Habari za Punde

Umoja wa Wazalendo na Wafanyabiashara watoa misaada kukabiliana na Mapambano Dhidi ya Virusi Vya Corona COVID -19.









PRESS RELEASE

MAKABIDHIANO YA MISAADA KUTOKA UMOJA WA
WAZALENDO NA WAFANYABIASHARA KATIKA
MAPAMBANO DHIDI YA VIRUSI VYA KORONA
3 APRIL 2020

On Behalf of the entire Business Community, Patriotism and Friends of Zanzibar both in Mainland Tanzania and Zanzibar
Telephone: 0779 060 338



PRESS RELEASE

Mheshimiwa Waziri
Kwanza nitoe shukrani kwa niaba ya Umoja wa Wazalendo na wafanyabiashara kwako Mhe. Waziri, kwa kuchukua muda wako kujumuika nasi katika shughuli yetu ya leo ya makabidhiano ya bidhaa , madawa na vifaa vilivyoochangwa au kutolewa na wafanyabishara, Wazalendo na Marafiki wa Zanzibar
Natambua majukumu makubwa ulionayo ya kitaifa, lakini umeweza kulipa uzito suala hili. Tunakushukuru  sana!
Vile vile ninawashukuru wafanyabiashara, Wazalendo, Marafiki wa Zanzibar, Taasisi na watumishi wa umma waliojitokeza na kutuunga mkono katika juhudi zetu za kupambana na mlipuko huu wa virusi vya korona (Covid19 outbreak).
Mheshimiwa Waziri
Ni miezi mitatu imepita tangu ugonjwa hatari wa korona umeingia duniani. Kasi ya kusambaa kwa ugonjwa huu inazidi kuongezeka na hatimaye ugonjwa huu umefika nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania. Katika kuunga mkono juhudi za Mhe Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dr Ali Mohammed Shein na Serikali yake, Umoja huu wa Wafanyabiashara na Wazalendo Tanzania Bara na Visiwani haukubaki nyuma katika mapambano dhidi ya ugonjwa huu, tangu uliporipotiwa duniani na hata ulipotangazwa kuingia hapa nchini. Tunatambua kuwa, tayari serikali imeweka mikakati mahususi ya kupambana na ugonjwa huu na kuhakikisha wafanyabiashara na wananchi wamejiandaa na athari zinazoweza kusababishwa na ugonjwa huu wa Covid19 kiuchumi, kiafya na kijamii kwa ujumla.
Mheshimiwa Waziri
Kwa kutambua na kuunga mkono juhudi za Mhe Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dr Ali Mohammed Shein na Serikali yake kwenye afya, naomba niwasilishe Architectural Drawings (Ramani ya mchoro) wa Laboratory Level 3 ambayo kungepenga kuwasilisha kwa serikali na kama ikiwapendeza serikali, tuje tukae chini kuangalia namna ya kuisadia Serikali kiujenzi na kwa vifaa
Mheshimiwa Waziri
Umoja huu; umeleta mshikamano wa pamoja wa wafanyabiashara na taasisi mbalimbali za kibishara na umekuwa ukitoa ushirikiano wa karibu kwa Serikali (Public Private Partnership – PPP) katika kuhakikisha kuwa mapambano dhidi ya ugonjwa huu yanaleta ushindi.
Mheshimiwa Waziri
Ushirikiano na moyo wa uzalendo uliopo kati ya umoja huu wa Wazalendo na Wafanyabiashara nchini umewezesha kuunganisha nguvu na hatimaye kufanikisha kupatikana kwa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi 126 milioni  vitakavyosaidia kwenye mapambano dhidi ya ugonjwa wa corona.
Naomba nitoe orodha ya wale wote waliochangia
Explain the HOTSPOTS areas identified: Malindi Port;Stone Town; Marikiti; Kivingo Beach; Mnazi Mmoja Hospital; Kiinua Miguu Prison; Soko La Mwanakwerekwe; Bububu; Forodhani Park; Kituo cha Mabasi Airport; Darajani; Soko la Saateni; Mlandege; Michenzani; Kariakoo; Rahaleo; Mwembeladu Hospital; Jangombe; Mombasa; Mwera; Ngungwi Beach; Kiwengwa; etc.

