Habari za Punde

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.Ndg. Salum Maulud Afunga Mafunzo ya Upishi na Ukarimu Zanzibar.

KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ndg. Salum Maulid Salum (kulia) akimkabidhi Cheti Mshiriki wa Mafunzo ya Upishi na Ukarimu Ndg. Rajab Abass Rajab, wakati wa ufungaji wa Mafunzo hayo yaliotolewa na Taasisi ya China National Research Institute of Food&Fermentation Industrieskulia kwa Katibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Mr. Dong Jianhui, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakili Kikwajuni Jijini Zanzibar. Leo
MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya China National Research Institute of Food &Fermantation Industries Mr. Dong Jianhui, akizungumza wakati wa hafla ya ufungaji wa mafunzo hayo ya Upishi na Ukarimu, yaliotolewa na Taasisi yake, hafla hiyo ya ufungaji wa mafunzo hayo imefanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar
Mkuu wa Kitengo cha Uchumi na Biashara wa Ubalozi Mdogo wa Jamhuri ya Watu wa China aliyepo Zanzibar  Bibi Shen Qi alieleza kuwa hatua hiyo ni miongoni mwa juhudi za kuendeleza uhusiano na ushirikiano wa kihistoria uliopo baina ya pande mbili hizo.
WANAFUNZI wa Mafunzo ya Upishi na Ukarimu wakifuatilia hafla hiyo ya ufungaji wa mafunzo yao katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar
WASHIRIKI wa Mafunzo ya Ukarimu na Mapishi wakionesha kwa vitendo jinsi mafunzo hayo waliyoyapata kupitia Taasisi ya China National Research Institute of Food &Fermentation Industries, wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar
WASHIRIKI wa Mafunzo ya Ukarimu na Mapishi wakionesha kwa vitendo jinsi mafunzo hayo waliyoyapata kupitia Taasisi ya China National Research Institute of Food &Fermentation Industries, wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar
KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ndg. Salum Maulid Salum akihutubia wakati wa ufungaji wa Mafunzo ya Upishi na Ukaramu yaliotolewa na Taasisi kutoka China National Research Institute of Food &Fermentation Industries, hafla hiyo ya ufungaji wa mafunzo hayo imefanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar
 





MSHIRIKI wa Mafunzo ya Upishi na Ukarimu yaliotolewa na Taasisi ya China National Research Institute of Food &Fermentation Industries, akitowa neno la shukrani kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo yaliowashirikisha Wanafunzi kutoka katika Taasisi za Serikali na Binafsi yaliochukuwa wiki nne.wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.


WASHIRIKI wa Mafunzo ya Upishi na Ukarimu yaliotolewa na Taasisi ya China National Institute of Food & Fermentation Industries, wakiwa katika picha ya pamoja na Vyeti vyao baada ya kukabidhiwa na kufunga mazunzo hayo katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.