STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 10.08.2019
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, amemtumia salamu za
rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk. Kebwe Stephan Kebwe kufuatia ajali ya
kuripuka kwa lori la mafuta na kusababisha vifo pamoja na majeruhi kadhaa.
Katika salamu za rambirambi ambazo Rais Dk. Shein
amemtumia Mkuu wa Mkoa, alieleleza kuwa amemepokea kwa huzuni na masikitiko
makubwa taarifa ya ajalai ya kuripuka kwa lori la mafuta iliyotokea asubuhi ya
leo, tarehe 10 Agosti, 2019 katika maeneo ya Itigi Msavu Mkoani Morogoro na
kusababisha vifo vya Watanzania walatao 60 na majeruhi kadhaa.
Rais Dk. Shein katika salamu hizo alieleza kuwa
yeye binafsi pamoja na wananchi wote wa Zanzibar anatuma salamu za rambi rambi
kwa wanafamilia wa marehemu, marafiki, wananchi wa Mkoa wa Morogoro na Jamahuri
ya Muungano wa Tanzania kwa jumla.
“Kwa hakika msiba huu umetugusa wananchi sote wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuondokewa ghafla na ndugu zetu ambao ni
nguvu ya Taifa” ilieleza sehemu ya taarifa ya Rais Dk. Shein.
Aidha, salamu hizo zilimuomba Mwenyezi Mungu ampe
Mkuu huyo wa Mkoa, wanafamilia pamoja na Watanzania wote moyo wa subira katika
kipindi hichi kigumu cha msiba.
Vile vile katika salamuhizo za rambirambi, Rais
Dk. Shein alimuomba MwenyeziMungu awalaze mahala pema wote na awape nafuu ya
haraka majeruhi wa ajali hiyo ili waweze kupata shifaa na waendelee na majukumu
yao mbalimbali ya ujenzi wa Taifa.
Mapema leo asubuhi lori lililokuwa limebeba shehena
ya mafuta aina ya petroli likitokea Dar-es-Salamu lilipinduka na kuwaka moto
katika eneo la Itigi Msamvu wakati
wananchi wakijaribu kuchota mafuta yaliyomwagika baada ya gari hilo kupata
ajali na kuanguka.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment