Na Mwashungi
Tahir Maelezo 23-12-2019.
Mkurugenzi Mtendaji Kamisheni ya Maafa Ndg.Makame Khatib Makame
amesema elimu kwa watu wenye ulemavu wa
kusikia wanahitaji kupewa mafunzo ya lugha za alama ili waweze kujinusuru pale
wanapofikwa na tatizo.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Ulemavu
Abeida Rashid huko kwenye Ukumbi wa Tume
ya Uchaguzi ulioko Maisara wakati wa kufunga mafunzo ya Lugha ya Alama kwa walemavu wa kusikia.
Amesema elimu hiyo ni ya lazima kupatiwa watu hao kwa lengo
la kukuza lugha ya alama na kuweza kutumika kwenye jamii na kuwalinda ili wanapofikwa
na madhara na waweze kufahamika.
Pia amesema mafunzo hayo
yanatoa mwanga kwa kuweza kuelewa ili kutoa ushahidi mahakamani pale watu
hao wanapofikwa na vitendo viovu hasa
vitendo vya udhalilishaji ambavyo vimekithiri nchini.
“Mafunzo haya ya lugha ya alama
nakutakeni muyatumie vizuri ili muweze kutoa huduma kwa watu wenye ulemavu wa
kusikia pale wanapofikwa na vitendo viovu ikiwemo vya udhalilishaji hasa
panapotakiwa kutolewa ushahidi”, alisema Mkurugenzi huyo.
Aidha amesema Serikali
inaangaliya fursa kutoa lugha za alama na imekuwa na sasa inatumika sehemu
nyingi ikiwa sehemu za mikutano, katika
Baraza la Wawakilishi na sehemu
nyingi zinazotumiwa na jamii.
Hata hivyo aliwaomba watoaji wa
mafunzo kukamilika kwa mafunzo hayo
isiwe mwisho bali iwe endelevu yazidi
kuendelezwa na kutoa mafanikio zaidi.
Nae mwanafunzi wa mafunzo hayo Fatma Said Khamis akisoma risala ameitaka Serikali ione umuhimu
wa kutupatia mafunzo ya ulemavu wa kusikia
ili kuweza kuhudumia jamii na kuisaidia wanapofikwa na matatizo.
Amesema wanaomba mafunzo
hayo yawe endelevu kwa Serikali na
binafsi ili waweze kutumia taaluma kwa watu wenye ulemavu wa kusikia kwa
kuhakikisha wanapatiwa haki zao.
Pia amesema wameweza kufarijika kwa kupatiwa mafunzo hayo
ya lugha za alama na kupata muamko wa kutoa huduma kwa jamii.
Hivyo wameishukuru Ofisi ya
Makamo wa Pili wa Rais na Idara ya Watu wenye Ulemavu kwa kuwapatia mafunzo hayo
ambayo watayafanyia kazi na kuwa walimu kwa wenzao.
Kwa upande wake mshiriki wa
dawati la jinsia Mkoa wa Kaskazini Unguja Salum
Khamis Machano amesema mafunzo
haya ya lugha za alama kwa watu wenye ulemavu wa kusikia yataweza kuwasaidia
hususan wahanga wanaokumbwa na vitendo vya udhalilishaji.
Mafunzo hayo ya siku kumi
yamewashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo
Jeshi la Polisi,Mahkama,Wanasheria na Dawati la Udhalilishaji.
No comments:
Post a Comment