HOTUBA YA WAZIRI
WA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA
KWA MWAKA 2020/2021
UTANGULIZI
1.
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba
Baraza lako Tukufu liingie katika Kamati ili niweze kutoa maelezo ya makadirio
ya mapato na matumizi ya Fedha ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa mwaka
wa fedha 2020/2021.
2.
Mheshimiwa Spika, Kwanza kabisa,
namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehma kwa kutujaalia uhai, uzima na afya njema.
Vile vile akatuwezesha tukakutana katika kikao hiki cha bajeti katika kipindi
cha uongozi wa Awamu ya Saba ya Kiongozi wetu mahiri Mheshimiwa Dk. Ali Mohamed
Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Namuomba Mwenyezi
Mungu atuzidishie kheri naneema zake na anipe uwezo na uwasilishaji fasaha wa
hotuba hii ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara yangu. Pia namuomba
Mwenyezi Mungu atujaalie wasaa wajumbe wote wa kuichangia vizuri na hatimae
Baraza lako tukufu liweze kuipitisha kwa kauli moja.
3.
Mheshimiwa Spika, pili, nachukua nafasi
hii kumpongeza kwa dhati Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein kwa uongozi wake imara, wenye busara na moyo thabiti
katika kusimamia uimarishaji wa huduma za jamii kwa wananchi wake ikiwemo
huduma ya elimu. Pongezi za pekee kwa kutimiza miaka kumi ya uongozi wake ulioleta
maendeleo makubwa katika nchi yetu. Maendeleo yaliyotokana na uongozi wake
imara ambao umehakikisha kuwa changamoto zote zinazowakabili watoto na vijana
wote katika kupata elimu zinapatiwa ufumbuzi kikamilifu ikiwemo kufuta michango
ya wazazi na Serikali kutoa fedha za ruzuku kwa skuli kufidia fedha zilizokuwa
zikitolewa na wazazi kwa skuli. Mwenyezi Mungu amzidishie umri mrefu wenye
kheri, afya njema na maarifa zaidi ili aendelee kuiongoza na kuiendeleza nchi
yetu. Vile vile, napenda kutoa pongezi zetu na shukurani za dhati kwa Makamo wa
Pili wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, kwa utendaji wake
mzuri, uliokuwa karibu na Wizara yetu na wadau mbalimbali wa elimu wa ndani na
nje ya nchi pamoja na michango yake binafsi katika kuiendeleza sekta ya elimu.
4.
Mheshimiwa Spika, Vilevile,nachukua
fursa hii kukupongeza wewe, Naibu Spika pamoja na Mwenyekiti wa Baraza kwa
mashirikiano yenu na miongozo mizuri mnayotupatia inayopelekea kupata ufanisi
katika utendaji wa majukumu yetu unaochangia katika kuleta maendeleo ya Taifa
letu. Namuomba Mwenyezi Mungu akuzidishieni busara, hekima, umahiri na uadilifu
katika kuliongoza Baraza hili tukufu.
5.
Mheshimiwa Spika, Naomba pia shukurani
za dhati nizifikishe kwa wajumbe wote wa Baraza hili Tukufu na hasa Wajumbe wa
Kamati ya Ustawi wa Jamii chini ya uongozi mahiri wa Mwenyekiti wake Mheshimiwa
Mwanaasha Khamis Juma kwa ushauri na maelekezo ya kimaendeleo wanayotupatia
katika utekelezaji wa shughuli zetu mbalimbali wanapopata muda wa kuwa nasi
katika taasisi za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali.
6.
Mheshimiwa Spika, Kwa dhati kabisa, napenda
kumpongeza na kumshukuru Mheshimiwa Simai Mohammed Said, Naibu Waziri wa Elimu
na Mafunzo ya Amali kwa kunipa mashirikiano ya karibu yaliyowezesha kwa kiasi
kikubwa katika utekelezaji wa mpango wa elimu. Aidha, nawapongeza watendaji
wote wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali wakiwemo Katibu Mkuu, Manaibu
Katibu Wakuu, Wakurugenzi, Wajumbe wa Bodi mbali mbali za Elimu, Maafisa wa
ngazi mbalimbali wa Wizara, Viongozi na watendaji mbalimbali wa Ofisi ya Rais,
Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalumu za Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar bila kuzisahau Kamati zetu za skuli kwa mashirikiano yao makubwa
katika kuleta maendeleo ya elimu. Aidha, shukurani ziwafikie walimu, wazazi,
wanafunzi na washirika wote wa elimu wa ndani na nje ya nchi kushiriki
kikamilifu katika kusaidia harakati za utoaji na upatikanaji wa huduma ya elimu
iliyo bora kwa watoto, vijana na wazee wetu waliokosa fursa hiyo. Mola
awazidishie moyo wa imani na upendo ili michango yao iendelee kuwapatia elimu
wahitaji wote kwa kiwango chenye ubora.
7.
Mheshimiwa Spika, Mwisho nawashukuru
sana watendaji wa Wizara ya Fedha na Mipango kwa ushirikiano wao ambao
umechangia katika kuimarisha huduma za elimu katika mwaka 2019/20. Nimatumaini
yetu kuwa ushirikiano huo utaimarika zaidi katika kuimarisha upatikanaji wa
huduma za elimu katika Taifa letu kwa kupitia kauli mbiu ya Wizara yetu ya “Elimu Bora Kwanza”.
8.
Mheshimiwa Spika, kabla ya kuelezea
utekelezaji wa mipango ya elimu ya Mwaka 2019/2020 na matarajio ya mwaka 2020/2021,
napenda kuelezea walau kwa ufupi maendeleo tuliyoyapata katika kipindi cha
miaka 10 (2011-2020) chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dk. Ali Mohamed Shein, Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
HALI YA MAENDELEO YA
ELIMU KWA KIPINDI CHA MIAKA 10, 2011-2020.
9.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha
kuanzia mwaka 2011 hadi 2020, miundombinu ya elimu imeimarika kwa kiwango
kikubwa katika ngazi zote za elimu. Idadi ya skuli za maandalizi imeongezeka
kutoka 242 (29 za Serikali na 213 za binafsi) mwaka 2011 hadi kufikia skuli 368
(35 za serikali na 328 za binafsi) mwaka 2020. Aidha, uandikishaji wa wanafunzi
katika ngazi yaelimu ya maandalizi umeongezeka kutoka wanafunzi 33,229 mwaka
2011 ikiwa sawa na asilimia 37.1 na kufikia wanafunzi 92,098 mwaka 2020 sawa na
asilimia 86.0.
10.
Mheshimiwa Spika, katika kuongeza
ushiriki wa watoto katika ngazi ya elimu ya maandalizi, Wizara ilianzisha
utoaji wa elimu ya maandalizi kupitia vituo vya Tucheze Tujifunze (TuTu) hasa katika
maeneo ambayo hayakuwa naskuli. Idadi ya Vituo vya TuTu imeongezeka kutoka 179vyenye
jumla ya wanafunzi 7,022 mwaka 2011na kufikia vituo 366 vyenye jumla ya
wanafunzi 17,769 mwaka 2020.
11.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa elimu ya
msingi, idadi ya skuli zimeongezeka kutoka skuli 200 mwaka 2011 zikiwa na
wanafunzi 237,690 sawa na asilimia 118.5 ya uandikishaji mwaka 2011 na kufikia
skuli 431 mwaka 2020 zenye wanafunzi 313,097 sawa na asilimia 120.7mwaka
2020.
12.
Mheshimiwa Spika, idadi ya skuli za
sekondari imeongezeka kutoka skuli 201 mwaka 2011 na kufikia 213 mwaka 2020.
Hii imepelekea ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi wa Kidato cha Kwanza hadi
cha Nne kutoka wanafunzi 77,671 sawa na asilimia 67.2 mwaka 2011 na kufikia
wanafunzi 124,493 sawa na asilimia 79.5 mwaka 2020. Skuli za msingi na
sekondari za kisasa zenye majengo ya ghorofa zimeanzishwa chini ya uongozi wa
Dk. Ali Mohamed Shein.
13.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa elimu ya
Sekondari ya juu (kidato cha 5 hadi kidato cha 6) uandikishaji wa wanafunzi umeongezeka
kutoka wanafunzi 4,073 mwaka 2011 na kufikia wanafunzi 5,679 mwaka 2020.
14.
Mheshimiwa Spika, Ubora wa elimu umekuwa
ukiongezeka mwaka hadi mwaka kama inavyodhihirika katika matokeo ya mitihani ya
Taifa. Katika mitihani ya kidato cha pili, idadi ya wanafunzi waliofaulu na
kuteuliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tatu imeongezeka kutoka watahiniwa 11,562
ikiwa ni sawa na asilimia 58.2 ya watahiniwa wote wa mwaka 2010/2011 na kufikia
watahiniwa24,946 sawa na asilimia 76.8 ya watahiniwa wote mwaka 2019/2020.
15.
Mheshimiwa Spika, katika mtihani wa
kidato cha nne, idadi ya watahiniwa waliofaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza
na pili imeongezeka kwa zaidi ya mara Sita (6) kutoka watahiniwa 260 mwaka
2010/11 na kufikia wanafunzi 1,808 mwaka 2019/2020. Aidha, matokeo ya mtihani
ya Kidato cha sita nayo yameimarika ambapo idadi ya watahiniwa imeongezeka
kutoka 1,959 mwaka 2010/2011 hadi kufikia watahiniwa 2,065mwaka 2019/2020.
