Kaimu Mkuu wa Kanda
ya Kati wa Shirika la Viwango Tanzania, Bi. Salome Emmanuel, akiwaonesha
waandishi wa habari bidhaa zisizokidhi viwango na kuisha muda wake wa
matumizi wakati wa zoezi la uteketezaji
wa bidhaa hizo lililofanyika leo Januari 16, 2020 katika dampo la Chidaya Jijini Dodoma.
Na
Mwandishi wetu
Shirika la Viwango
Tanzania (TBS) limeteketeza bidhaa zenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa
kukosa kukidhi ubora.
Akizungumza wakati wa
zoezi la uteketezaji wa bidhaa hizo zikiwemo vipodozi, vyakula na vinywaji, Kaimu
Mkuu wa Kanda ya Kati ya Shirika hilo Bi. Salome Emmanuel amesema kuwa baadhi
ya bidhaa zilizoteketezwa ni zile ambazo muda wake wa matumizi umekwisha na bado
wafanyabiashara wasio waadilifu walikuwa wakiendelea kuziuza.
“Ukaguzi tuliofanya
kati ya mwezi Oktoba na Desemba 2019 katika mikoa ya Dodoma na Singida
umetuwezesha kubaini bidhaa hizi ambazo baadhi ya bidhaa zizisokidhi viwango na
nyingine muda wake wa matumizi umekwisha lakini bado wafanyabiashara wasio waaminifu wamekuwa wakiendelea kuziuza”
alisisitiza Bi. Solome
Akifafanua Bi. Solome
amesema kuwa Shirika hilo litaendelea kufanya ukaguzi mara kwa mara ili
kuhakikisha kuwa bidhaa zilizopo sokoni zinakidhi vigezo kwa mujibu wa sheria.
Aliongeza kuwa wananchi
wana jukumu la kushirikiana na shirika hilo katika kuhakikisha kuwa wafanyabiashara
wasio waadilifu hawafanikiwi kuuza bidhaa ambazo muda wake umekwisha na ambazo
hazikidhi vigezo.
Aidha, aliwataka
wafanyabiashara wote kuzingatia sheria na kanuni pale wanapotaka kuingiza
bidhaa hapa nchini na hata wale wanaofanya uzalishaji hapa nchini.
Kwa upande wake mkaguzi
wa Chakula waShirika hilo Bw. AbelDeule amesema kuwa
Shirika hilo linaendelea kuhakikisha kuwa
wananchi wanalindwa dhidi ya bidhaa zisizo na ubora na zile ambazo muda wake wa
matumizi.
Shirika la Viwango
Tanzania (TBS) limekuwa likifanya ukaguzi wa mara kwa
mara ili kuhakikisha kuwa bidhaa zinazoingia nchini zinakidhi vigezo .
Sehemu ya bidhaa
zilizokamatwa kwenye zoezi la kubaini bidhaa zilizoisha muda wa matumizi zikiwa
tayari kuteketezwa leo Januari 16, 2020 katika Dampo la Chidaya Jijini Dodoma.
Oparesheni hiyo imefanikiwa kukamata bidhaa zenye thamani ya shilingi
milionikumi.
Mtambo maalum
unaotumika kuteketeza taka na bidhaa katika dampo la Chidaya Jijini Dodoma ukiendelea
na kazi ya kuteketeza bidhaa zilizoisha muda wa matumizi zilizokamatwa kwenye
zoezi lililoendeshwa na Shirika la Viwango Tanzania kwenye mikoa ya Dodoma na
Singida kati ya mwezi Oktoba na Desemba 2019.
No comments:
Post a Comment