Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimuapisha Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda Zanzibar Ndg. Juma Hssan Juma Reli, hafla hiyo imefanyika leo katika Ukumbi wa Ikulu Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein
leo amewaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni kushika nyadhifa mbali mbali
katika Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Viongozi walioapishwa na Rais Dk. Shein katika
hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar ni Abeid Juma Ali anaekuwa Mkuu wa
Wilaya ya Magharibi ‘’A’’ Unguja. Kapteni Khatib Khamis Mwadini anaekuwa Mkuu
wa Wilaya ya Wete Pemba,
Wengine ni Juma Hassan Reli anaekuwa
Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda na Mwita Mgeni Mwita anaekuwa Katibu
Mtendaji Tume ya Mipango.
Hafla hiyo, ilihudhuriwa na viongozi kadhaa
akiwemo Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd, Spika wa Baraza la
Wawakilishi Zubeir Ali Maulid, Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu ,Mwanasheria Mkuu wa
Zanzibar Said Hassan Said, Mawaziri, Manaibu Mawaziri, Naibu Spika wa Baraza la
Wawakilishi Mgeni Hassan Juma pamoja na Makatibu Wakuu.
Wengine ni Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh
Saleh Omar Kabih, Sheikh Hassan Othman Ngwali Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar,
Sheikh Mahmoud Mussa Wadi Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed
Mahmoud, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib, Washauri
wa Rais wa Zanzibar, na viongozi wengine wa Serikali pamoja na wanafamilia.
Nao viongozi walioapishwa hivi leo
walieleza kuwa uteuzi huo unaashiria kuwa ni uthibitisho unaoonesha kwamba bado
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein
anawaamini katika utekelezaji wa majukumu yao.
Aidha,viongozi hao waliomba ushirikiano
katika taasisi wanazokwenda kuzifanyia kazi ili kufanikisha malengo
yaliokusudiwa katika kuiletea Zanzibar maendeleo pamoja na wananchi wake.
Sambamba na hayo, viongozi hao waliahidi
kusimamia na kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020 ikiwa ni
Dira katika kutekeleza na kusimamia
maendeleo katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar , Kutekeleza Mipango Mikuu
ya Maendeleo ambayo ni MKUZA III, Dira
ya Maenedeleo ya 2020 pamoja na Mpango wa Dunia wa Maendeleo Endelevu.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment