Habari za Punde

KAMISHNA CP SABAS AKUTANA NA KIKOSI MAALUM CHA KUPAMBANA NA UHALIFU KILICHOWASILI MKOANI MTWARA KATIKA KUIMALISHA ULINZI NA USALAMA KATIKA MPAKA WA TANZANIA NA MSUMBIJI.

Mapema leo 30/03/2020 katika Uwanja wa Mazoezi wa Kikosi cha kutuliza Ghasia  Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi La Polisi CP Liberatus Sabas, ameongea na Askari wa Vikosi Maalum kutoka mikoa mbalimbali waliowasili mkoani Mtwara kwaajili ya kuimalisha Ulinzi katika mpaka ya Tanzania na Msumbiji baada ya kutokea machafuko nchini humo
Kamishna wa Opereshni na Mafunzo CP Liberatus Sabas, akikagua moja ya silaha aina ya Mota ambayo itatumika katika Operesheni ya kuimalisha ulinzi katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji baada ya Nchini humo kuvamiwa kwa kambi za Jeshi na vituo vya Polisi pamoja na Mabenki nchini Msumbiji siku ya tarehe 23/03/2020. 

Kamishna wa Opereshni na Mafunzo CP Liberatus Sabas, akiwatia Moyo Askari waliopangwa kufanya Doria maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mtwara baada ya kutokea kwa uvamizi wa vituo vya Polisi, Kambi za Jeshi na Mabenki huko nchini Msumbiji.
(PICHA NA JESHI LA POLISI)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.