Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akijibu suala wakati wa mahojiano na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Zanzibar Ndg,Chande Omar Omar yanayohusu miaka tisa ya Uongozi wake,katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo.[Picha na Ikulu.]02/11/2019.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein ameeleza kuridhishwa na mafanikio makubwa yaliopatikana
Zanzibar chini ya uongozi wake wa Serikali ya Awamu ya Saba ambao umetimiza
miaka tisa.
Rais Dk. Shein
aliyasema hayo leo Ikulu mjini Zanzibar wakati alipofanya mahojiano na
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Zanzibar (ZBC) Chande Omar Omar kufuatia
kutimiza miaka tisa ya uongozi wake wa kuiongoza Zanzibar.
Katika maelezo yake
Rais Dk. Shein alisema kuwa anafurahia miaka tisa ya uongozi wake kutokana na
mafanikio makubwa yaliopatikana hapa Zanzibar ambayo kwa kiasi kikubwa
yametokana na kutekeleza mambo ya msingi ikiwemo kutekeleza Ilani ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka
2010-2015 na 2015-2020.
Aliongeza kuwa
Serikali inatakiwa baada ya kumaliza uchaguzi wake chama kilichoingia
madarakani kinatakiwa kutekeleza ahadi zake jambo ambalo ndilo lililofanywa na
Serikali anayoiongoza ambayo imetekeleza kwa kiasi kikubwa ahadi ilizoahidi
ndani ya kipindi cha miaka tisa ya uongozi wake.
Aidha, Dk. Shein
alisema kuwa amefurahi kuona kwamba katika uongozi wake mafanikio makubwa
yamepatikana katika utekelezaji wa MKUZA II alioanza nao na MKUZA III
unaondelea hivi sasa.
Alieleza ni kuendeleza
Alieleza kuwa Serikali anayoiongoza imeendeleza umoja na mshikamano mkubwa wa
wananchi wa Zanzibar kwa kutambua kuwa bila ya kuwepo kwa umoja na mshikamano huo
hapatakuwa na maendeleo endelevu.
Alisisitiza kuwa azma
ya CCM ni kutekeleza umoja na mshikamano na ndio maana katika kipindi chote cha
uongozi wake wa miaka tisa ulinzi na usalama wa nchi na wananchi wa Zanzibar
umeimarika.
Alieleza kuwa Serikali
zote mbili ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar zinaendelea kusimamia amani na usalama uliopo nchini na kusisitiza
kuwa ndani ya miaka tisa ya uongozi wake nchi imekuwa salama.
Rais Dk. Shein alieleza
kuwa sekta nyingi za maendeleo zimeimarika katika kipindi cha miaka tisa cha
uongozi wake ulinzkatika katika uongozi
wake Serikali imetekeleza kwa kiasi kikubwa shughuli za kijamii zikiwemo huduma
za afya, elimu, suala zima la kuangalia hali za wananchi pamoja na shughuli za
maendeleo zimeimarika.
Alisema kuwa kila
sekta imeweza kupata mafanikio makubwa sana na kueleza kuwa anajivunia kwa
kiasi kikubwa mafanikio hayo yaliofikiwa katika kutekeleza Ilani ya CCM ya
mwaka 2010-2015 na 2015-2020 pamoja na MKUZA II na MKUZA wa III.
Rais Dk. Shein ambaye
pia, ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar alieleza kuwa wananchi wataendelea
kuiunga mkono CCM kutokana na juhudi zake za maendeleo ukuaji uchumi
uliopatikana nchini.
Rais Dk. Shein
aliwataka wananchi kuhakikisha huduma na miundombinu iliyofanywa na Serikali wanaitunza
na kuitumia vizuri.
Alieleza umhimu wa
kuongeza bidii ili uchumi uendelee kukua kwa kasi na nguvu zaidi ambapo
alipoingia madarakani kasi ya ukuaji ilikuwa asilimia 4.3 na sasa ni asilimia 7.1,
ukuaji huo umetoa mwelekeo vizuri wa kuweza Zanzibar kufikia nchi ya uchumi wa
kati ifikapo mwaka 2020 huku akieleza dhamira yake kwa kipindi kilichobakia
atafanya jitihada ya kuhakikisha kasi ya ukuaji uchumi inafikia asilimia 7.5 mnamo
mwezi Juni mwakani.
Alieleza kuwa kwa
upande wa mfumko wa bei umepungua kwani ulikuwa asilimia 6.1 alipoingia
madarakani na hivi sasa umefikia
asilimia 3.9 jambo ambalo linaleta utulivu katika mwenendo wa biashara.
Alisema kuwa katika
kipindi chake juhudi kubwa zimechukuliwa katika ujenzi wa miundombinu ya barabara,
ujenzi wa skuli za kisasa katika ngazi zote zikiwemo za Maandalizi, Msingi na Sekondari.
Alifahamisha kwamba
Skuli 13 za ghorofa zizmejengwa zikiweko 9 kutoka Mkopo wa Benki ya Maendeleo
ya Afrika na skuli tatu kutoka kwa Washirika wa maendeleo na moja aliyojengwa
na mwananchi mzalendo Said Salim Bakhresa.
