Habari za Punde

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Mihayo Akabidhi Vifaa Saidizi Kwa Watoto Wenye Ulemavu Zanzibar.

Naibu Waziri wa nchi ofisi ya Makamo wa pili wa Rais Mihayo Juma Nhunga akikabidhi visaidizi kwa wazee wa watoto wenye mahitaji maalum katika hafla iliyofanyika migombani katika ofisi ya idara ya watu wenye ulemavu Zanzibar.

Na Ali Issa- Maelezo Zanzibar    20/11/2019.w
Naibu Waziri Wanchi Ofisi ya Makamu wa Pili Wa Rais Mihayo Juma Nhnunga amesema Visaidizi vilivyo tolewa kwa watoto wenye ulemavu ndio dhamira ya Serikali kuona kuwa walemavu wanasaidiwa ili kuwawezesha katika shughuli zao za kimaisha likiwemo suala zima la elimu.
Ameyasema hayo leo huko migombani zanzibar wakati akikabidhi vifaa hivyo kwa watoto hao katika  hafla maalumu iliofanyika hapo.
Amesema Serikali imepeleka Madaraka mikowani ili kuona suala la kupatiwa huduma wananchi liwe jepesi na ukaribu.
Amesema vifaa waliopewa watoto hao nimuafaka kwani vitawarahisishia mambo yao.
"Sheria za Manispaa zinaeleza kuwa kupewa misaada wananchi kwa kuwasaidia ni moja ya jukumu lao"alisema Naibu Waziri.
Aidha alimesema watoto wenye ulemavu hupata tabu  wakati wakifuatilia masomo yao katika masafa marefu jambo ambalo huwalazimu wazazi kuwabeba na kuwafikisha sehemu husika  .
Aidha alisema utowaji wa visaidizi hivyo vitawafanyia  wepesi wazazi wa watoto kwa kuwafikisha skuli kwa wakati na kuweza kufikia malengo waliojiwekea .
Naibu huyo aliwataka wazazi na walezi kuvitunza  vifaa hivyo ili viweze kudumu kwa  muda mrefu na vinapo haribika kufanyiwa matengenezo.
Nae Afisa wa Halmashauri za Wilaya ya Magharibi "A" Yumna Ali Mwinjuma alisema msaada huo  utakuwa endelevu kwa watoto wengine wenye  mahitaji maalum.
akizungumza kwa niamba ya wazazi wenzake Juma Suleiman alisema kuwa visaidizi hivyo vimekuja wakati muafaka na watavitumia kwa dhamira iliokusudiwa ikiwa ni pamoja na kuwapelekea skuli watoto wao wanaotoka masafa ya mbali.
 “Shukurani kubwa kwetu kwa kupata wepesi kwani tulizowea kuwabeba watoto kuwapeleka sehemu tofauti za elimu na shughuli za kijamii “alisema Mzee huyo.
Visaidizi  hivyo vimetolewa kwenye wilaya ya magharibi A na B kwa lengo la kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum kwa kukuza kiwango cha elimu nchini.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.