Habari za Punde

Bei ya Mafuta Kutoka ZURA Itaanza Kutumika Kuan zia Kesho 14 -8-2019 Zanzibar.

Na Mwashungi Tahir          Maelezo  
Mamlaka ya udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) imefanya mabadiliko 
ya bei za mafuta zitakazoanza kutumika rasmi kuanzia siku ya Jumatano ya Tarehe 14-08-2019.
Akizungumza na waandishi wa habari huko Ofisini kwake Maisara Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na  Mawasiliano (ZURA) Khuzaimat Bakar Kheir akitoa sababu za mabadiliko ya bei za mafuta kwa Mwezi Agosti 2019 ni kushuka kwa bei za bidhaa hizo katika Soko la Dunia.
Akielezea   aina ya mafuta  kwa upande wa  Petroli bei ya mwezi wa Julai , 2019 lita TSHS 2,338 ambapo bei ya mwezi Agosti , 2019  litaTSHS 2,181 tofauti -157  sawa na asilimia 
6.72%.
Mafuta ya Dizeli bei ya mwezi wa Julai, 2019 lita TSHS 2,319  ambapo bei ya mwezi Agosti , 2019 lita 2,221 tofauti -98 sawa na asilimia 4.23%.
Pia Mafuta ya Taa bei ya mwezi wa Julai, 2019 lita TSHS 1,753 ambapo bei ya mwezi  Agosti, 2019 lita TSHS 1,675 tofauti-78  sawa na asilimia 4.45%.
Vile vile Mafuta ya Meli  Banka bei ya mwezi wa Julai, 2019 lita TSHS 2,145 ambapo bei ya  mwezi  Agosti, 2019 lita TSHS.2,047 tofauti -98 sawa na asilimia 4.57%.
Hivyo Khuzaimat amesema Mamlaka ya udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar ZURA inawajuilisha wananchi kwamba bei zilizotangazwa ndio bei halali na kuanza kutumika rasmi kuanzia siku ya Jumatano tarehe 14-08-2019.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.