Alisema kuwa huduma za
afya kwa upande wa Zanzibar zimeimarika kwa kiasi kikubwa ikilingalishwa na
nchi nyengine za bara la Afrika na hata nje ya bara hilo.
Pia, alieleza jinsi Hospitali
za Zanzibar zilivyopandishwa daraja sambamba na kuanzishwa kwa utoaji wa huduma za usafishaji figo,
saratani na nyengine za afya.
Alisema kuwa vituo vya
afya vina kidhi mahitaji ya wananchi na mgonjwa haendi zaidi ya masafa ya kilomita
5 ya sehemu anayoishi kwa ajili ya kufuata huduma hizo.
Alifahamisha kwamba
alipoingia madarakani kulikuwa vituo 135 na hivi sasa kuna vituo 160 Unguja na
Pemba ambapo pia, sekta nyengine za maendeleo kama vile kilimo, uvuvi nazo zimeimarika huku akieleza
kuwa tayari meli mpya na kubwa ya uvuvi imeshawasili Zanzibar.
Kuhusua suala la
uimarishajai wa sekta ya utalii alisema kuwa mafanikio makubwa yamepatikana
katika sekta hii ambapo lengo lililobainishwa na Ilani la kupokea watalii 500,000
ifikapo mwaka 2020 tayari limeshafikiwa kabla ya wakati huo na kubainisha
kwamba mwaka jana Zanzibar ilipokea watalii 52,0809.
Alibainisha kwamba
hivi sasa kumekuwa na ongezeko la Mashirika ya kigeni kuleta wageni Zanzibar
kutoka nchi mbali mbali ikiwemo Urusi na Mataifa mengine ya Ulaya Mashariki na
kueleza matumaini yake kwamba Zanzibar inaweza kupokea watalii 700,000 ifikapo
mwaka 2020.
Alieleza kuwa kuwepo
afya bure, elimu bure sambamba na kuwepo kwa miasingi ya utawala bora na haki
za binaadamu ikiwemo uhuru wa kuabudu na kuwepo kwa uvumilivu wa dini hapa
Zanzibar.
Hata hivyo, alieleza
changamoto zilizopo ikiwemo suala zima la ajira ambapo tayari serikali imeweka
miakati ikiwa ni pamoja na kuweka mifuko maalum ukiwemo ‘Mfuko wa kuwaewezesha
kiuchumi wajasiriamali’ pamoja na ‘Mfuko wa
vijana’ ambapo kwa upande wa ‘Mfuko wa Vijana’ tayari Bilioni 46
zimetengwa.
Alieleza imani yake
kwa wananchi kuwa wataendelea kuichagua CCM, na ameridhika kwamba Serikali
anayoiongoza inafanya vizuri katika kuwatumikia wananchi ambapo na wananchi
wenyewe wameridhika na uongozi wa Serikali yao ya Zanzibar.
Alieleza kuwa
changamoto zipo na fedha hazitoshi lakini juhudi za makusudi zinaendelea
kuchukuliwa na Serikali kwani hata hivyo, uwezo haujafikiwa asilimia 100 na
kueleza kasi ya Mapinduzi ya kuwaweka wananchi katika mazingira bora ipo kwani
miji 20 itajengwa sambamba na ujenzi unaondelea wa miradi kadhaa.
Rais Dk. Shein
aliendelea kusisitiza kuwa amani na utulivu ndio suala muhimu katika maendeleo
ya Zanzibar hatua ambayo imemfanya abuni mradi wa ‘Zanzibar Salama’ ili usalama
uimarike sambamba na kuimarika kwa sekta ya utalii na mazingira yake.
Alifahamisha kwamba
hivi sasa utegemezi wa Bajeti ya Serikali umepungua kutoka asilimia 30.2 mwaka
2010 hadi asilimai 6 hivi sasa hali ambayo imechangiwa na juhudi kubwa
zilizochukuliwa katika kuimarisha ukusanyaji wa mapato.
Alisema kwamba misaada
inayopatikana kutoka kwa wahisani
inatumika zaidi kwa miradi ya maendeleo.
Alisema kuwa Serikali
inakusanya kwa mwezi TZS Bilioni 67 kwa mwezi ambapo mwaka 2010 Bilioni 13.5 na
kuweza kuvuka lengo la Ilani ya CCM hatua ambayo imepelekea kununua vifaa kadha
vikiwemo vya barabara, vifaa vya uchunguzi wa afya, dawa za kila aina na
kupelekea kuwepo kwa afya bure na elimu bure.
Kwa upande wa suala
zima la uzalilishaji wa wanawake na watoto, Rais Dk. Shein alisema kuwa
Serikali inapiga vita na imeweka sheria kali katika kupambana na vitendo hivyo
sambamba na dawa za kulevya, rushwa na maadili ya viongozi.
Pia, Rais Dk. Shein
aliendelea kusisitiza kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar utadumisha na
yeye na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Johm Pombe Magufuli
watausimamia vyema.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment