JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA
YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
SALAMU
ZA POLE
|
TAARIFA KWA
UMMA
Aprili
1, 2020 Dodoma.
Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.
Harrison
Mwakyembe (Mb)
ametoa pole kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habari Tanzania (TBC) Dkt. Ayub
Rioba kwa kuondokewa na Mwanahabari Nguli Bw. Marin Hassan Marin leo asubuhi Jijini
Dar es Salaam.
Akiongea moja kwa
moja na televisheni ya TBC 1, Dkt. Mwakyembe ameeleza kuwa TBC na tasnia ya habari kwa ujumla imepata pigo kwani Bw. Marin alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha sekta ya Habari inakuwa na mchango chanya katika maendeleo ya jamii.
Enzi za uhai wake marehemu alikuwa mmoja wa
waasisi wa vipindi kadhaa vya TBC vikiwemo Jambo Tanzania, Nyumba ya Jirani na
Aridhio.
Dkt.
Mwakyembe ametoa pole kwa familia, ndugu,jamaa,marafiki na wadau wote wa tasnia ya habari nchini.
Imetolewa na
Lorietha
Laurence
Kaimu Mkuu wa
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
No comments:
Post a Comment