Mkurugenzi wa Mfuko wa Khalifa Fund, wenye Makao Makuu ya Nchini Abu Dhabi UAE.Ndg. Nizar Cheniour, akizungumza na Waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar,kwa ziara ya Siku Tatu Nchini Zanzibar.
MKURUGENZI wa Mfuko wa
‘KhalifaFund’ Naizar Cheniour, amesema mfuko huo umeazimia kuwawezesha vijana wa Zanzibar katika nyanja
mbali mbali za kiuchumi ili kuweza kujiajiri na kuinua hali zao za maisha.
Mkurugenzi huyo
amesema hayo leo wakati alipozungumza na
waandishi wa habari, mara baada ya ujumbe wa Mfuko huo ulipowasili katika
Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.
Ujumbe huo upo nchini
kwa ziara maalum, ikiwa ni muendelezo wa mazungumzo na Serikali, yenye lengo la
kufanikisha utekelezaji wa programu mbali mbali katika sekta za biashara,
ujasiriamali, miundombinu na nyenginezo.
Alisema Mfuko umelenga
kuwawezesha vijana wa Zanzibar katika upatikanaji wa rasilimali fedha, utaalamu
na masuala ya kiufundi ili waweze kujiajiri kupitia shughuli za ujasiriamali na
hivyo kuweza kujitegemea.
Aliwataka vijana na Wazanzibari
kwa ujumla kutarajia mafinikio makubwa kutokana na program mbali mbali zitakazotekelezwa kupitia
Mfuko huo.
Alisema mfuko wa
KhalifaFund, una uzoefu mkubwa katika utekelezaji wa programu za maendeleo na
shughuli za kiuchumi, ambapo umekuwa ukifanya kazi hizo katika nchi mbali
mbakli duniani.
Mapema, Katibu Mkuu wa
Wizara ya Biashara na Viwanda,Ndg.Juma Ali Juma alisema ujio wa Viongozi wa Mfuko
wa’ KhalifaFund’ umelenga kukamilisha
mazungumzo yaliofikiwa katika kikao kilichopita ili kuwa tayari kwa utekelezaji
wa yale yalioafikiwa.
Alisema mfuko huo wa
kifedha, wenye makao makuu yake Abu Dhabi ,UAE utatowa msukumo mkubwa katika utekelezaji wa program mbali mbali za
kimaendeleo na kiuchumi, sambamba na kuwawazesha vijana kupitia kazi za
ujasiriamali.
Alisema wakati ukiwa
nchini utakutana na kufanya mazungumzo na taasisi mbali mbali za Serikali
pamoja na kutembelea maeneo tofauti.
Hii ni mara ya pili
kwa viongozi wa Mfuko wa ‘KhalifaFund’ kuja nchini kwa ajili hiyo, ambapo kabla
ulipata fursa ya kutembelea sekta tofauti za maendeleo na kiuchumi Unguja na
Pemba.
Aidha, ujio wa mfuko
huo unafutia ziara ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Dk. Ali Mohamed Shein aliyoifanya Umoja wa nchi za Falme ya Kiarabu (UAE)
Januari mwaka uliopita.
Abdi Shamnah,
Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax:
024 2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment