Aliyekuwa
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege
Tanzania (TAA), Renatus Msangira akifungua mafunzo ya uandaaji na
uwakilishwaji wa vitabu vya Hesabu za fedha kwa kuzingatia viwango vya
Kimataifa vya Uhasibu kwa Taasisi za serikali (IPSAS accrual), yaliyoanza
leo kwenye ukumbi wa mikutano wa Jengo la Pili la Abiria la Kiwanja cha
Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA_TB2), kwa kushirikisha
Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani.
Wahasibu
na Wakaguzi wa Ndani wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), leo
wakiwa kwenye mafunzo ya uandaaji na uwakilishwaji wa vitabu vya Hesabu za
fedha kwa kuzingatia viwango vya Kimataifa vya Uhasibu kwa Taasisi za
serikali (IPSAS accrual), yanayofanyika kwa siku tano kwenye ukumbi wa
mikutano wa Jengo la Pili la Abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha
Julius Nyerere (JNIA_TB2).
Mkurugenzi
wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Paul
Rwegasha (kushoto) akizungumza na Kamishna Msaidizi wa Zimamoto na Uokoaji
(ACF) Bakari Mrisho (wa pili kushoto), aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa
Utawala na Rasilimali Watu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania,
Renatus Msangira (kulia), na Meneja wa Utawala na Rasilimali Watu na
Mafunzo, Abdi Mkwizu.
Na Bahati Mollel, TAA
MAFUNZO ya uandaaji
na uwakilishwaji wa vitabu vya Hesabu za fedha kwa kuzingatia viwango vya
Kimataifa vya Uhasibu kwa Taasisi za serikali (IPSAS accrual), yameelezwa kuwa
yataondoa hoja za Wakaguzi wa ndani na nje.
Kaimu Mkurugenzi wa
Fedha na Biashara wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), CPA Josephine
Kolola amesema hayo wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyoanza leo kwenye
Jengo la Pili la Abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere
(JNIA-TB2) kwa kushirikisha Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani wa Mamlaka hiyo,
ambapo yanashirikisha washiriki 56 kutoka Viwanja vya ndege vya serikali
vilivyopo Tanzania Bara.
“Pia ni matarajio
yangu baada ya mafunzo haya kutawezesha kupungua kwa kiasi kikubwa na hata
kutokuwepo kabisa kwa hoja za wakaguzi wa ndani na nje kutokana na uelewa
utakapopatikana kwa washiriki,” amesema CPA Kolola.
CPA Kolola amesema
mafunzo hayo pia yatashirikisha suala zima la maadili ya Uhasibu (Code of Conduct & Ethics for
Professional accountants); uzingatiaji wa miongozo mbalimbali ya kifedha
kadiri inavyotolewa na serikali (MoFP), hivyo kutoa taarifa za fedha zenye
kuonesha uhalisia na mwelekeo wa Mamlaka wenye tija kwa watumiaji wa taarifa
hizo.
“Mafunzo haya
yatawakumbusha wahasibu wote wa Mamlaka dhamana waliyonayo katika masuala yote
ya kifedha hivyo kuwa makini katika kazi zao za kila siku kwa kuhakikisha
umakini wa kuingiza data za mapato, matumizi, madeni nk, hivyo kuepusha makosa
kwenye vitabu vya hesabu,” amesema CPA Kolola.
Awali akifungua
mafunzo hayo aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa TAA, Renatus
Msangira akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu Mhandisi Mshauri Julius Ndyamukama, aliwataka
wahasibu na wakaguzi hao wa ndani kuhakikisha wanatunza siri za hesabu ya
taasisi hiyo, kwa kuwa ni kosa la kisheria kuzitoa kwa watu wasiohusika.
“Hesabu za taasisi au
ofisi yeyote ya Umma hazipaswi kusambazwa hovyo kwa watu wasiostahili hizo ni
moja ya siri na zinapaswa kutunzwa vyema, na hutolewa kwa kibali maalum endapo
itahitajika, lakini sio zaidi ya hapo” alisisitiza Msangira.
Pia amewataka
washiriki hao wapatao 56 kutoka viwanja mbalimbali vya ndege Tanzania Bara watumie
fursa hiyo kwa kuboresha utendaji wao wa kazi kwa kushirikiana vyema na Vitengo
na Idara zilizopo, ili kufanikisha lengo la Mamlaka la kuwa na hesabu bora.
Hatahivyo,
aliwasisitizia kufanya kazi kwa upendo, uadilifu na amani kwa kutojiwekea msongo
wa mawazo kwani wanaweza kuharibu kazi kutokana na akili kutokuwa sawa.
“Nina imani kubwa
kwamba mafunzo haya yatawaongezea kitu kikubwa sana katika kada zenu, hivyo
mjaribu kuzingatia kazi na kada zenu na msiingilie kazi zisizowahusu,” amesema.
Halikadhalika
aliwasisitizia kujiendeleza zaidi kitaaluma ili wapate CPA, ambayo itawaruhusu
kukafanya kazi kwa viwango vinavyohitajika kitaifa na kimataifa.
Mafunzo hayo ya siku
tano yanaendeshwa na Wataalam kutoka Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi
Tanzania (NBAA).
No comments:
Post a Comment