Naibu Waziri Ofisi ya Makamu
wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima akisalimiana na viongozi wa
Wilaya ya Namtumbo mara baada ya kuwasili Wilayani hapo kwa lengo la kubaini
changamoto za kimazingira na kuweka mikakati ya kuhifadhi Ikolojia ya Vyanzo
vya Maji.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu
wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima akitoka kukagua chanzo cha Maji
cha Mto Luegu kilichopo katika Kijiji cha Ngwinde, Kata ya Litola Wilaya ya
Namtumbo. Chanzo Mto Luegu kinachangia asilimia 19 ya Maji katika Mto Rufiji.
Katika ziara yake Wilayani Namtumbo, Mheshimiwa sima amesisitiza uhifadhi
endelevu katika eneo hilo ili chanzo hicho kisivamiwe kwa shughuli za
kibinadamu.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa
Rais Muungano na Mazingira Mhe. Waziri Mussa Sima akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa
Ruvuma Christina Mndeme vitambulisho maalumu vya wakaguzi wa Mazingira
vilivyotolewa na Ofisi yake kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004. Vitambulisho
hivyo maalumu vitawezesha wakaguzi wa mazingira kutekeleza majukumu yao kifanisi
ikiwa ni pamoja na kusimamia uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira. Makabidhiano
hayo yamefanyika hii leo Mkoani Ruvuma.
Picha na Lulu Mussa.
No comments:
Post a Comment