Habari za Punde

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Simbachawene : Kifungo cha Nje Suluhisho Msongamano Magerezani Nchini.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Jamii kabla ya kuzindua Kamati hiyo, jijini Dodoma, leo, ambayo itasimamia Utekelezaji wa Sheria ya Huduma kwa Jamii inayotoa fursa kwa wafungwa wa vifungo vidogo kutumikia adhabu hizo kwenye jamii. Pia Waziri huyo ameitaka Kamati hiyo, iweke mikakati zaidi ya kusimamia adhabu mbadala ya kifungo cha nje ili kuondoa msongamano magerezani.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (katikati meza kuu), akimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Christopher Kadio, alipokuwa akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Jamii kabla uzinduzi wa Kamati hiyo, jijini Dodoma, leo.  
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kulia), akimsikiliza Katibu wa Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Jamii, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Huduma za Uangalizi, Aloyce Musika, alipokuwa anazungumza kabla ya kabla uzinduzi wa Kamati hiyo, jijini Dodoma, leo. Waziri Simbachawene amezindua Kamati hiyo, ambayo itasimamia Utekelezaji wa Sheria ya Huduma kwa Jamii na kutoa fursa kwa wafungwa wa vifungo vidogo kutumikia adhabu hizo kwenye jamii.  Wapili kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Jaji Zephrine Galeba.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (katikati meza kuu), akimsikiliza Mjumbe wa Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Jamii, Isaac Nantanga (kushoto), wakati alipokuwa anajitambulisha kabla ya uzinduzi wa Kamati hiyo, jijini Dodoma, leo. Watatu kulia ni Katibu Mkuu, Christopher Kadio.  

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (wanne kushoto), Katibu Mkuu, Christopher Kadio (wanne kulia), Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Jamii, Jaji Zephrine Galeba (watatu kushoto), Katibu wa Kamati, Aloyce Musika (watatu kulia), Kamishna Jenerali wa Magereza, Suleiman Mzee (wapili kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati hiyo, jijini Dodoma, leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.