Idadi ya wanafunzi waliofaulu imeongezeka kutoka wanafunzi 1,517mwaka 2010/2011
ikiwa ni sawa na asilimia 77.4 ya watahiniwa hadi kufikia wanafunzi 2,000 sawa
na asilimia 96.9 mwaka 2019/2020. Aidha, idadi ya wanafunzi waliopata daraja la
kwanza (Division 1) imeongezeka kutoka wanafunzi 24 mwaka 2010/2011 na kufikia
wanafunzi 188 mwaka 2019/2020.
16.
Mheshimiwa Spika, chini ya Uongozi wa
Dk. Ali Mohamed Shein akiwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar Chuo
kimepiga hatua kubwa kwa kuimarika kwa miundombinu na kuongezeka kwa idadi ya
skuli, Taasisi, programu mbali mbali za masomo, miongoni mwa skuli mpya ni
skuli ya kilimo, skuli ya utibabu wa Meno na Taasisi ya Masomo ya Ubaharia.
Aidha programu mbalimbali zimezinduliwa zikiwemo za Shahada ya kwanza ya
Uuguzi, Shahada ya kwanza ya Sayansi na Kilimo, Shahada ya Utabibu wa Meno na
Shahada ya Uzamili ya Lugha na Elimu. Vilevile katika kipindi cha miaka 10
iliyopita Chuo cha SUZA kimetanuliwa kwa kuunganishwa na vyuo vitano vikiwemo
Chuo cha Afya, Chuo cha Utalii, Chuo cha Kilimo, Chuo cha Usimamizi wa Fedha na
kufungua kampas ya Chuo cha ualimu cha Benjamin Wiliam Mkapa Pemba.
17.
Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha
miaka tisa bajeti ya sekta ya elimu imeongezeka kwa asilimia 91.4 kutoka TSh. 93,468,089,000/=
mwaka 2010/2011 hadi kufikia TSh. 178,917,149,000/=
mwaka 2019/2020. Kuongezeka kwa matumizi ya Serikali kwa sekta ya elimu
kunadhihirisha namna Serikali ilivyotoa kipaumbele katika kufanikisha
utekelezaji wa kauli mbiu ya “Elimu Bora
Kwanza”.
18.
Mheshimiwa Spika, baada ya muhutasari
huo, naombasasa nitoe maelezo ya utekelezaji wa kazi kwa mwaka wa fedha 2019/2020.
MIRADI YA SEKTA YA ELIMU
19.
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha
2019/2020, Wizara ilitekeleza kazi zake kupitia miradi mikuu mitano, ifuatayo:
-
1.
Uimarishaji wa Elimu ya
Maandalizi
2.
Uimarishaji wa Elimu ya Msingi
3.
Uimarishaji wa Elimu ya Lazima
4.
Uimarishaji wa Elimu Mbadala na
Amali
5. Miundombinu
katika elimu
UTEKELEZAJI WA KAZI ZA
WIZARA KWA MWAKA 2019/20
20.
MheshimiwaSpika, sasa naomba kuwasilisha
utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya elimu kwa mwaka wa fedha wa 2019/20 kwa
kupitia programu sita za Wizara yangu.
MUUNDO WA PROGRAMU
21.
Mheshimiwa Spika, programu
kuu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ni hizi zifuatazo: -
Programu ya 1: Elimu ya Maandalizi na
Msingi
Programu ya 2: Elimu ya Sekondari.
Programu ya 3: Elimu ya Juu
Programu ya 4: Elimu Mbadala na Mafunzo
ya Amali
Programu ya 5: Ubora wa Elimu
Programu ya 6: Uongozi na Utawala
MAELEZO YA UTEKELEZAJI KWA
PROGRAMU
22.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2019/20
Wizara ilitekeleza kazi zakekupitia Programu nilizoziainisha kwa kuzingatia
maendeleo ya elimu ya Kitaifa na Kimataifa ikiwemo Dira ya Taifa ya Maendeleo
ya Zanzibar ya mwaka 2020, lengo la MKUZA III, vipaumbele vya sekta pamoja na
lengo la nne la Maendeleo Endelevu Duniani.
23.
Mheshimiwa Spika, Programu hizo
zilitekelezwa kwa mashirikiano kati ya Serikali, Jamii na Washirika wa
Maendeleo wa ndani na nje ya Zanzibar. Programu zilitengewa jumla ya TSh.
178,917,149,000/-. Kati ya fedha hizo, TSh. 39,725,500,000/- kwa ajili ya matumizi
ya kazi za kawaida, TSh. 65,817,601,000/- matumizi ya mshahara na TSh.
73,374,048,000/- kwa kazi za maendeleo. Kati ya fedha za maendeleo, TSh.
5,800,000,000/- ni mchango wa SMZ na TSh. 67,574,048,000/- ni mchango wa
wahisani wakiwemo Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya Afrika (Badea), Mfuko wa
OPEC, Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Benki ya Dunia.
24.
Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Aprili,
2020, jumla ya TSh. 115,519,162,374/= sawa na asilimia 65 ya makadirio
zilipatikana. Kati ya fedha hizo, TSh. 58,077,204,998/= sawa na asilimia 88
zilitumika kulipia mishahara ya wafanyakazi na TSh. 25,319,542,615/= sawa na
asilimia 64 zimetumika kwa ajili ya kazi za kawaida. Kwa upande wa fedha za
maendeleo, jumla ya TSh. 32,122,414,761/=zilipatikana. Kati ya fedha hizo TSh. 1,453,046,000/=
sawa na asilimia 25 ni mchango wa Serikali na TSh. 30,669,368,761/= sawa na asilimia 45 ni kutoka kwa
wahisani. Jadweli Nam. 10(b) inatoa ufafanuzi zaidi.
25.
Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi wa
Programu za Wizara yangu ni kama ifuatavyo: -
PROGRAMU YA KWANZA:
ELIMU YA MAANDALIZI NA
MSINGI
26.
Mheshimiwa Spika, Programu hii inahusika
na uimarishaji na utoaji wa elimu ya maandalizi na msingi kwa wanafunzi wenye
umri kati ya miaka minne na kumi na mbili. Programu hii inatekelezwa kwa sehemu
kubwa katika kazi za kawaida kupitia Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali
za Mitaa na Idara Maalumu za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mashirikiano
ya karibu sana na Wizara yangu.
27.
Mheshimiwa Spika, Programu hii
ilitengewa jumla ya TSh. 9,010,580,000/-. Kati ya fedha hizo TZS. 157,169,000/-
kwa ajili ya kazi za kawaida, Tsh. 383,709,000/- kwa ajili ya malipo ya
mishahara ya wafanyakazi na TZS. 8,469,702,000/- kwa kazi za maendeleo kutoka
kwa Washirika wa Maendeleo. Hadi kufikia Aprili, 2020, jumla ya TSh. 2,980,270,068/=
sawa na asilimia 33 zilipatikana.
28.
Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi wa
programu hii ni kama hivi ifuatavyo: -
i).
Wanafunzi katika skuli 27 za msingi Unguja
na Pemba wanafaidika na huduma ya chakula.
ii).
Kuongezeka kwa uandikishaji wa wanafunzi
katika ngazi za maandalizi na msingi. Jumla ya wanafunzi 92,098 sawa na
asilimia 86.0 wameandikishwa katika madarasa ya maandalizi kwa mwaka 2020 ikiwa
ni ongezeko la asilimia 6.6 ikilinganishwa na wanafunzi 85,974 sawa na asilimia
81.4 walioandikishwa mwaka 2019.
iii).
Jumla ya seti 11,560 za madawati ya
wanafunzi watatu watatu wa skuli za msingi zimenunuliwa kutoka China. Jumla ya seti 7065 zimeshapokelewa na
kusambazwa katika skuli za msingi Unguja na Pemba. Seti 4,495 za madawati
zinatarajiwa kupokelewa katika mwezi Julai 2020
iv).
Skuli za maandalizi za Serikali
vimepatiwa vifaa kufundishia na kujifunzia, vikiwemo mikasi 1,260, rangi za
maji pc 630, brashi pc 1,080, gundi pc 617, vifutio pc 492, peni za ubao pc
630, manila bunda 87, gundi za karatasi pc 214, rangi za nta 360, vibao vya
kusomea pc 1700 na penseli pakiti 35.
v).
Jumla ya vituo 20 vipya vya Tucheze
Tujifunze (TuTu) vimefunguliwa katika Wilaya ya Kaskazini “A” (5), Wilaya ya
Magharibi “A” (5) kwa Unguja na Wilaya ya Wete (5), Wilaya ya Chakechake (5)
kwa Pemba. Idadi ya vituo vya TuTu imefikia 364 mwaka 2020 ikilinganishwa na
vituo 342 mwaka 2019. Kati ya vituo hivyo 172 vipo Unguja na vituo 192 vipo
Pemba. Aidha, walimu 728 wa vituo vya TuTu wamelipwa posho lao la kila mwezi
pamoja na kuwapatia chakula wanafunzi wote wa ngazi ya elimu ya maandalizi wa
skuli za maandalizi za Serikali Unguja na Pemba.
vi).
Vifaa vya kufundishia na kujifunzia
vimenunuliwa na kusambazwa katika vituo 20 vya TuTu Unguja na Pemba. Aidha,
vituo hivyo vimesaidiwa vifaa vya ujenzi yakiwemo mabati, saruji na matofali.
vii).
Jumla ya skuli 27 za jamii zikiwemo 11
Unguja na 16 Pemba zimeanzishwa pamoja na kupatiwa vifaa vya kufundishia na
kujifunzia.Aidha, jumla ya walimu 54 wa skuli za jamii na wasaidizi 26 wa vituo
vya TuTu wamepatiwa mafunzo ya maandalizi kupitia Programu ya “Madrasa Early
childhood”.
viii).
