Mapema leo 30/03/2020 katika Uwanja
wa Mazoezi wa Kikosi cha kutuliza Ghasia Kamishna wa Operesheni na Mafunzo
ya Jeshi La Polisi CP Liberatus Sabas, ameongea na Askari wa Vikosi Maalum kutoka
mikoa mbalimbali waliowasili mkoani Mtwara kwaajili ya kuimalisha Ulinzi katika
mpaka ya Tanzania na Msumbiji baada ya kutokea machafuko nchini humo.
Kamishna wa Opereshni
na Mafunzo CP Liberatus Sabas, akikagua moja ya silaha aina ya Mota ambayo itatumika
katika Operesheni ya kuimalisha ulinzi katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji baada
ya Nchini humo kuvamiwa kwa kambi za Jeshi na vituo vya Polisi pamoja na Mabenki
nchini Msumbiji siku ya tarehe 23/03/2020.
Kamishna wa Opereshni na Mafunzo CP Liberatus Sabas,
akiwatia Moyo Askari waliopangwa kufanya Doria maeneo mbalimbali ya Mkoa wa
Mtwara baada ya kutokea kwa uvamizi wa vituo vya Polisi, Kambi za Jeshi na Mabenki
huko nchini Msumbiji.
(PICHA NA JESHI LA POLISI)
No comments:
Post a Comment