi Emmanuel G. Manirabona (kushoto), akiwa na Meneja Mkazi, Mradi wa Kenya-Tanzania Interconnection Project-Lot2 SBU Power Bouygues ya Ufaransa, Christophe Batholome
Mhandisi Mshauri Mradi wa umeme wa Kenya-Tanzania Interconnection-Lot2(KTPIP-Lot2), Gilles Allard kutoka kampuni ya Intec
Mhariri wa gazeti la Majira, Bw. Imma Mbuguni akizungumza jambo.
Mashimo manne ya nguzo nne za mnara (tower) moja. mafundi wanasubiri kumwaga zegu.
Mafundi wakiwa wamesimama mbele ya moja ya shimo litakalotumika kusimika mnara (tower). Kwa kawaida Mnara mmoja nashikiliwa na nguzo nne, hili shimo ni la kusimika nguzo moja kati ya hizo.
Mhandisi Kigadye akifafanua jambo eneo la uchimbaji na usimikazji minara ambapo kazi ya kumimina zege kwenye mashimo imeanza
Waandishi na wahariri wakinukuu taarifa muhimu eneo la utendaji huko wilayani Monduli.
Mafundi wakiwa kazini.
Vifaa viko site tayari
Vifaa viko site tayari
Zege linamwaga kwenye msingi wa kusimika mnara wa kupitisha nyaya za umeme mkubwa
Eneo la ujenzi wa kituo cha kupoza umeme Kisongo.
Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayehusika na Miradi, Mhandisi
Emmanuel G. Manirabona (kushoto), akimsikiliza Mhandisi Mshauri Mradi wa umeme wa Kenya-Tanzania Interconnection-Lot2(KTPIP-Lot2), Gilles Allard kutoka kampuni ya Intec, kwenye eneo la ujenzi wa kituo cha kupoza na kusambaza umeme kinachojengwa eneo la Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha Januari 22, 2019.
Mhandisi Herini Mhina. Meneja wa TANESCO jijini Arusha. Mhandisi Peter Kigadye
Mhandisi Peter Kigadye
Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayehusika na Miradi, Mhandisi Emmanuel G. Manirabona (kushoto), akiwa na Meneja Mkazi, Mradi wa Kenya-Tanzania Interconnection Project-Lot2 SBU Power Bouygues ya Ufaransa, Christophe Batholome
Mhandisi Mshauri Mradi wa umeme wa Kenya-Tanzania Interconnection-Lot2(KTPIP-Lot2), Gilles Allard kutoka kampuni ya Intec
Mhariri wa gazeti la Majira, Bw. Imma Mbuguni akizungumza jambo.
Meneja Mkazi, Mradi wa Kenya-Tanzania
Interconnection Project-Lot2 SBU Power Bouygues ya Ufaransa, Christophe Batholome(kulia), akibadilishana mawazo na Meneja wa TANESCO jijini Arusha, Mhandisi Herini Mhina, (katikati) na Msimamizi wa ujenzi kutoka Tanesco.
Mashimo manne ya nguzo nne za mnara (tower) moja. mafundi wanasubiri kumwaga zegu.
Mafundi wakiwa wamesimama mbele ya moja ya shimo litakalotumika kusimika mnara (tower). Kwa kawaida Mnara mmoja nashikiliwa na nguzo nne, hili shimo ni la kusimika nguzo moja kati ya hizo.
Mhandisi Kigadye akifafanua jambo eneo la uchimbaji na usimikazji minara ambapo kazi ya kumimina zege kwenye mashimo imeanza
Waandishi na wahariri wakinukuu taarifa muhimu eneo la utendaji huko wilayani Monduli.
Mafundi wakiwa kazini.
No comments:
Post a Comment