Jumla ya walimu 412 wa skuli za maandalizi
pamoja na wavituo vya TuTu Unguja na Pemba wamepatiwa mafunzo ya miezi sita ya
kuwajengea uwezo wa kufundisha elimu ya maandalizi kwa ufanisi zaidi.
ix).
Jumla ya walimu 350 wakiwemo 200 wa
Unguja na 150 kutoka Pemba wa Madrasa na Vyuo vya Kur’ani wamepatiwa mafunzo ya
umuhimu wa kutumia vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Aidha, vifaa vya
kukalia na kusomea viligawiwa katika Madrasa na Vyuo vya Kur’ani 100 Unguja na
60 Pemba.
Matokeo ya Muda Mfupi;
i.
Jumla ya watoto 92,098 ambao sawa na
asilimia 86.0 wameandikishwa katika ngazi ya elimu ya maandalizi, wakiwemo
wanaume 45,524 na wanawake 46,574. Hii ni sawa na ongezeko la asilimia 4.6
ikilinganishwa na asilimia 81.4 ya uandikishaji ya mwaka 2019. Jadweli namba 13(a), (b) na (c) yanatoa
ufafanuzi zaidi.
iii.
Jumla ya wanafunzi 313,097
wameandikishwa katika ngazi ya elimu ya msingi kwa mwaka 2020 ambao ni sawa na
asilimia 120.7. Kati yao, wanaume ni 158,383 sawa na asilimia 121.5 na wanawake
ni 154,714 sawa na asilimia 119.8. Jadweli namba
14 linatoa ufafanuzi zaidi.
PROGRAMU YA PILI: ELIMU YA
SEKONDARI.
29.
Mheshimiwa Spika, Programu hii inalenga
kutoa na kuimarisha elimu ya sekondari. Kwa mwaka 2019/20 programu hii
imetekelezwa kwa pamoja kati ya SMZ na Washirika wa Maendeleo wa ndani na nje
ya nchi. Jumla ya TSh. 104,591,382,000/- zilipangwa kutumika. Kati ya fedha
hizo, TSh. 6,824,440,000/- ni kwa kazi za kawaida, TSh. 42,362,596,000/-
zilitengwa kwa ajili ya kulipa mishahara na TSh. 55,404,346,000/- kwa miradi ya
maendeleo zikiwemo Tsh. 3,300,000,000/- za SMZ na TSh. 52,104,346,000/- za
wahisani. Hadi kufikia Aprili, 2020, jumla ya TSh.63,477,435,535/- zilipatikana
sawa na asilimia 61. Kati ya fedha hizo, TSh. 21,660,245,933/- sawa na asilimia
39 ni kwa ajili ya kazi za maendeleo. Aidha, TSh.20,828,245,933/- zimetolewa na
Washirika wa Maendeleowakiwemo BADEA, Mfuko wa OPEC, Benki ya Dunia na Shirika
lisilo la kiserikali la Korea (Good Neighbours) sawa na asilimia 40 na TSh.
832,000,000/- sawa na asilimia 25 kutoka SMZ.
30.
Mheshimiwa Spika, Utekelezaji kwa
programu hii ni kama hivi ifuatavyo: -
i).
Watahiniwa 23,380 wa skuli za sekondari
za Serikali waliofanya mitihani ya Kidato cha Nne mwezi Novemba, 2019
wamelipiwa TSh. 1,200,000,000/- ikiwa niada ya mitihani
ii).
Jumla ya TSh. 3,175,685,943/= za ruzuku
zimetolewa kwa skuli 204 za sekondari za Serikali kwa ajili ya uendeshaji baada
ya kufutwa michango ya wazee.
iii).
Jumla ya wanafunzi 59 wanaotoka maeneo
ya vijijini wanaosoma Skuli ya Sekondari ya SUZA wamelipiwa kiasi cha shillingi
23,010,000/- kwa ajili ya gharama za huduma ya chakula.
iv).
Jumla ya wanafunzi 89,240 wamepatiwa
vikalio kufuatia kununuliwa kwa seti 44,620 za viti na meza kwa ajili ya
wanafunzi wa skuli za Sekondari.
v).
Vifaa vya maabara na kemikali kwa ajili
ya Mitihani ya Taifa vimenunuliwa na kusambazwa katika skuli za sekondari 175
zenye madarasa ya kidato cha nne.Aidha, tathmini ya manunuzi ya vifaa vya
maabara kwa skuli 15 zenye madarasa ya kidato cha sita kwa Unguja na Pemba ipo
katika hatua ya mwisho.
vi).
Skuli za Sekondari za Ufundi ya
Mikunguni Unguja na Kengeja kwa Pemba zimepatiwa vifaa vya kufundishia na
kujifunzia masomo ya ufundi katika fani za Umeme, Ujenzi, Makenika na Kompyuta.
vii).
Taratibu za manunuzi ya madaftari 6,740,036
ya wanafunzi wa Sekondari zinaendelea. Ripoti ya tathmini iliwasilishwa Mamlaka
ya Manunuzi kwa ajili ya kupitiwa na kupata ushauri. Ushauri huo tayari
umeshawasilishwa na kwa sasa Wizara inaufanyia kazi.
viii).
Wanafunzi 1,571 wa Unguja na Pemba
wanaoishi dakhalia wamelipiwa jumla ya TSh. 453,240,000/= kwa ajili ya gharama
za huduma ya chakula.
ix).
Jumla ya walimu wapya 572 wameajiriwa wakiwemo
204 wa Sayansi na 368 wa Sanaa na wamepatiwa mafunzo elekezi na tayari wamepangiwa
kazi katika skuli za sekondari Unguja na Pemba.
x).
Jumla ya wanafunzi 18,601 wamefaulu
mtihani wa Kidato cha Nneuliofanyika Novemba, 2019 nawanafunzi 4,714
wataendelea na na masomo ya Kidato cha Tano katika skuli mbalimbali za Serikali
za Unguja na Pemba.
xi).
Jumla ya wanafunzi 2,687 wa Kidato cha
Sita wakiwemo 2,218 kutoka skuli za Serikali na 469 kutoka skuli binafsi ambao
walitarajiwa kufanya mitihani ya kumalizia Kidato cha Sita katika mwezi
Meihawakuweza kufanya mitihani yao kutokana na janga la maradhi ya Korona ambapo
skuli zote zimefungwa na mitihani imeakhirishwa mpaka litakapotolewa tamko
rasmi Serikalini.
xii).
Jumla ya washiriki 375 walipatiwa
mafunzo ya athari za utoro wa wanafunzi, lengo la mafunzo haya ni kuweza
kuihamasisha jamii ili kupunguza au kuondosha kabisa tatizo la utoro katika
skuli zetu.
xiii).
Jumla ya wanafunzi 10 wakiwemo sita kutoka
Unguja na wanne kutoka Pemba wamechanguliwa kujiunga na masomo ya Kidato cha
Kwanza katika Skuli za Mama Salma Kikwete za Mkoa wa Pwani Wilaya ya Rufiji na
Mkoa wa Lindi katika Wilaya ya Lindi.
xiv).
Skuli 10 za Unguja na Pemba zimejengewa
visima na matangi ya kuhifadhi maji kwa kushirikiana na Shirika lisilo la
kiserikali la Time to Help na Skuli ya Sekondari ya Feza. Skuli hizo ni
Sebleni, Paje, Mgambo, Mtende, Dimani, Fuoni na Chunga kwa Unguja na skuli ya
Wete, Kijumbani, Mizingani na Pujini kwa Pemba. Aidha ujenzi wa visima katika skuli
za Kandwi na Uzi Ng’ambwa kwa Unguja na Mgogoni kwa Pemba unaendelea.
xv).
Ujenzi wa kukamilisha Skuli ya Sekondari
ya Donge uliofanywa na mhisani kutoka Falme za Kiarabu kupitia shirika lisilo
la Kiserikali la Kinderhut umekamilika. Wizara imeipatia skuli hiyo seti 765 za
viti na meza kwa ajili ya madarasa yote. Aidha, skuli hiyo pia imepatiwa samani
kwa ajili ya walimu, maktaba, ofisi na maabara.
xvi).
Ujenzi wa Jengo jipya katika Skuli ya
Sekondari ya Biashara Mombasa lenye madarasa tisa uliofanywa kwa msaada wa
Mheshimiwa Ahmada Abdulwakil kupitia kampuni ya SHA umekamilika. Wizara
imeipatia skuli jumla ya seti 360 ya viti na meza.
xvii).
Ujenzi wa skuli 9 za sekondari za
ghorofa umekamilika licha ya kazi ndogo ndogo zilizobakia kwa skuli ya Muambe
na Kizimbani Pemba. Skuli hizi zilifunguliwa rasmi na Mheshimiwa Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein tarehe
05/01/2020 katika maadhimisho ya sherehe za miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Aidha, ujenzi wa Skuli ya Sekondari ya Kibuteni unaendelea.
xviii).
Ujenzi wa skuli tatu mpya za sekondari
za kisasa kwa ushirikiano na Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA)
umeanza rasmi mwezi Machi 2020. Utekelezaji umeanza kwa hatua ya kutangaza
zabuni na ununuzi wa gari mbili, ambazozitatumika kwa shughuli za ufuatiliaji
wa kazi za ujenzi. Aidha mialiko imetangazwa kwa ajili ya kupata kampuni za Ushauri
Elekezi za kusanifu michoro na kusimamia ujenzi kutoka Afrika na nchi za
Kiarabu.
Matokeo ya muda mfupi;
i.
