JAMHURI YA
MUUNGANO WA TANZANIA
HALMASHAURI YA WILAYA YA TUNDURU
(Barua zote zipitie kwa
Mkurugenzi Mtendaji)
MKOA WA RUVUMA MKURUGENZI MTENDAJI
SIMU NA: 2680004 S.L.P 275,
FAX NA: 2680208
TUNDURU
Barua pepe: info@tundurudc.go.tz
Website: www.tundurudc.go.tz
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
KUKANUSHA
TAARIFA ZA VYOMBO VYA HABARI KWAMBA WANAFUNZI 350 WA WAACHA SHULE KWA UTORO,
MIMBA
Tunduru
30, Oktoba 2019.
Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
mkoani Ruvuma inapenda kukanusha habari ya upotoshaji iliyotolewa na Gazeti la Habari Leo la tarehe 28 Oktoba 2019 na Kituo cha
Televisheni cha ITV ikisomeka kuwa “Wanafunzi 350 waacha shule kwa utoro,
mimba,” habari hii haina ukweli
wowote kama ilivyoripotiwa.
Tunapenda kuuarifu umma kuwa baada ya kuwepo kwa taarifa
hiyo Ofisi ya Mkurugenzi imefanya ufuatiliaji wa kina katika Shule ya Sekondari
Marumba ambayo imetajwa katika habari hiyo iliyosema kuwa wanafunzi 350 wa shule hiyo wameshindwa kuendelea
na masomo kwa sababu ya utoro na mimba kwa kipindi cha miaka minne mfululizo kuanzia mwaka 2016 hadi 2019.
Ni vyema umma ukafahamu kuwa katika kipindi cha miaka minne
yaani 2016 hadi 2019, shule hii ilipangiwa idadi ya wanafunzi 603 ikiwa wavulana
320 na wasichana 283, waliosajiliwa kwa kipindi hicho ni wanafunzi 515 ikiwa
pungufu ya wanafunzi 88 kati ya waliopangwa.
Takwimu zinaonesha kuwa idadi ya wanafunzi waliopo katika
shule ya Sekondari Marumba hadi kufikia tarehe 28/10/2019 ni 345 ikiwa wavulana 208 na wasichana 137
kukiwa na upungufu wa wanafunzi 170.
Akitoa ufafanuzi huo Mkurugenzi Mtendaji Halmasahuri ya
Tunduru Gasper Balyomi amesema hii ni wazi kuwa idadi ya wanafunzi 350 wa sekondari ya Marumba walioripotiwa
hawajulikani walipo hazina ukweli wowote kufuatia takwimu zilizotolewa na
kubaini kuwa:-
1.
Kwa
kipindi cha miaka minne mfululizo jumla ya wanafunzi 20 walihama kwenda katika
shule nyingine.
2.
Wanafunzi
15 waliacha masomo baada ya kupata ujauzito
3.
Wanafunzi
63 waliacha masomo kutokana na sababu mbalimbali
4.
Wanafunzi
72 waliopewa nafasi ya kurudia masomo baada ya kufeli kidato cha pili baadhi yao wazazi waliamua kuwapeleka katika
vyuo vya Ufundi stadi kama (VETA) na shule
binafsi.
Hivyo kufanya jumla ya wanafunzi 170 kwa kipindi cha miaka minne ndio hawapo shuleni tofauti na
taarifa ilivyoonesha jumla ya wanafunzi 350
wa shule hiyo wameacha masomo.
Aidha kuhusu suala la utoro wa reja reja Halmshauri
inaendelea kushirikiana na wazazi pamoja walezi wa wanafunzi katika kuahikisha
utoro mashuleni unadhibitiwa.
Imetolewa na
Kitengo cha Habari na Mawasiliano
Halmashauri ya Tunduru
No comments:
Post a Comment