Meneja Mkuu wa Mkwabi Super Market Kawkab Hussein kulia akizungumza
na Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure kushoto wakati wa ziara yake kwa
walipakodi wanaotumia mashine na EFD na wasiokuwa nazo
ili kubaini changamoto na kuziboresha
Meneja Mkuu wa Mkwabi Super Market Kawkab Hussein kulia
akizungumza na Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure kushoto wakati walipoingia kwenye
duka hilo
Meneja Mkuu wa Mkwabi Super Market Kawkab Hussein kulia
akimuonyesha Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure namna wanavyotumia mfumo wa EFD
Mashine kutoka huduma zao kwa wateja wao kushoto wakati walipoingia
kwenye duka hilo
Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure kulia akimuonyesha Mfanyabiashara
Yusuph Tayabani kitu kwenye risiti wakati wa ziara hiyo
Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure kulia akitoka kwenye mmoja ya duka
ambalo alilitembelea wakati alipowatembelea walipakodi
wanaotumia mashine na EFD na wasiokuwa nazo ili kubaini changamoto na
kuziboresha
Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure katikati akiwa na maafisa wengine
wa TRA mkoani Tanga wakitoka kwa duka la kuuzia gesi wakati wa ziara
hiyo
Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga Specioza Owure |
MAMLAKA ya Mapato nchini (TRA) Mkoani Tanga wamefanya
ziara ya kutembelea walipakodi waliokuwa na mashine za EFD na
wasiokuwa nazo ili kuweza kubaini changamoto zao na kuweza kuboresha
huduma zao.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Meneja wa
TRA Mkoani Tanga Specioza Owure alisema baada ya kutembelea walipakodi
hao wameona wapo walikuwa wanastahili kuwa na mashine za EFD lakini
hawana hivyo kuwaachia barua za kwenda kununua mashine hizo.
Alisema pia wamelazimika kutoa barua za wito kwa baadhi yao ili waweza
kufika ofisi za mamlaka hiyo kwa ajili ya kuona kumbukumbu za mauzo na
manunuzi ili kuona kama wanastahili kwa na mashine za EFD
Meneja huyo alisema kwamba ni muhimu sana kwa wafanyabiashara
kuendelea kutumia mashinde za EFD ikiwemo kuwataka wanunuzi nao kudai
risiti wakati wanapofanya manunuzi.
“Lakini pia
tumewaelimisha walipa kodi athari za kutokutoa risiti na kutokutumia
mashine za EFD na kwamba usipotoa risiti adhabu yake ni milioni tatu
mpaka nne na nusu huku kwa wale wasiodai risiti adhabu yake inaanzia
elfu 30 hadi milioni 1.5 au kifungo kisichozidi miaka mitano”Alisema.
Awali akizungumza katika ziara hiyo Meneja Mkuu wa Mkwabi
Super Market Kawkab Hussein alisema umuhimu wa mashine hizo ni mkubwa
kwani unarahisisha kufahamu mauzo ya siku na pia kuchangia maendeleo
ya nchi .
Hussein alisema pia mfumo huo unawafanya
wafanyabiashara kutokuibiwa kutokana na kila anayenunua bidhaa anapata
risiti na hivyo kuwa rahisi kuweza kujua mauzo ya siku husika lakini
pia kuchangia maendeleo ya nchi.
Hata hivyo alisema kwamba
changamoto kubwa ambayo wanakumbana n ayo ni mtandao wa hizo mashine
wakati mwengine unasumbua lakini pia ni ghali sana inabidi wapunguze
maeneo ya mauzo yao unatakiwa ununua sita au zaidi ya hapo kama
utaboreshwa mfumo vizuri unawasaidia kuweza kutambua mauzo.
Mamlaka hiyo iliwatembelea maduka mbalimbali yakiwemo ya dawa,vituo
cha kuuzia mafuta cha Ratco,Super Marketi ya Mkwabi na maduka ya
kuuza bidhaa za jumla za vyakula.
No comments:
Post a Comment