Jumla ya wanafunzi 112,983
wameandikishwa katika ngazi ya Elimu ya Sekondari ya awali (kidato 1 – 4). Kati yao, wanafunzi 65,282 wa kidato cha
kwanza na pili wakiwemo wanaume 30,764na wanawake 34,518.Wanafunzi wa kidato
cha tatu na nne kina jumla ya wanafunzi
47,912 wakiwemo wanaume 22,641 na wanawake 25,271
ii.
Jumla ya wanafunzi 4,737 wameandikishwa
katika ngazi ya sekondari ya juu (kidato 5-6). Kati yao wanafunzi 2,519 ni wa
kidato cha tano wakiwemo wanaume 1,140 na wanawake 1,379 na wanafunzi 2,218 wa
kidato cha sita kati yao wanaume ni
1,090 na wanawake 1,128.
PROGRAMU
YA TATU: ELIMU YA JUU
31.
Mheshimiwa Spika, Madhumuni ya programu hii ni kutoa elimu itakayomuwezesha
muhitimu kujiajiri au kuajiriwa. Programu hii ina programu ndogo moja ambayo ni
mafunzo ya ualimu na maeneo manne ya huduma, ikiwemo Huduma ya Ushauri na
Utafiti, Huduma ya Sayansi na Teknolojia, Huduma ya Mikopo ya Elimu ya Juu na
Huduma ya Uratibu wa Elimu ya Juu. Utekelezaji wa programu hii ni kama
ifuatavyo: -
Programu
ndogo ya Mafunzo ya Ualimu
32.
Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo ilitengewa jumla ya TSh. 1,719,367,000/-
za SMZ kwa kuendelea kutoa mafunzo ya ualimu katika ngazi ya Stashahada na
kutoa mafunzo ya Ualimu kazini. Kati ya fedha hizo TSh. 534,531,000/- zilitengwa
kwa matumizi ya kawaida na TSh. 1,184,836,000/- kwa matumizi ya mshahara. Hadi kufikia Aprili, 2020, jumla ya TSh. 1,456,457,780/= sawa na asilimia 84.7 zilipatikana.
33.
Mheshimiwa Spika, utekelezaji halisi wa programu hii ndogo ni kama hivi
ifuatavyo: -
i).
Moduli mbili
za mwongozo wa mafunzo kazini kwa walimu wa Maandalizi na Msingi zimetayarishwa
kwa lengo la kuratibu mafunzo ili kuimarisha ufundishaji wa masomo kwa
wanafunzi wao.
ii).
Jumla ya walimu 392 wakiwemo wanawake 132 na wanaume 260 wa skuli za sekondari wamepatiwa
mafunzo ya ufundishaji wa mada zinazowapa ugumu katika kuzifundisha kwa masomo
ya Jiografia, Historia Kiingereza na Hisabati. Vile vile walimu hawa wamepatiwa
taaluma na mbinu za namna ya kuwafundisha wanafunzi njia bora za kujibu maswali
ambayo hayajibiwi vizuri katika mitihani ya Taifa.
iii).
Jumla ya walimu 639 wa Sanaa
wanaofundisha masomo ya Sayansi na Hisabati Kidato cha Kwanza na cha Pili
wanaendelea na mafunzo kazini ya kuwawezesha kufundisha masomo hayo kwa umahiri
katika vituo vya walimu vya Unguja na Pemba. Lengo la mafunzo hayo ni kupunguza
tatizo la uhaba wa walimu wa Sayansi na Hisabati katika skuli zetu za
sekondari. Pia, walimu hawa wanapatiwa mafunzo ya lugha ya Kiingereza ili
waweze kuitumia vizuri lugha hiyo katika kufundisha masomo husika. Hata hivyo,
mafunzo hayo yamesimamishwa kutokana na maradhi yanayosababishwa na virusi vya
Korona (COVID 19).
iv).
Jumla ya walimu 200 wa madarasa ya Tatu
na Nne wa lugha ya Kiingereza wamehudhuria mafunzo juu ya mbinu za kufundishia,
utamkaji wa maneno, matumizi ya wakati pamoja na imla kwa wanafunzi wa madarasa
hayo.
v).
Jumla ya walimu 1,341 wamehudhuria
mafunzo ya ufundishaji wa somo la Hisabati. Kati ya walimu hao 284 ni Walimu
Wakuu na 1,057 ni Walimu wa somo hilo kwa madarasa ya Kwanza na Pili.
vi).
Jumla ya vitabu 7,500 kwa ajili ya
mafunzo ya Elimu Masafa vimechapwa na kusambazwa katika vituo vya Walimu Unguja
na Pemba.
vii).
Jumla ya walimu wanafunzi 529 wamefanya
mitihani ya Elimu Masafa daraja la 3A. Wanafunzi tisa wamefanya mitihani maalum
kutokana na kutofanya mitihani ya awali kwa sababu ya ugonjwa na 98 wamerudia
baadhi ya masomo. Matokeo ya mitihani hiyo yameonesha kwamba wanafunzi
wamefanya vizuri katika masomo yote isipokua somo la Hesabati.
viii).
Jumla ya ziara 80 za ufuatiliaji
utekelezaji wa mafunzo ya Elimu Masafa zimefanyika katika vituo tisa vya walimu
Unguja na Pemba. Matokeo yanaonesha kwamba hali ya ufundishaji ipo vizuri.
ix).
Jumla ya ziara 1,470 zimefanywa katika
skuli za Serikali na Binafsi Unguja na Pemba. Aidha, jumla ya walimu 2,651 wa
ngazi zote wamepatiwa mafunzo na ushauri juu ya matumizi ya zana za kufundishia
pamoja na kuwapatia taaluma ya utungaji wa
maswali ya mitihani.
x).
Jumla ya Wakufunzi 56 wa Chuo cha
Kiislamu wa masomo yote wamepatiwa mafunzo ya uandaaji wa zana za tathmini ili
waweze kutunga mitihani inayokidhi viwango vya ubora. Katika mafunzo hayo aina
za maswali, sheria za utungaji, sifa za maswali pamoja na mambo ya kuzingatia
katika kuandaa mtihani yalijadiliwa.
xi).
Tathmini ya awali juu ya ufundishaji wa
somo la Kiingereza Unguja na Pemba imefanyika. Jumla ya walimu 120 wa Darasa la
Kwanza na Sita walishiriki katika tathmini hiyo. Matokeo yameonesha kuwa walimu
wanahitaji taaluma zaidi juu ya utamkaji sahihi wa maneno ya Kiingereza na
kutofautisha wakati. Kati yao Walimu 108 wamepatiwa mafunzo ya somo hilo kwa
awamu ya kwanza.
xii).
Mapitio na marekebisho yamefanywa katika
Mwongozo wa kazi Namba.11 kuhusu Vituo vya Walimu. Muongozo huu uliandaliwa kwa
walimu wa Msingi tu kwa wakati ule. Kwa hivyo ulihitaji marekebisho ili uweze
kutumika pia katika ngazi za Maandalizi na Sekondari.
xiii).
Jumla ya wanafunzi 800 (600 Unguja na
200 Pemba) kautoka skuli 80 (60 Unguja na 20 Pemba) za Maandalizi wameshiriki
katika mashindano ya kusoma na kuandika herufi na silabi. Lengo ni kuwatathmini
walimu wa maandalizi katika ufundishaji wao. Matokeo ya mashindano hayo
yanathibitisha kazi nzuri inayofanywa na walimu. Mashindano haya yameweza
kuongeza ari ya ufundishaji kwa walimu wa Maandalizi.
Matokeo ya muda mfupi
i)
Jumla ya wanafunzi 976 wanasomea
mafunzo ya Ualimu kwa ngazi ya Cheti cha Maandalizi, Stashahada ya Dini na
Kiarabu, Stashahada ya Sayansi Jamii, Stashahada ya Elimu ya Msingi kwa Unguja
na Pemba na Cheti cha Elimu Mjumuisho kwa Unguja. Kati yao, wanafunzi 702 wakiwemo wanaume 120 na
wanawake 582 wanasomea Ualimu katika Chuo cha Kiislamu Mazizini Unguja na
wanafunzi 274 wakiwemo wanaume 67 na wanawake 207 katika Chuo cha Kiislamu
Kiuyu Pemba.
Huduma ya Elimu ya Juu,
Ushauri na Utafiti
34.
Mheshimiwa Spika, Huduma ya Elimu ya
Juu, Ushauri na Utafiti ina lengo la kuwaandaa wanafunzi kuingia katika fani za
kitaalamu na ajira. Huduma hii inatolewa katika Vyuo vikuu vitatu vilivyopo
Zanzibar ambavyo ni Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA), Chuo cha
Kumbukumbu ya Abdulrahman Al-Sumait cha Chukwani na Chuo Kikuu cha Zanzibar
Tunguu.
35.
Mheshimiwa Spika, ngazi hii ya elimu ina
jumla ya wanafunzi 7,303 wanaosoma katika vyuo vikuu vitatu. Kati ya wanafunzi
hao, 3,112 ni wanaume na 4,191ni wanawake. Kwa mwaka wa fedha wa 2019/20, Chuo
Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kilitengewa ruzuku ya TSh.
11,239,100,000/-. Kati ya fedha hizo TSh. 500,000,000/- zilitengwa kwa matumizi
ya kawaida na TSh. 10,739,100,000/- kwa matumizi ya mishahara. Hadi kufikia
Aprili, 2020, jumla ya TSh. 10,666,409,562/= sawa na
asilimia 95zimepatikana.
36.
Mheshimiwa Spika, utekelezaji halisi wa
huduma hii ni kama hivi ifuatavyo: -
i).
Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar
kimezindua skuli skuli ya Kilimo, Skuli ya Utibabu wa Meno na Taasisi ya Masomo
ya Ubaharia. Aidha, Chuo kimeanzisha programu mpya nne ambazo ni Shahada ya
kwanza ya Uuguzi, Shahada ya Kwanza ya Sayansi na Kilimo, Shahada ya Utabibu wa
Meno na Shahada ya Uzamili ya Lugha na Elimu.
ii).
Jumla ya wanafunzi wapya 2,200
wa masomo ya ngazi mbalimbali wa SUZA
wamedahiliwa.
iii).
Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar kilifanya mahafali ya kumi na tano (15) tarehe 31/12/2019. Katika
mahafali hayo, Mkuu wa Chuo ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein aliwatunuku shahada, stashahada na vyeti
wahitimu 1,716 (wanaume 790 wanawake 926) waliohitimu katika programu
mbalimbali.
iv).
Mhadhiri Msaidizi mmoja
ameajiriwa katika taaluma ya Afya. Aidha, Chuo kimeendelea kuwalipia ada za
masomo wafanyakazi wake 50 ambao wapo masomoni kwenye ngazi za Shahada ya
Uzamivu (27), Shahada ya Uzamili (19), Shahada ya Kwanza (4).
Matokeo ya muda mfupi;
i.
Jumla ya wanafunzi 4,808
wameandikishwa katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA). Kati ya
wanafunzi hao, wanaume ni 2,070 na wanawake ni 2,738. Jadweli Nambari 26(g)
linatoa ufafanuzi zaidi.
ii.
Jumla ya wanafunzi 1,716 (790
wanaume na 926 wanawake) wamehitimu SUZA na kutunukiwa Stashahada, shahada,
shahada ya uzamili na shahada ya uzamivu katika mahafali ya 15 yaliyofanyika
katika Kampasi ya Tunguu, tarehe 31 Disemba 2019.
iii.
Jumla ya wanafunzi 875 wakiwemo
wanaume 363 na wanawake 512 wameandikishwa katika Chuo cha Kumbukumbu ya
Abdulrahman Al-Sumait cha Chukwani. Jadweli namba 27 linatoa ufafanuzi zaidi.
iv.
Jumla ya wanafunzi 1,620
wameandikishwa katika Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu, kati yao wanaume ni 679
na wanawake 941 Jadweli namba 28 linatoa ufafanuzi zaidi.
Huduma ya Sayansi na
Teknolojia
37.
Mheshimiwa Spika, Huduma ya Sayansi na
Teknolojiaina madhumuni ya kuimarisha elimu ya sayansi na teknolojia nchini Shughuli
za huduma hii zinatekelezwa na Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia. Kwa mwaka 2019/20, Taasisi
ilitengewa ruzuku ya TSh. 1,626,000,000/-. Kati ya fedha hizo, TSh.
420,100,000/- ni kwa ajili ya matumizi ya kazi za kawaida na TSh. 1,205,900,000/-
ni kwa matumizi ya mishahara. Hadi
kufikia Aprili, 2020, jumla ya TSh. 1,393,132,060/= sawa na asilimia
86zilipatikana.
38.
Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi wa huduma hii
kwa mwaka 2019/20 ni kama ifuatavyo: -
ii).
Jumla
ya wanafunzi wapya 343, wanaume 236 na wanawake 107 kwa fani zote za Taasisi
wameandikishwa.
iii).
Wafanyakazi
wapya 19, kati yao 15 wa kada ya wakufunzi na wanne wa kada za uendeshaji
wameajiriwa.
iv).
Mafunzo
mapya ya kuiendeleza Taasisi na yale ya kuisaidia jamii kwa kutumia Sayansi na
Teknolojia yameanzishwa.
Matokeo ya muda Mfupi
Jumla ya wanafunzi 1,529 wakiwemo wanaume 1,297na wanawake 232 wanaendelea na masomo katika fani mbalimbali
zikiwemo Shahada ya Urubani na Uhandisi wa ndege, Stashahada za Uhandisi, Stashahada ya Teknolojia ya Habari Mawasiliano na Biashara, Stashahada ya
Mafunzo ya Hisabati na Sayansi kwa Skuli za Msingi, Stashahada mafunzo ya Ualimu (VTA), Stashahada
ya Usimamizi wa Maabara na Cheti kwa Mafunzo
ya Amali (VETA). Jadweli nambari 29 linatoa ufafanuzi Zaidi.
Huduma ya Mikopo ya Elimu ya Juu
39.
Mheshimiwa Spika, Bodi ya Mikopo ya
Elimu ya Juu Zanzibar inatoa mikopo kwa wanafunzi wanaojiunga na wanaoendelea na masomo ya elimu ya juu
katika fani mbalimbali ndani na nje ya nchi. Kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020, Bodi
ilitengewa jumla ya TSh. 10,298,600,000/-.
Hadi kufikia Aprili 2020, jumla ya TSh. 6,706,532,312/= sawa na asilimia 65 ya makadirio zilipatikana.
40.
Mheshimiwa Spika,Utekelezaji halisi wa programu hii
ni kama ifuatavyo: -
i)
Jumla ya wanafunzi 4,081 wamepatiwa
mikopo ya elimu ya juu wakiwemo wanafunzi wapya 1,860 na 2,221 wanaoendelea na
masomo. Idadi hii imeongezeka kwa 562 sawa na asilimia 16 ukilinganisha na
mwaka 2018/2019.
ii)
Wanafunzi 72 wamepatiwa nafasi za
ufadhili wa masomo nje ya nchi zilizotolewa na washirika wa maendeleo
mbalimbali wakiwemo Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China (30), Serikali ya
Falme ya Oman (5), Falme ya Ras Al-Khaimah (4), Sudan (10), Algeria (8) na
Malaysia (15).
iii)
Wanafunzi 108 wakiwemo wapya 60 na wanaoendelea
na masomo 48 wamepatiwa ufadhili wa masomo wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zasnzibar kutokana na ufaulu wao wa ngazi ya juu katika mtihani wa Kidato cha
Sita.
iv)
Jumla ya wanafunzi wapya 38 wamepatiwa
ufadhili wa masomo kwa vyuo vya ndani ya nchi wakiwemo 27 kupitia taasisi za
Darul Imaan katika Chuo Kikuu cha Zanzibar kilichopo Tunguu na 11 kupitia Shirika la “Direct Aid”
lililotoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Abdulrahman
Al-Sumait cha Chukwani.
v)
Jumla ya wanafunzi 987 wakiwemo
wanafunzi 666 wanaosoma vyuo vya Zanzibar, 231 katika vyuo vya Tanzania Bara na
90 wa vyuo vya nje ya Tanzania wanatarajiwa kuhitimu masomo yao katika fani
na ngazi mbalimbali.
41.
Mheshimiwa Spika,Bodi ilitarajia kukusanya TSh. 2,300,000,000/= ikiwa
ni marejesho ya mkopo hadiifikapo mwezi wa Juni, 2020. Hadi kufikia mwezi
Aprili, 2020, jumla ya TSh. 1,970,000,000/= sawa na asilimia 85.6 ya lengo
lililowekwa zimekusanywa.
Huduma ya Uratibu wa Elimu
ya Juu
42.
Mheshimiwa Spika, Huduma ya Uratibu wa
Elimu ya Juuina jukumu la kusimamia na kutathmini maendeleo ya elimu ya juu.
Huduma hii inatekelezwa na Kitengo cha Uratibu wa Elimu ya Juu, Sayansi na
Teknolojia. Kwa mwaka 2019/20 Kitengo kilitengewa jumla ya TSh. 50,000,000/=
kutoka Serikalini. Hadi kufikia Aprili 2020, jumla ya TSh. 28,000,000/= sawa na
asilimia 56 zimepatikana. Utekelezaji halisi ni kama ifuatavyo: -
i)
Nafasi za masomo kwa ufadhili kutoka Jumuiya
ya Afrika Mashariki na nchi za China, Algeria, Morocco, , Malaysia, Poland,
Nelson Mandela, Queen Elizabeth, Hungary, na Jumuiya ya Madola zimetangazwa.
Nafasi hizo zilijumuisha fani mbalimbali zikiwemo; Udaktari, Uchumi, Uhandisi,
Uuguzi na Sayansi ya Mazingira, Kilimo, Chakula na Lishe, Usimamizi wa Biashara
na Utawala kwa viwango vya Shahada ya Kwanza, ya Pili na ya Tatu. Jumla ya
waombaji 112 wakiwemo wanaume 78 na wanawake 34 waliwasilisha maombi yao. Kati
yao, wanafunzi 38 (wanaume 27 na wanawake 11) wamenufaika na nafasi hizo.
Matokeo ya muda mfupi;
i.
Jumla ya wahitimu 1,120 wa fani
mbalimbali zikiwemo Kilimo, Mazingira, Uongozi wa Fedha, Udaktari wa Meno kwa
kiwango cha Stashanada, Shahada ya Kwanza na , Shahada ya Uzamili waliripoti
kwa kujitambulisha na orodha wa wahitimu hao na fani zao za masomo
zimewasilishwa Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
PROGRAMU YA NNE: ELIMU
MBADALA NA MAFUNZO YA AMALI
43.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kutoa Elimu ya Mafunzo ya Amali na Elimu Mbadala kwa wanafunzi
kulingana na mahitaji ya soko la ajira. Programu hii ina programu ndogo mbili;
Mafunzo ya Amali na Elimu Mbadala na Watu Wazima.
Programu ndogo ya Mafunzo
ya Amali
44.
Mheshimiwa Spika, programu hii ndogo ilikuwa
na madhumuni ya kutoa elimu itakayowawezesha vijana kujiajiri ili kujikwamua na
umasikini na ilitengewa jumla ya ruzuku ya TSh.7, 761,200,000/-. Hadi kufikia
Aprili, 2020, jumla ya TSh. 4,916,633,665/= kutoka SMZ
zilipatikana sawa na asilimia 63.
45.
Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi kwa
programu hii ni kama hivi ifuatavyo: -
i)
Jumla ya vikundi vitano (viwili Unguja
na vitatu Pemba) vimepatiwa mkopo wenye thamani ya TSh. 33,850,550/-. Mkopo huu
unalenga kuwawezesha vijana kujiajiri.
ii)
Mamlaka imesimamia ufanyaji wa Mtihani
wa Taifa wa MMA kwa wanafunzi wa vituo 15 vikiwemo vitatu vya Serikali na 12
vya binafsi ambapo jumla ya wanafunzi 1,875 (1,255 wanaume na wanawake 620)
walishiriki katika mitihani hiyo.
iii)
Ujenzi wa Vituo vya Mafunzo ya Amali vya
Makunduchi na Daya unaendelea na umefikia asilimia 79 kwa Makunduchi na
asilimia 87 kwa Daya.
iv)
Jumla ya vituo 24 vya binafsi vinavyotowa
mafunzo ya amali vimefanyiwa ukaguzi wa kawaida kwa lengo la kuangalia kiwango
pamoja na kutoa maelekezo ya njia nzuri za utoaji wa mafunzo ya fani husika.
Aidha, vituo 16 vimefanyiwa ukaguzi wa usajili ambapo vituo viwili vimepatiwa
usajili wa kudumu na vituo 14 vimepatiwa usajili wa muda. Vituo vilivyopatiwa
usajili wa kudumu ni Muna Beauty Academy na Melisha Computer Training Center.
Aidha, vituo vilivyopatiwa usajili wa muda ni Experience Vocational Training
Center, Wingwi Alternative Learning Center, Zanzibar Technical Center, ICPS
Vocational Training Center, Zanzibar Commercial Technical Training Center,
Ikigai Center for Career Training, Zanzibar Aviation Training Center, Dodeani
Vocational Training Center, Center for Professional and Vocational Training,
Rahaleo Alternative Learning Center, ZAWA Training Center, Babel Center for
Proffesional Studies, Hamasika Tailoring and Designing Vocational Training and
Noah Training Center.
v)
Mamlaka imewalipia wafanyakazi wake tisa
masomo ya muda mrefu wakiwemo watano wanaoendelea na masomo na wanne wapya. Pia
imewapatia wafanyakazi 22 udhamini wa masomo ya muda mfupi ya Domain name and security extention (mfanyakazi mmoja),mafunzo ya matengenezo ya
simu za mkononi (13), mafunzo ya Sheria ya Manunuzi (2) na wafanyakazi sita
walipatiwa mafunzo ya Quick Book.
vi)
Jumla ya wanafunzi 472 wanaoishi
dakhalia ya Mkokotoni (320) na Vitongoji (152) wanapatiwa huduma ya chakula ya
milo mitatu kwa siku.
vii) Jumla ya vijana wa kike 147 wamepatiwa mafunzo ya ukulima na usarifu
wa mwani katika maeneo ya Paje, Unguja Ukuu, Matemwe na Kidoti kwa Unguja
na maeneo ya Kuukuu Kangani, Chokocho,
Kisiwa Panza, Chwale, Kiungoni, Msuka, Gando, Shumba mjini, Tumbe na
Maziwang’ombe kwa Pemba.
Matokeo ya muda mfupi;
i.
Jumla ya vijana wapya 250 (wanaume
138 na wanawake 112) wamejiunga na vituo vya Mamlaka ya Mafunzo ya Amali
mwanzoni mwa mwaka 2020.
ii.
Jumla ya TSh. 21,773,050/=
zimerejeshwa na vikundi vya vijana vilivyopatiwa mkopo wa kuweza kujiajiri.
iii.
Jumla ya vijana 1,875 wa Vituo
vya Mwanakwerekwe, Mkokotoni na Vitongoji wamehitimu mafunzo yao. (Wanaume 1,255
na wanawake 620).Wanafunzi 1,113 kati ya hao sawa na asilimia 59 wamefaulu
mitihani yao.
Programu ndogo ya Elimu
Mbadala na Watu Wazima
46.
Mheshimiwa Spika, Programu hii
inatekelezwa na Idara ya Elimu Mbadala na Watu Wazima na ina lengo la kupunguza kiwango cha wasiojua kusoma,
kuandika na kuhesabu miongoni mwa wanajamii. Kwa mwaka wa fedha 2019/20,
programu hii ilitengewa jumla ya TSh. 8,974,245,000/-. Kati ya hizo, TSh.
535,304,000/- zilitengwa kwa kazi za kawaida, TSh. 438,941,000/- kwa matumizi
ya mshahara na TSh. 8,000,000,000/- ni kwa kazi za maendeleo. Kati ya fedha za
maendeleo TSh. 1,000,000,000/- ni mchango wa SMZ na TSh.7, 000,000,000/- ni
kutoka ADB. Hadi kufikia Aprili, 2020, jumla ya TSh. 7,837,587,279/= sawa na
asilimia 87 zilipatikana. Kati ya fedha hizo, TSh. 7,205,441,846/- ni
kwa kazi za maendeleo ambazo ni sawa na asilimia 90 zikiwemo TSh. 171,046,000/=
za SMZ sawa na asilimia 17.1. Aidha, jumla ya TSh. 632,145,433 kwa matumizi ya
kawaida sawa na asilimia 65 zimepatikana.
47.
Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi wa
shughuli za programu hii ni kama ifuatavyo: -
i)
Madarasa 47 mapya ya kisomo kwa
Unguja na Pemba yamefunguliwa. Idadi ya madarasa ya kisomo imefikia 528 mwaka
2020 kutoka 521 mwaka 2019. Aidha, jumla ya wanakisomo 7,874 wa kisomo cha Watu
Wazima wamefanyiwa upimaji katika hatua zote nne za kisomo. Wanafunzi 474 wa
hatua ya nne wamekombolewa kupitia upimaji huo.
ii)
Maadhimisho ya Juma la Elimu ya
Watu Wazima yamefanyika. Uzinduzi wa Juma hilo ulifanyika katika Wilaya ya
Chake Chake Pemba katika Skuli ya Madungu Sekondari na kilele kilifanyika
Wilaya ya Kati Unguja.
iii)
Jumla ya vikundi 117 (71 Unguja
na 46 Pemba) vyenye jumla ya wanachama 2,583 vimeendelezwa kwa lengo la
kuwapunguzia utegemezi wanawake na umasikini wa kipato.
iv)
Jumla ya wanafunzi 863 (wanaume
365 na wanawake 498) wamesajiliwa katika vituo vya kujiendeleza Unguja na
Pemba. Aidha, wanafunzi 71 (wanaume 6 na wanawake 65) walioshindwa kuendelea na
masomo yao baada ya mtihani wa Kidato cha Pili na cha Nne wameandikishwa katika
Kituo cha Sayansi Kimu Forodhani kusomea fani ya Upishi, Ushoni, Kudarizi na
Kufuma.
v)
Walimu 26 wa Vituo vya Elimu
Mbadala wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo.Pia, viongozi mbali mbali
wakiwemo Makatibu Tawala, Wenyeviti na Makatibu wa Mabaraza ya Madiwani,
Maafisa Ustawi, Masheha, Umoja wa Vijana, Jumuia ya Wazazi, Maafisa Elimu
Sekondari na Walimu wakuu walihudhuria semina ya uhamasishaji wa kutambua
programu ya Elimu Mbadala.
vi)
Vipindi 20 vya Elimu Mbadala na
Watu Wazima viliandaliwa na kurushwa hewani kupitia Shirika la Utangazaji la
Zanzibar kwa ajili ya kuielimisha jamii juu ya umuhimu wa programu zinazotolewa
na Idara ya Elimu Mbadala na Watu Wazima zenye lengo la kuhamasisha
uandikishaji wa wanafunzi katika vituo ili wapate elimu itakayowakomboa na
changamoto za kijamii na kiuchumi.
Matokeo ya muda mfupi;
i.
Jumla ya wanakisomo 690
wameandikishwa wakiwemo wanaume 48 na wanawake 642.
ii.
Jumla ya wanafunzi 1,254 wenye
umri wa miaka 9 hadi 14 waliokuwa nje ya mfumo rasmi wa elimu wameandikishwa
katika madarasa ya Elimu Mbadala. Kati ya hao, wanafunzi 677 wameandikishwa
Unguja na 577 kwa Pemba wakiwemo wanaume 827 na wanawake 427.
iii.
Jumla ya wanafunzi 401 wenye
umri kati ya miaka 15 hadi 22 wameandikishwa katika Kituo cha Elimu Mbadala
Rahaleo Unguja na Kituo cha Wingwi Mtemani Pemba. Kati yao, wanaume 267 na
wanawake 134. Vijana hawa wanasomea fani za Umeme, Ushoni, Upishi, Udobi,
Uchoraji, Kilimo, Ufugaji, Useremala, Mafunzo ya Kompyuta na Utunzaji Nyumba
pamoja na masomo ya kawaida.
iv.
