Habari za Punde

SERIKALI YAVUNJA MKATABA NA KAMPUNI YA ROM SOLUTIONS, WAZIRI SIMBACHAWENE ASEMA SERIKALI HAIDAIWI, HAIDAI

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akizungumza na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa mikutano wa Wizara, jijini Dodoma, leo. Simbachawene amesema Serikali imevunja Mkataba na Kampuni ya Rom Solutions ya Nchini Romania ambao ulihusu ununuzi wa vifaa vya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa gharama ya Euro 408,416,288.16, ambazo ni sawa na Shilingi Trilioni moja. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Christopher Kadio, na kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Ramadhani Kailima. 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (katikati), akimsikiliza Mwandishi wa Habari wa gazeti la Habari leo, Mroki Mroki alipokuwa anamuuliza swali katika Mkutano na Waandishi wa habari uliofanyika, ukumbi wa mikutano wa Wizara, jijini Dodoma, leo. Simbachawene amesema Serikali imevunja Mkataba na Kampuni ya Rom Solutions ya Nchini Romania ambao ulihusu ununuzi wa vifaa vya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa gharama ya Euro 408,416,288.16, ambazo ni sawa na Shilingi Trilioni moja.
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.