Habari za Punde

JESHI LA POLISI LASEMA KILA MMOJA ASUBIRI UCHUNGUZI WA WATAALAM UKAMILIKE NDIPO TAARIFA ITATOLEWA NA MAMLAKA HUSIKAA


                                                                   04/02/2020

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ndugu waandishi wa Habari,
Nimekuwa nikipokea simu nyingi kutoka kwa watu mbalimbali wakiuliza maendeleo ya  uchunguzi wa tukio la watanzania wenzetu 20 waliopoteza maisha huko Mkoani Kilimanjaro baada ya kukanyagana kwenye hitimisho la kongamano la ibada ya maombi tarehe 01.02.2020 na hatma ya  waliokuwa wakishikiliwa na Jeshi la polisi.

Kama ilivyokwisha kuelezwa na viongozi mbalimbali na kwenye taarifa yangu kwenu ya tarehe 03.02.2020 hatua mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa ni kwamba baada ya tukio hilo Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Nyakoro Sirro (IGP) alituma timu ya maofisa wakiwepo wataalamu wa Uchunguzi wa Sayansi ya Jinai kwenda kuungana na timu ya wataalamu kule Kilimanjaro katika uchunguzi.

Ndugu waandishi wa habari,
Katika uchunguzi huo walikamatwa watu nane (8) akiwepo Bonifase Mwamposa na kuhojiwa kwa kina na baada ya kujiridhisha na yale yaliyokuwa yanahitajika kutoka kwao wamepewa dhamana kwa mujibu wa sheria ili waendelee kuripoti wakati uchunguzi ukiendelea.

Uchunguzi bado unaendelea na baada ya kukamailika yatakayobainika yatatolewa kwa mamlaka husika na kutelekezwa kwa mujibu wa sheria kanuni na taratibu. Hivyo kila mmoja anatakiwa awe na subira na uchunguzi unaofanywa na wataalam utakapokamilika mtajulishwa.


Ahsanteni kwa kunisikiliza

Imetolewa na:
David A. Misime  - SACP 
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi.



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.