Jumla ya watahiniwa 4,155
wamefanya mtihani wa faragha wa Kidato cha Nne, kati yao wanafunzi 1,599 sawa
na asilimia 38.5 ya watahiniwa wote wamefaulu. Aidha, wanafunzi 141 kati ya 219
waliofanya mtihani wa faragha wa Kidato cha Sita mwezi Mei, 2019 kwa Unguja na
Pemba ambao ni sawa na asilimia 63.3 wamefaulu.
PROGRAMU YA TANO: UBORA WA ELIMU
48.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina lengo la kutoa elimu bora kwa
ngazi zote za elimu. Progamu hii ina jumla ya programu ndogo tatu na
maeneo matano ya kutoa huduma kama yafuatayo: -
Huduma ya Mitaala na Vifaa
vya Kufundishia
49.
Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina
madhumuni ya kutayarisha mitaala ya elimu na kuratibu upatikanaji wa vifaa vya
kufundishia na kujifunzia kwa
ngazi za elimu ya maandalizi, msingi, sekondari na mafunzo ya
Ualimu. Shughuli za utoaji wa huduma hii zinatekelezwa na Taasisi ya Elimu
Zanzibar. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, Taasisi ilitengewa ruzuku yenye jumla ya
TSh. 573,100,000/-. Kati ya fedha hizo TSh. 301,600,000/- ni kwa kazi za
kawaida na TSh. 271,500,000/- kwa matumizi ya mshahara. Hadi kufikia Aprili,
2020, jumla ya TSh. 503,978,320/= sawa na asilimia 88 zilipatikana.
Utekelezaji halisi wa huduma hii ni kama ifuatavyo:-
i)
Muundo wa Paneli za mitaala za
Kitaifa kwa ngazi ya Elimu ya Maandalizi, Msingi na kwa vituo 10 vya walimu
(vituo sita Unguja na vinne Pemba) umeandaliwa. Aidha, Muundo wa utumishi wa
taasisi, mpango mkakati na muongozo wa vigezo vya kuandika na kutathmini vitabu
vya kiada na ziada vipo katika hatua ya mwisho kukamilika.
ii)
Rasimu za Kanuni za Sheria ya
Taasisi ya Elimu ya Zanzibar zimeandaliwa.
iii)
Jumla ya Skuli 34 za maandalizi
na msingi zikiwemo 23 za Serikali na 11 binafsi zilifuatiliwa Unguja na Pemba
katika kuendelea na kuimarisha utekelezaji wa mitaala.
iv)
Mapitio ya Mtaala wa Elimu ya
Maandalizi na Msingi yanaendelea. Jumla ya mikutano 16 iliyowashirikisha wadau
1,074 wa elimu Unguja na Pemba imefanyika kwa lengo la kupata maoni zaidi. Rasimu
ya awali ya Mtaala imewasilishwa Serikalini na kutolewa mapendekezo na ushauri
mbali mbali..
v)
Jumla ya wafanyakazi 23
wamepatiwa mafunzo ya muda mfupi ya ukuzaji mitaala. Wafanyakazi watatu
wanaendelea na mafunzo ya muda mrefu ambapo wawili katika shahada ya uzamili
fani ya uongozi katika elimu na uongozi wa fedha na mmoja shahada ya uzamivu
(Kiswahili).
Huduma ya Upimaji na
Tathmini ya Elimu
50.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kupima na kutathmini utekelezaji
wa utoaji wa elimu. Shughuli za huduma hii zinatekelezwa na Baraza la Mitihani
la Zanzibar. Kwa mwaka wa 2019/20 ya huduma ya Upimaji na Tathmini ilitengewa
ruzuku ya TSh. 4,941,800,000/-. Kati ya fedha hizo TSh. 4,517,000,000/-
zilitengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida TSh. 424,800,000/- kwa matumizi ya
mishahara. Hadi kufikia Aprili, 2020,
jumla ya TSh. 4,319,112,010/= ambazo ni sawa na asilimia 87 zilipatikana.
Utekelezaji halisi wa shughuli za huduma ya Upimaji na Tathmini ni kama
ifuatavyo: -
i)
Jumla ya wanafunzi 55,631 (wanaume 28,252 na wanawake 27,379) wa darasa
la Nne walisajiliwa kufanya mtihani wa
kuwapima maendeleo yao kitaaluma katika ngazi ya elimu ya msingi chini (Darasa
la Kwanza hadi la Nne) na uwezo wa kuendelea na darasa la elimu ya msingi juu
(darasa la tano). Wanafunzi halisi waliofanya mtihani huu ni 52,307 sawa na
asilimia 94 ya walioandikishwa wakiwemo wanaume 26,429 na wanawake 25,878.
ii)
Jumla ya wanafunzi 31,185 (wanaume ni
14,552 na wanawake ni 16,633) wa Darasa la Sita ambao ni sawa na asilimia 96.5
ya waliosajiliwa walifanya mtihani wa kumalizia elimu ya msingi. Kati ya watahiniwa hao, 1,508 walifaulu
kuendelea na masomo katika madarasa ya mchepuo, wanafunzi 194 walifaulu
kuendelea na masomo katika madarasa ya vipawa maalumu, wanafunzi 1508 walifaulu
madarasa ya mchepuo na wanafunzi 28,717 wamefaulu kuendelea na masomo ya Kidato
cha Kwanza katika madarasa ya kawaida.
iii)
Jumla ya wanafunzi 32,476 sawa na
asilimia 94.2 kati ya wanafunzi 34,473 waliosajiliwa walifanya mtihani wa
kumaliza Kidato cha Pili, wakiwemo wanaume 14,725 na wanawake 17,751. Jumla ya
wanafunzi 24,946 sawa na asilimia 76.8wamefaulu na kuendelea na masomo ya
Kidato cha Tatu.
iv)
Jumla ya walimu wanafunzi 316 (Unguja na
Pemba) watakaofanya mitihani ya kumalizia masomo yao ya Stashahada ya Ualimu wa
ngazi ya Msingi na ngazi ya Sekondari katika Vyuo vya Kiislamu vya Mazizini
Unguja na Kiuyu Pemba wamesajiliwa. Kati ya hao, 263 ni wanawake na 53 ni
wanaume.
v)
Kazi ya kuupitia na kuufanyia
marekebisho Mfumo wa Upimaji na Tathmini wa Baraza la Mitihani la Zanzibar
inaendelea.
Matokeo ya Muda mfupi;
i.
Jumla ya wanafunzi waliofaulu
mtihani wa Darasa la Nne ni 42,110 sawa na asilimia 80.5, Kati ya hao, wanaume 19,337 sawa na asilimia 37.0 na
wanawake ni 22,773sawa na asilimia 43.5 ya watahiniwa wote.
ii.
Wanafunzi waliofaulu mtihani wa
kumaliza Darasa la Sita ni 30,419 sawa na asilimia 97.5 ya watahiniwa wote
(wanaume ni 13,902 sawa na asilimia 44.6 na wanawake ni 16,517 sawa na
asilimia 53) .
iii.
Wanafunzi 24,946 kati ya waliofanya mtihani wa kumaliza Kidato cha Pili ambao ni
sawa na asilimia 76.8 wamefaulu kuendelea na masomo yao ya Kidato cha tatu (wanaume ni 10,017 na wanawake ni
14,929).
Huduma ya Ukaguzi wa Elimu
51.
Mheshimiwa Spika, utoaji wa huduma hii
una madhumuni ya kusimamia ubora wa elimu itolewayo kwa kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa
inafuata sera, sheria, miongozo
na taratibu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali. Shughuli za huduma hii zinatekelezwa na Ofisi
ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu. Kwa mwaka wa
fedha 2019/20, huduma hii imepangiwa jumla ya ruzuku ya TSh. 1,090,500,000/-, kati
ya fedha hizo TSh. 333,600,000/- ni kwa kazi za kawaida na TSh. 756,900,000/- ni
kwa ajili ya mshahara. Hadi kufikia
Aprili, 2020, jumla ya TSh. 809,277,751/= zilipatikana ambazo ni sawa na
asilimia 74. Utekelezaji halisi ni kama ifuatavyo: -
i)
Jumla ya skuli 595 (470 za Serikali na
125 za binafsi) Unguja na Pemba sawa na asilimia 80.5 ya makadirio ya skuli
zilizopangwa kukaguliwa zimekaguliwa. Kati ya skuli hizo 399 ni za Maandalizi
na msingi, 196 za sekondari. Aidha,
skuli 28 zimekaguliwa kwa ajili ya kupatiwa usajili.
ii)
Jumla ya walimu 1,857 wamekaguliwa na
kupewa ushauri kulingana na masomo wanayofundisha, Unguja na Pemba.
Huduma za Maktaba
52.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kutoa fursa ya kutumia vitabu na nyenzo nyengine za taaluma kwa
watoto, wanafunzi wa ngazi zote
na watu wote. Shughuli za huduma hii zinatekelezwa na Shirika la Huduma za
Maktaba Zanzibar. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, huduma hii ilipangiwa kutumia
ruzuku yenye jumla ya TSh. 886,200,000/-.Kati ya fedha hizo TSh. 493,100,000/-
kwa kazi za kawaida na TSh. 393,100,000/- zilitengwa kwa matumizi ya mshahara.
Hadi kufikia Aprili, 2020 jumla ya TSh. 586,049,457/= sawa na asilimia 66
zilipatikana.
