Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Hassan Khatib Hassan akitowa shukrani kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, baada ya kumalizika kwa hafla ya Futari aliowaandalia Wananchi wa Kusini Unguja katika Ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa Tunguu Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein amefutari pamoja na wananchi wa Mkoa wa Kusini Unguja na kuwataka waumini
wa dini ya Kiislamu kuzidisha ibada na upendo katika mwezi huu Mtukufu wa
Ramadhani.
Hafla hiyo ya futari iliyoandaliwa
na Rais Dk. Shein kwa ajili ya wananchi wa Mkoa huo wa Kusini Unguja ilifanyika
katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA), Tunguu, Wilaya ya
Kati Mkoa wa Kusini Unguja na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali, dini,
vyama vya siasa pamoja na wananchi wa Mkoa huo.
Akitoa neno la
shukurani kwa niaba ya Rais Dk. Shein, Mkuu wa Mkoa huo Hassan Khatib alisisitiza
kuwa mwezi Mkutukufu wa Ramadhani ni mwezi wa kuzidisha ibada na upendo ikiwa
ni pamoja na kuhakikisha wanaofunga wanapata futari.
Aliongeza kuwa
kuzidisha ibada na upendo katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani ndio njia moja wapo
ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu sambamba na kuufanyia wema mwezi huo ambao una
rehma nyingi ndani yake.
Aidha, alisisitiza
suala zima la amani na utulivu ndio msingi wa maendeleo hivyo kila mmoja
anapaswa kuilinda na kuiendeleza kwa nguvu zake zote.
Alieleza kuwa
maendeleo yote yaliopatikana katika Mkoa huo yanatokana na kuwepo kwa amani, utulivu
na upendo mkubwa ambayo ndio chachu ya mafanikio.
Akitoa neno la
shukurani kwa niaba ya wananchi Mkuu wa Mkoa huyo alimpongeza Rais Dk. Shein na
Serikali anayoiongoza kwa azma yake ya ujenzi wa barabara katika Mkoa huo
ikiwemo barabara ya Charawe na Ukongoroni itakayojengwa kwa kiwango cha lami itakayoanzia
Jozani, ujenzi unaotarajiwa kuanza hivi karibuni.
Sambamba na hayo,
wananchi wa Mkoa huo pia, wamefurahishwa na ahadi ya Rais Dk. Shein aliyoitoa katika
ziara yake aliyoifanya katika Mkoa huo mwezi Februari mwaka huu ya ujenzi wa
daraja kati ya kisiwa cha Uzi na Unguja Ukuu kwa lengo la kurahisisha usafiri
wa barabara hali ambayo itaondosha usumbufu wa usafiri kwa wananchi wa kisiwa
hicho iliyodumu kwa muda mrefu.
Pia, Mkuu huyo wa Mkoa
alieleza kuwa wananchi wa Mkoa huo wameendelea kupata mafanikio makubwa
kutokana na amani iliyopo hatua iliyopelekea kupungua kwa matukio kadhaa mabaya
yakiwemo udhalilishaji wa wanawake na watoto pamoja na kutokuwepo kwa ajili za
barabarani katika kipindi hichi Mkoa humo.
Wananchi wa Mkoa huo
walitoa shukurani kwa Rais Dk. Shein kwa kuendeleza utamaduni wake huo wa
kufutari nao pamoja katika mwezi mtukufu wa Ramadhani na kumuombea dua kwa
Mwenyezi Mungu ili azidi kumpa afya, nguvu na uzima yeye na Aila yake ili
waungane nae tena katika mwezi wa Ramadhani wa mwakani.
Alhaj Dk. Shein
aliwatakia Ramadhani njema wananchi wa Mkoa huo na kuwasisitiza kuutukuza mwezi
huu mtukufu wa Ramadhan kwa kusoma sana Qur-an kwani ndio mwezi ulioshuka
kitabu hicho kitakatifu.
Dk. Shein aliwataka
wananchi wa Mkoa huo kuendelea kushirikiana na kupendana sambamba na kuwa
wamoja na kuwataka kuachama na mambo yote yaliyokatazwa ndani ya mwezi huu na
miezi mengineyo ili waendelee kupata neema za Allah.
Pamoja na hayo, Alhaj
Dk. Shein aliwashukuru wananchi wote waliohudhuria katika futari hiyo aliyowaandalia
na kupongeza jinsi walivyoonesha upendo mkubwa kwake wa kukubali muwaliko wake
huo.
Wakati huohuo, nae Mke wa Rais wa
Zanzibar Mama Mwanamwema Shein kwa upande wake aliungana na viongozi wanawake
wa kitaifa pamoja na wananchi wa Mkoa huo wa Kusini Unguja katika futari hiyo
maalum aliyoianda Rais Dk. Shein.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment