Na Raya Hamad OR-UUB
Mashirikiano na uaminifu unaendana na
uwajibikaji wa kazi ndio siri ya
mafanikio katika kukuza ufanisi na
kuleta maendeleo endelevu pia kukabiliana
na changamoto zinazoweza kujitokeza mahali popote na wakati wowote hatimae kuwa
na maamuzi sahihi kwa maendeleo na mustakabali mwema wa kazi
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa
Umma na Utawala Bora Mheshimiwa Haroun
Ali Suleiman ameyasema hayo wakati wa makabidhiano kufuatia mabadiliko
yaliyofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dk
Ali Mohamed Shein ambapo Wizara iliyokuwa Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bora imegaiwa mara mbili .
Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala
Bora inaongozwa na Waziri Haroun Ali Suleiman
, Katibu Yakout Hassan Yakout na Naibu Katibu Seif Shaaban Mwinyi kwa upande
wa Wizara ya Katiba na Sheria inaongozwa na Waziri Khamis Juma Mwalim ,
Katibu Mkuu ni George Kazi
Waziri Haroun amesisitiza baadhi ya mambo ya msingi ambayo bado yanahitaji
kusimamiwa ikiwemo Sheria ya Mufti ambayo bado haijakamilika na kusisitiza
kufanyiwa kazi ili kikao kijacho cha Baraza la Wawakilishi iweze kusomwa kwa
mara ya kwanza.
Aidha amemkumbushia Waziri wa Katiba na
Sheria kuwa kwa nafasi yake anakuwa
Mjumbe wa Kamati ya Uongozi ya Baraza la Wawakilishi, Mwenyekiti wa
Kamati ya Kitaifa inayoshughulikia
masuala ya Udhalilishaji, Mjumbe wa Kamati ya Kupambana na Dawa za Kulevya .
Akitoa shukurani zake kwa Watendaji wa
iliyokuwa Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bora Waziri wa Katiba na Sheria inaongozwa na Waziri Khamis Juma Mwalim amesema mashirikiano ya pamoja na uwajibikaji kwa wote ndio siri
ya mafanikio ambayo yamelekea kuleta ufanisi katika kazi katika kipindi chote
kabla ya kugaiwa kwa Wizara
Ndugu Khamis pia amemshukuru Waziri Haroun
na kuelezea kuwa alitumia muda ili kupata ushauri na maelekezo katika masuala
ya kazi , Jimbo na hata familia “
nilifanya hivyo kwani Mwalim Haroun ni mkongwe na ni shina la mti wa mafanikio ambae ana hikima na busara na nashukuru hakuwa
mchoyo kunifahamisha, kuniongoza,
kuniendeleza na kunipa ushauri ”alisisitiza
Ameahidi kudumisha na kuendeleza mshikamano
na viongozi pamoja na wafanyakazi
kushirikiana kufanya kazi kwa pamoja na kutekeleza majukumu yaliyopo na kuandaa
taratibu na mipango imara ya uwajibikaji kwa maslahi ya Taifa
Nae Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria ndugu
George Kazi ameahidi kusimamia mfumo wa Katiba na Sheria na kuahidi
kushirikiana na watendaji na wafanyakazi na kila mmoja kuwajibika ipasavyo
pamoja na kutekeleza na kusimamia vyema Ilani ya Chama Cha Mapinduzi
Akitowa shukurani kwa niaba ya wafanyakazi
na watendaji wote Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali Bi Fatma Moh’d suala la mashirikiano ni muhimu kwa sekta
zote kwani haiwezekani kuwa na utawala bora bila ya kuwa na sheria , Uwazi
na Uwajibikaji “ tunafanya yale ya muhimu na wajibu ili Zanzibar itawalike
hivyo basi nakuahidini tutawakaguwa nyote hata kama tuko nyumba moja kama
sheria na Katiba ya nchi inavyoeleza” alisisitiza
Aidha Katibu wa Mufti Zanzibar Sheikh
Fadhil Soraga ambae nae alitowa wasia mfupi kwa kusema ufanisi hauwezi kupatikana isipokuwa kwa juhudi
kubwa na Taufiq haipatikani isiokuwa kwa Allah hivyo ni wajibu wetu sote
kumuomba sana Mwenyezi Mungu .
Viongozi hao wote kwa pamoja wamemshukuru
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe Dk Ali Mohamed Shein
juu ya namna anavyosimamia Utawala bora na
pia kuwaamini na kuwateuwa kuwa viongozi
katika Taasisi hizo
No comments:
Post a Comment