Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni
Sanaa na Michezo Bibi.Susan Mlawi akizungumza na wafanyakazi wa Wizara yake Aprili
02, 2019 Jijini Dodoma kuhusu kuboresha utendaji kazi kwa ajili ya maendeleo ya
Taifa.
Na
Shamimu Nyaki -WHUSM
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi.Susan Mlawi amesema
kuwa ujenzi wa Ofisi za Wizara zilizopo Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma zipo katika hatua za mwisho kukamilika na kuwataka watumishi wake kuwa
tayari kuhamia kati ya mwezi wa nne na
wa tano mwaka 2019.
Hayo ameyasema jana Jijini Dodoma wakati wa kikao na Wafanyakazi wa Wizara hiyo kilicho
wapa fursa wafanyakazi hao kiliwakutanisha fursa
ya kujadiliana mambo mbalimbali ya kiutendaji.
“Ni
vyema mkajiandaa na kuwa tayari kuhamia
mji wa Serikali kwakua kwa sasa ofisi zipo katika hatua za mwisho kukamilika na
matarijio yangu ni kwamba kati ya mwezi wanne na wa tano tutakuwa tumehamia rasmi”.alisema
Bibi.Susan.
Aliongeza
kwa kueleza kuwa Wizara imefanya
michakato mbalimbali ya kuhakikisha inawakwamua watumishi wake kiuchumi kwa
kuanzisha SACCOS pamoja na Mfuko wa
kufarijiana wenye lengo la kuwasaidia watumishi katika masuala mbalimbali ya
kijamii .
Aidha Katibu Mkuu huyo amewataka watumishi kufanya kazi kwa ushirikiano na upendo ili
kuleta matokeo chanya katika utendaji, huku akisisitiza kuwa hakuna haki bila
wajibu.
Naye Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu
Bw. Orest Mushi amewataka watumishi hao kufuata na kuzingatia sheria , taratibu
na kanuni za Utumishi wa Umma katika utendaji wa kazi.
No comments:
Post a Comment