Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, Awaapisha Viongozui Aliowateua Hivi Karibuni.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimuapisha Katibu Mtendaji wa Tume ya Utangazaji Zanzibar.Ndg. Omar Said Ameir, hafla hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni kushika nyadhifa mbali mbali katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Viongozi walioapishwa na Rais Dk. Shein katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar ni Hamida Mussa Khamis ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Kati Unguja, Khalid Abdalla Omar anaekuwa Naibu Katibu anayeshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ.

Mwengine aliyeapishwa hivi leo ni Omar Said Ameir anaekuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Utangazaji Zanzibar.

Hafla hiyo, ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said, Mawaziri, Manaibu Mawaziri, Makatibu Wakuu, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih.

Wengine ni Mkuu wa  Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib pamoja na Washauri wa Rais wa Zanzibar, viongozi wengine wa Serikali pamoja na wanafamilia.

Mapema wafanyakazi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ofisi ya Faragha ya Rais walimtakia kheri ya siku ya kuzaliwa Rais Dk. Shein  ambaye amezaliwa Machi 13, 1948.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.