Kwa
miaka kadhaa Serikali za duniani kote zimekuwa zikipigania haki za watoto na
haki za binaadamu pamoja na kuweka vipaumbele muhimu ambapo taasisi za kijamii na za kimataifa zimekuwa zikiainisha mahitaji ya makundi maalum katika jamii zinazohitaji
huduma muhimu na za kipekee ili kulinda ustawi wa watoto.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe
Khamis Juma Mwalim ameeleza hayo wakati
akiwasilisha mada kuhusiana na haki za watoto kwenye mkutano Mkuu wa 20 wa
Majaji wa Dunia unaofanyika katika ukumbi wa Lucknow nchini India.
Amesema makundi ya Watoto yanakabiliwa
na matukio tofauti ya ukatili, kushindwa
kupata haki zao kutokana na kudhulumiwa kiakili, kiwiliwili na kimaadili pamoja
na kukosa kupata mahitaji yao ya msingi.
Ameeleza kuwa matatizo hayo yanachangiwa
kwa kukosekana ufahamu dhidi ya ulinzi wa haki ya watoto, muhali, aibu na
vikwazo katika familia zenye migogoro kwa misingi ya Imani na kukosa msaada wa uchumi wa familia.
Waziri
khamis amefahamisha kuwa kuna haja ya kuanzisha utaratibu maalum wa kupambana
na unyanyasaji wa aina zote dhidi ya watoto kupitia sheria ya kimataifa
inayolinda watoto itakayotekelezwa duniani kote.
“Ukatili dhidi ya watoto uko kila mahali duniani
ndio maana sababu dunia inapaswa kuungana pamoja katika kupigania na kulinda
ustawi wao na kuunda sheria na mifumo madhubuti ya kukabiliana na ukiukwaji wa
haki za watoto.”
Ameongeza
kuwa ana Imani kuwa Mkutano huu, umedhamiria kushawishi dunia kuwafanya watoto
kuwa huru dhidi ya ubaguzi wa wanaotendewa pamoja na kuwanusuru na majanga
yanayotokana na vurugu.
Bunge
moja la dunia linahitajika kwa lengo la kulinda watoto,vizazi vijavyo na jamii
kwa ujumla dhidi ya vita vinavyoendelea katika nchi mbalimbali pamoja na matishio ya ugaidi.
Amesema Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na Tanzania imeridhia mikataba mbali mbali na matamko kadhaa ya kimataifa ya kulinda haki za mtoto
Kutokana
na mikataba hio Zanzibar imeweka sera mbali mbali na sheria zinazoendana na
mikataba hiyo na kutolea mfano sheria ya mtoto ya mwaka 2011, Sheria ya elimu
ya mwaka 1982 na sheria ya adhabu ya mwaka 2018 ambazo kwa pamoja amesema
zimeelezea haki zote za msingi za mtoto na ulinzi wake .
Akiifafanua haki ya kupata elimu Waziri Khamis amesema imepewa umuhimu wa kipekee na ndio maana sera ya elimu na afya ya Zanzibar zinaeleza kuwa elimu bila malipo na matibabau ya Afya bure kwa kila mtoto na wananchi kwa ujumla
Aidha ameilezea sheria ya kazi ya mwaka 2005 inayomlinda mtoto na ajira za utotoni pamoja na kuelezea namna Zanzibar inavyochukulia suala la mtoto kwa umakini mkubwa na ndio maana imewekewa Wizara maalum
Aidha Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Kazi ya mwaka 2005 kwa pamoja sheria hizi mbili zinakataza aina mbaya zaidi ya ajira kwa watoto na inakataza mtoto chini ya umri wa miaka 18 kuajiriwa kwenye mgodi, kiwanda au kama wafanyakazi kwenye meli au mtu mwingine yeyote, ambapo hali za kazi zinaweza kuzingatiwa kuwa hatari.
Wizara ya Kazi,
Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Wazee, Wanawake na Watoto inasimamia haki za
watoto, inashughulikia changamoto zinazowakabili vijana na watoto, kukuza
mazingira mazuri ya utunzaji bora na ustawi wa watoto na pia kutunza watoto
yatima.
Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar imefanya jitihada za makusudi katika kukuza haki za watoto kwa kuanzisha dawati
maalum linaloitwa jinsia na watoto kwa wahanga wa unyanyasaji wa watoto na
unyanyasaji wa kijinsia ambayo yapo katika vituo vya polisi
Hivi
karibuni , Baraza la Mwakilishi wa Zanzibar limetunga Sheria ya Msaada wa
Sheria Namba 13 ya 2018 ambayo hutoa kwa urahisi ulinzi wa haki za watoto
kupitia huduma za bure za Msaada wa Kisheria.
Katika
kufanikisha azma ya Mkutano huo amesema
ulimwengu unahitaji kuwa huru usio na ubaguzi dhidi ya watoto na uhuru
kutokana na janga la vita, hivyo kuna haja ya kuanzisha utaratibu maalum wa
kupambana na unyanyasaji wa aina zote dhidi ya watoto kupitia sheria ya
ulimwengu inayotekelezwa kwa watoto ambayo inaweza kutekelezwa kila mahali kote
ulimwenguni.
Waziri Khamis amewasilisha mada inayozungumzia kuunganisha
ulimwengu kwa watoto kupitia sheria zinazotekelezeka za ulimwengu na utawala
bora na amemalizia kwa kusisitiza kuimarishwa kwa Amani, ulinzi na
usalama na maendeleo endelevu kwa ajili
vizazi vijavyo
Katika
mkutano huo Zanzibar inawakilishwa na
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Khamis
Juma Mwalimu akiwa ameongozana na Jaji Mkuu
Mhe Omar Othman Makungu, Mtendaji Mkuu wa Mahakama ndg Kai Bashiru na
Mrajis wa Mahakama Kuu Zanzibar Ndg. Mohamed Ali Shein.
No comments:
Post a Comment