Mkurugenzi Mkaazi wa Benki ya Dunia nchini Bi
Bella Bird akizungumza wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya Hali ya Umasikini
Tanzania Bara uliofanyika jijini Dodoma ambapo amesema Benki ya Dunia
itaendelea kushirikiana na Tanzania katika jitihada zake za kujiletea maendeleo
ikiwemo kupambana na umasikini
Waziri
wa Biashara na Viwanda Innocent Bashungwa akihutubia wakati wa kuzindua Ripoti
ya Hali ya Umasikini Tanzania Bara uliofanyika jijini Dodoma. Bashungwa
ameeleza kuwa ripoti hii imechambua kwa kina hali ya umasikini nchini na kutoa
dira ya kukabiliana na umasikini na hatimaye kufikia Malengo Endelevu ya Dunia
ya “Hakuna Umaskini duniani ifikapo mwaka 2030”
Baadhi
ya wadau wa Takwimu waliohudhuria uzinduzi wa Ripoti ya Hali ya Umasikini Tanzania
Bara uliofanyika jijini Dodoma wakifuatilia uwasilishwaji wa matokeo ya ripoti
hiyo.
(Picha na
Ofisi ya Taifa ya Takwimu)
Mkurugenzi Mkaazi wa Benki ya Dunia nchini Bibi Bella
Bird amesema anakubaliana na hoja kuwa mustakabala wa ajira na ukuaji wa uchumi
jumuishi kwa Tanzania uko kwenye maendeleo ya sekta ya kilimo.
Bi Bella Bird alisema hayo wakati akifunga mjadala kuhusu
Ripoti ya Tathmini ya Umasikini Tanzania Bara ambao uzinduzi wake uliofanywa na
Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa katika hoteli ya Morena jijini
Dodoma.
Mkurugenzi huyo wa Benki ya Dunia alieleza kuwa mabadiliko
yanayoendelea hivi sasa katika sekta hiyo ni muhimu kuhakikisha kuwa yanapewa
kila aina ya uwezeshaji ili kilimo kiweze kuchukua nafasi yake katika uchumi wa
nchi na kupunguza umasikini.
“Vijana wengi hivi sasa wameamua kujiunga na kuwekeza
katika sekta ya kilimo na huko wakileta ubinifu mkubwa ikiwemo kutumia njia za
kisasa za kilimo pamoja uchakataji wa mazao ya kilimo kuongeza thamani”
alieleza Bi Bella Bird.
Aliongeza kuwa kinachotakiwa ni kuongeza jitihada za
kuweka mazingira mazuri kuvutia uwekezaji katika sekya hiyo huku akitambua
jitihada za serikali za kuimarisha miundombiu maeneo ya vijijini na kusambaza
umeme vijijini ambayo amesema ni miongoni mwa vivutio vya uwekezaji katika
sekta hiyo.
Hata hivyo, alieleza kuwa suala la huduma za kifedha
kwa wakulima bado ni kitendawili pamoja na kuwa jitihada zimekuwa zikifanyika
lakini bado hapajawa na namna bora ambayo inaweza kuwasaidia vyema wakulima
kujiendeleza kiuchumi.
Geoffrey Kirenga mmoja wa wachanbuzi wa Ripoti hiyo alieleza
kuwa kuingia kwa makampuni ya ngazi ya kati katika sekta ya kilimo kumechochea
mabadiliko makubwa yanayoendelea kutokea katika sekta hiyo hivi.
“kuingia kwa makampuni hayo mbali ya mitaji
inayoingizwa lakini kunaifanya sekta ya kilimo kufaidika na utaalamu, ujuzi na
uzoefu wa sekta binafsi hivyo kuleta mabadiliko tunayoyaona hivi sasa katika
sekta hii” alibainsha Kirenga.
Kirenga ambaye ni Mkuu wa Taasisi ya Southern
Agriculture Growth Corridor alitoa wito kwa watunga sera nchini kuhakikisha
kunakuwepo mazingira mazuri zaidi ya kuvutia watu wengi zaidi kuingia katika
kilimo.
Mbali ya makampuni ya ngazi ya kati, Kirenga alieleza
pia kuwa wako pia watu wengi wa mijini ambao hivi sasa wanajishughulisha kilimo
na wote hao wanasaidia wakulima vijijini
kujifunza toka kwao na wao kujiendeleza.
Katika
hotuba yake ya ufunguzi waziri Bashungwa
alieleza kuwa ripoti hiyo imechambua kwa kina hali ya umasikini nchini na kutoa
dira ya kukabiliana na umasikini na hatimaye kufikia Malengo Endelevu ya Dunia
ya “Hakuna Umaskini duniani ifikapo mwaka 2030”
No comments:
Post a Comment