Mheshimiwa Waziri
Umoja wa Wazalendo na ya wafanyabiashara nchini, wakubwa kwa wadogo wote tumeguswa na tumewiwa kutoa ushirikiano kwa Serikali, jamii na kwenye maeneo yetu ya kazi kuhakikisha kuwa tunapambana kikamilifu na ugonjwa hatari wa corona.  Napenda tukuhakikishie Mhe Waziri kuwa Umoja huu wa Wazalendo na Wafanyabiashara nchini utaendelea kushirikiana na serikali na wadau wengine hadi pale ambapo ugonjwa huu utakapodhibitiwa kikamilifu.
Mheshimiwa Waziri
Ushiriki wa Umoja huu katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa corona haukwepeki!!. Pamoja na nia njema ya umoja huu, ikumbukwe pia kuwa umoja huu ambao ndio nguzo ya sekta binafsi una mchango mkubwa katika kujenga uchumi wa nchi na ndiyo sekta inayozalisha ajira nyingi nchini kwa takribani asilimia 80. Mheshimiwa Waziri, Sekta Binafsi tunashiriki kwa asilimia mia moja katika mapambano dhidi ya corona kwa kuwa sisi ni sehemu ya jamii. Tusipofanya hivyo, hakuna atakayebaki salama; na hata biashara zetu zitakufa pia. Mheshimiwa Waziri, kila jambo linahitaji watu. Nchi inahitaji watu. Maendeleo yanahitaji watu. Biashara pia zinahitaji watu, hivyo tuna kila sababu ya kushiriki kujilinda na kuwalinda wengine,”

Mheshimiwa Waziri
Vile vile Umoja huu unaipongeza Serikali kwa hatua na juhudi makini ilizochukua hadi sasa. Hatua hizo ni pamoja na kuwahamasisha watanzania kuchukua tahadhari na kuwa makini wakati wote kwani Kila mtu akitekeleza wajibu wake wa kujilinda yeye binafsi na kuwalinda wengine tutaweza kuvuka kwa mafanikio makubwa, hasa ikizingatiwa kuwa walio wengi wanapona hata baada ya kupata maambukizi ya ugonjwa huu

Mheshimiwa Waziri
Kabla ya kumaliza hotuba yangu naomba nitoe shukrani kubwa sana kwako, kwa walio hapa na wasiojaaliwa kuwepo ambao wameshiriki kwa hali na mali nikianzia na:



Mzee wangu Subhash Patel; Motisun and CTI Chairman
Mr Mohammed Bhaloo, Chairman Agha Khan Trust for Culture Zanzibar
Said Salim Bakhresa (Bakhresa Group)
Dhruv Jog, Advent Construction
Dr. Mohammed Ali, SADC Medical Expert
Abubakar Said Salim Bakhresa
Ambassador Antonio, Brazil (Personal Contribution)
Dr Maryam Lymo, Innovative Projects
Balozi Kindamba
Hamad Hamad, Zanzibar Chamber of Commerce
Mr. Rahim Bhaloo, Multi Color Printers Ltd
Parvin Hasnein
Asha Aslan
Lukman Fideli Ali
Farid Fazach
Aboud Nassor Khamis
Nafisa Jidawi, Wajamama
Zanzibar Sugar Factory Ltd
Skylink Travel & Tours
AZAM Marine Co Ltd
Amsons Group
Camel Oil
Association of Tanzania Oil & Gas (ATOGS)
ORYX Energies
Tridea Cosmetics Ltd
Majid Store
Aruna Pharmacy
Patel Import & Export 
Bharat Enterprises
Kay Sotta
Plastic Limited
Print Plus
Mozeti
Virgo Group
Print Plus
Ashton Media
Pamoja na wote waliotoa michango yao ya hali na mali .
Umoja ni nguvu, Utengano ni Udhaifu
Mshikamano Daima!


Asanteni sana

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.