Na.Himid Choko.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
imesema, kumekuwa na mafanikio makubwa
kutokana na kuweka mfumo mzuri wa udhibiti wa matumizi ya maliasili zisizoresheka ikiwemo
mchanga.
Akiwasilisha Ripoti ya utekelezaji wa
Maagizo ya Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo ya Baraza la Wawakilishi ya
Mwaka 2019/2020 kwa wizara yake, Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa
Mmanga Mjengo Mjawiri amesema miongoni mwa mafanikio hayo ni kupungua uchimbaji
holela wa mchanga, kifusi, mawe na kokoto.
Amesema hatua hiyo pia imepelekea
ongezeko la matumizi bora ya mali asili na hivyo kupunguza athari za kimazingira katika
maeneo ya uvunaji wa rasilimali hizo.
Mheshimiwa Mjawiri ameongoza kusema
kuwa, udhibiti wa mali asili hizo
kumepelekea kupungua kwa bei na upatikaji mzuri wa mchanga kwa mahitaji ya wananchi na
Miradi ya Maendeleo.
Aidha, Waziri Mjawiri amesema wizara yake imeweza kuongeza mapato
yanayotokana na mali asili zisizorejesheka.
“Mafanikio
mengine yaliyopatikana ni kuongezeka kwa
mapato yanayotokana na rasilimali zisizorejesheka kutoka shilingi 558,000,000 mwaka 2015 mpaka
shilingi 16,549,056 hadi kufikia mwezi Februari 2020.” Alisisitiza Mheshimiwa Mjawiri.
Wakati huo huo, Mheshimiwa Mjawiri
amesema Wizara yake inaendelea na utaratibu wa upandaji wa miti katika maeneo
ya uchimbanji wa mali asili hizo ambapo jumla ya Hekta 10.7 katika maeneo ya Pangatupu, na Donge Chechele kwa mwaka
2019/2020.
Nae, Mwenyekiti wa Kamati ya
Fedha, Biashara na kilimo ya Baraza la
Wawakilishi Mheshimiwa Dkt. Mwinyihaji
Makame akitoa maoni ya Kamati yeke kuhusiana na Ripoti hiyo ameishauri Serikali
kuyaruhusu Makampuni makubwa pamoja na
taasisi zenye matumizi makubwa ya mchanga kuagizishia mali asili hiyo kutoka nnje ya
zanzibar kwa utaratibu maalum ili mchanga uliopo uendelee kutumiwa na wananchi wa kawaida.
Baraza la Wawakilishi, Zanzibar.
Jumatatu, Aprili 14, 2020
No comments:
Post a Comment