JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA
ZIMAMOTO NA UOKOAJI
|
OFISI YA KAMISHNA JENERALI
JESHI LA
ZIMAMOTO NA UOKOAJI
S. L. P. 1509,
DODOMA.
02 APRILI, 2020
|
Simu Nambari: +255-22-2113537
Telefax: +255-22-2184569
BaruaPepe: fire.rescue@frf.go.tz
Dharura
simu Nambari 114
TAARIFA
KWA UMMA
Mkuu
wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, (CGF) John W. Masunga, amefanya mabadiliko ya
baadhi ya Makamanda wa Mikoa.
Makamanda
walioguswa na mabadiliko hayo ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Zimamoto na
Uokoaji (SACF) ABDALLAH MAUNDU anakwenda kuwa (RFO) Kamanda wa Zimamoto na
Uokoaji Mkoa wa Kigoma, kabla ya nafasi hii alikuwa Makao Makuu Dodoma.
Aliyekuwa
Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara, Kamishna Msaidizi Mwandamizi
(SACF) SALUM M. OMARI, anayekwenda kuwa (RFO) Kamanda wa Mkoa wa Kinondoni,
kuchukua nafasi ya Mrakibu Msaidizi wa Zimamoto na Uokoaji (ASF) JENIFER V.
SHIRIMA anayehamia Makao Makuu kuwa Mkuu wa dawati la Mambo ya Nje.
Aidha
nafasi ya (RFO) Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara inachukuliwa na
Mrakibu Msaidizi wa Zimamoto na Uokoaji (ASF) AUGUSTINE B. MAGERE.
Pia
aliyekuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Temeke, Kamishna Msaidizi
Mwandamizi (SACF) ELIA P. KAKWEMBE, anayekwenda kuwa (CFO) Kamanda wa Viwanja
vya Ndege Nchini, kuchukua nafasi ya Kamishna Msaidizi (ACF) BAKARI K. MRISHO
anayekwenda kuwa (RFO) Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Temeke.
Aliyekuwa
Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa
Shinyanga Mrakibu wa Zimamoto na Uokoaji (SF) OMARI H. SIMBA anayekwenda kuwa
(RFO) Kamanda wa Mkoa wa Simiyu na nafasi yake inachukuliwa na Mrakibu wa Zimamoto na Uokoaji (SF) GEORGE G. MRUTU
anayetoka Makao Makuu.
Mabadiliko
haya ni ya kawaida kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
KUOKOA MAISHA NA
MALI NI JUKUMU LETU SOTE
Imetolewa na;
Joseph
Mwasabeja – (INSP)
Msemaji wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Makao Makuu
S. L. P 1509
No comments:
Post a Comment