Habari za Punde

Mahafali ya Tano ya Darasa la Kiarabu katika Skuli ya Uweleni Pemba

 Wanafunzi wa Darasa la Kiarabu katika Skuli ya Uweleni Pemba , wakiwa katika mahafali ya tano ya Darasa hilo yanayoendesha kwa ufadhili wa Taasisi ya Samael Academy Pemba.
 Mkurugenzi wa Tasisi ya Samael Academy, Sheikh Nassor bin Said (Alrawah) akimvisha Jambia mwanafunzi wa Darasa la Kiarabu katika Skuli ya Uweleni Pemba, katika mahafali ya tano ya darasa hilo.
 Mkurugenzi wa Taasisi ya Samael Academy, Sheikh Nassor bin Said (Alrawah) , akizungumza na Wazazi na Wanafunzi wa Darasa la Kiarabu katika mahafali ya tano huko katika Skuli ya Uweleni Mkoani Pemba.
 Baadhi ya Wanafunzi wa Darasa la Kiarabu la Uweleni linalodhaminiwa na Taasisi ya Samael Academy ilioko Gombani Pemba, wakionesha umahiri wao juu ya somo hilo , ikiwa ni mahafali ya tano ya Darasa hilo.



Baadhi ya Wazazi wa Darasa la Kiarabu katika Skuli ya Uweleni Pemba, wakifuatilia kwa makini nasaha zinazotolewa na Mkurugenzi wa taasisi ya Samael Academy, Sheikh Nassor bin Said (Alrawah) katika hafla ya
mahafali ya tano ya Darasa hilo yaliofanyika katika Skuli ya Uweleni Pemba.


PICHA NA HABIBA ZARALI -PEMBA.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.