Utekelezaji halisi wa shughuli za huduma hii ni kama ifuatavyo: -
i)
Jumla ya vitabu vya msaada 25,341 kutoka
Shirika la ‘Book Aid International”
la Uingereza vimepokelewa na kusambazwa katika taasisi mbali mbali za elimu Unguja
na Pemba. Aidha, vitabu 5,649 vimegaiwa katika taasisi 32 za elimu Unguja na
Pemba. Taasisi husika ni Skuli 17 za msingi zimepatiwa vitabu 2,452, Skuli 11
za sekondari zimepatiwa vitabu 2,048 na vituo cha vya Mafunzo ya Amali (Vitongoji na Mwanakwerekwe)
vimepatiwa vitabu 380 na vitabu 769 vimepatiwa Chuo cha Mwenge Community na
Chuo cha Pemba School of Health Science.
ii)
Programu 101 za watoto
zilizowashirikisha watoto 5,644 zimefanyika. Miongoni mwa programu hizo,
programu 82 zilifanyika ndani ya Maktaba Kuu na programu 19 zilifanyika nje ya
Maktaba.
iii)
Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya
kujua kusoma na kuandika (International Literacy Day) yalishirikisha watu 893
(450 Unguja na 443 Pemba) wakiwemo wanafunzi, walimu, wazazi, waandishi wa
vitabu na viongozi mbalimbali yalifanyika katika viwanja vya Maktaba Kuu
Maisara kwa Unguja na Maktaba ya Chakechake kwa Pemba.
iv)
Mdahalo wenye mada ya “Nini kifanyike
ili idadi ya watumiaji wa huduma za maktaba iongezeke”ulifanyika. Jumla ya
washiriki 170 walitoa maoni yao juu ya kuimarisha huduma za maktaba nchini.
Mdahalo huo ulifanyika katika Maktaba Kuu za Unguja na Pemba. Aidha katika
midahalo hiyo, tovuti ya Shirika la Huduma za Maktaba (www.zls.go.tz) ilizinduliwa
rasmi.
v)
Jumla ya programu 18za Kiingereza za “Youth English Corner” (9 za nje na 9 za
ndani) kwa vijana zimefanyika nakuwashirikisha vijana 516. Programu hizi
zinaendeshwa kwa mashirikiano na jumuiya isiyo ya Kiserikali ya “Youth Empowerment and Change”.
vi)
Programu mbalimbali za kijamii kupitia
Kitengo cha “American Corner” zinaendeshwa kwa mashirikiano na Shirika la
Huduma za Maktaba na Ubalozi wa Marekani. Jumla ya wanajamii 8,513 walipatiwa
huduma kupitia kitengo hicho. Watu 4,997 (3,526 wanaume na wanawake 1,471) walipatiwa
huduma za kompyuta na 2,419 (1,385 wanaume na 1,034 wanawake) walipatiwa huduma
ya kusoma vitabu.
vii)
Huduma za maktaba kwa njia ya shamiana
ilitolewa katika viwanja vya Skuli ya Fuoni Unguja na Skuli ya Madungu kwa Pemba.
Jumla ya wanafunzi 714 walishiriki na kupata fursa ya kusoma vitabu na kupatiwa
maelezo yanayohusu shughuli zinazofanywa na maktaba zetu.
viii)
Mafunzo yaliyolenga kuwaongezea uwezo
wafanyakazi na kuwawezesha kukabiliana na ukuaji wa teknolojia ya habari na
mawasiliano kwa wakutubi wa maktaba za umma na maktaba za skuli yalitolewa.
Mafunzo hayo yalijadili mada za masuala ya ubunifu na mabadiliko (innovation and transformation), namna
nzuri ya kutoa huduma kwa mteja (customer
care) na huduma kwa kutumia mtandao (search 4 life). Jumla ya wakutubi 70
walishiriki katika mafunzo hayo.
Matokeo ya Muda Mfupi
i.
Jumla ya wanachama wapya 257
walisajiliwa katika Maktaba za Shirika Unguja na Pemba. Kati ya hao, wanachama
116 wamesajiliwa Unguja wakiwemo wanaume 72 na wanawake 44. Pia wanachama 141
kwa Pemba walisajiliwa wakiwemo 52 wanaume na 89 wanawake.
ii.
Idadi ya watumiaji wa maktaba
imefikia 23,326 Unguja na Pemba. Kati yao, 12,864 wakiwemo wanaume 5,172,
wanawake 4,338 na watoto ni 3,354 kwa
Unguja na watu 10,462 wakiwemo wanaume 4,153, wanawake 4,240 na 2,529 ni watoto
kwa Pemba.
Huduma ya Urajisi wa Elimu
53.
Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina
madhumuni ya kuhakikisha sheria, sera na taratibu za Wizara zinafuatwa katika
skuli za Serikali na za binafsi.
Huduma hii pia inatoa leseni kwa walimu na kuzisajili skuli za Serikali na za
binafsi. Shughuli za huduma hii zinatekelezwa na Ofisi ya Mrajisi wa Elimu. Kwa
mwaka wa fedha 2019/20, huduma hii ilipangiwa kutumia jumla ya ruzuku ya TSh.
249,600,000/-. Kati ya fedha hizo TSh. 100,200,000/- ni kwa kazi za kawaida na
TSh. 149,400,000/- zilitengwa kwa matumizi ya mshahara. Hadi kufikia Aprili, 2020, jumla ya TSh. 192,966,950 sawa na asilimia 77
zimepatikana.
54.
Mheshimiwa Spika, Utekelezaji halisi wa
huduma hii ni kama hivi ifuatavyo: -
i)
Mapitio ya rasimu ya Sheria ya Elimu
yanaendelea kufanyiwa kazi. Rasimu hiyo imewasilishwa kwa wadau kwa kupata
maoni yao kabla ya kuwasilishwa katika Kamati ya Uongozi ya Wizara.
ii)
Uhakiki wa wanafunzi ambao walipata
ujauzito kuanzia mwaka 2005 hadi 2015 ulifanyika. Lengo la uhakiki huo ni
kutaka kujua maendelelo ya elimu ya wanafunzi hao. Jumla ya kesi 69 za ujauzito
31 Unguja na 38 Pemba zimefuatiliwa kujua maendeleo ya wanafunzi waliokutwa na
kadhia hiyo baada ya kurejeshwa skuli.
iii)
Jumla ya kesi 43 za ujauzito
zilizopokelewa zikiwemo Unguja 32 na 11Pemba. Kesi hizo zimeripotiwa kwa
Kamanda wa Polisi wa Mikoa husika. Kati ya hizo, kesi 30 zimejadiliwa kwa
mujibu wa Sheria namba 4 (2005) ya Kuwalinda Wari na Mtoto wa Mzazi Mmoja ambayo
imewapa fursa wanafunzi hawa kuendelea na masomo yao. Wanafunzi 30 wamekubali
kuendelea na masomo yao na wanafunzi 8 wamekataa.
iv)
Jumla ya kesi 13 za ndoa (2 Unguja na 11
Pemba) zimeripotiwa. Kwa mujibu wa Sheria ya Elimu Namba 6 ya mwaka 1982
kifungu cha 20(3) wanafunzi hao hawaruhusiwi kuendelea na masomo yao kwa vile
bado wapo katika ngazi ya Elimu ya Lazima.
v)
Jumla ya migogoro 14 ya skuli za binafsi
imeripotiwa. Migogoro hiyo ni pamoja na mishahara ya walimu, kamati za skuli na
uongozi, kufukuzwa kwa wanafunzi katika skuli za binafsi, migogoro ya majengo
pamoja na umiliki wa skuli. Migogoro 10 kati ya hiyo imesikilizwa na kupatiwa
ufumbuzi.
Matokeo ya muda mfupi;
i.
Jumla ya walimu 1,465 wakiwemo wa Cheti
cha Ualimu, Stashahada, Shahada ya Kwanza na ya Pili walipatiwa leseni za
kufundishia za muda wa miaka mitano. Kati ya hao, walimu 736 wamesomea kazi ya
ualimu (LTT), walimu 211 hawajasomea ualimu wamepatiwa leseni za kufundishia za
muda wa mwaka mmoja (LUT) na wametakiwa kujiunga katika vyuo vya Ualimu
vilivyosajiliwa na kutambuliwa na Serikali ili kusomea kazi ya Ualimu na walimu
518 wameongezewa muda wa leseni zao.
ii.
Jumla ya kesi 27 za udhalilishaji
zimesikilizwa, kujadiliwa na kuripotiwa kwa Kamanda wa Polisi wa Mikoa husika.
Kati ya kesi hizo 5 Unguja na kesi 22 Pemba.Wanafunzi wanaohusika na kesi hizo
wamepatiwa ushauri nasaha na wanaendelea na masomo yao.
iii.
Jumla ya skuli 30 za Serikali zimepatiwa
usajili zikiwemo skuli moja ya maandalizi pekee, 14 za maandalizi na msingi,
moja ya msingi na 14 za sekondari kwa Unguja na Pemba.
iv.
Jumla ya skuli 38 za za binafsi
zimewasilisha maombi ya usajili wa muda na zimepewa usajili wao baada ya
kukaguliwa. Kati ya hizo, maandalizi 27, moja ya msingi, tisa za maandalizi na
msingi, skuli mbili za maandalizi msingi na sekondari.
v.
Chuo cha ‘Wete Institute’ huko Pemba kimesajiliwa kwa ajili ya kutoa mafunzo
ya ualimu ngazi ya cheti na stashahada ya elimu ya maandalizi.
Programu ndogo ya
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika Elimu
55.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kuifanya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano itumike katika ngazi
ya utawala, kujifunza na kufundishia, kuimarishahuduma ya mawasiliano, kutunza
usalama wa taarifa na katika maisha ya kila siku. Shughuli za programu hii zinatekelezwa na Idara ya
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika Elimu. Kwa mwaka fedha 2019/20,
programu hii ilipangiwa kutumia jumla ya TSh. 526,393,000/-. Kati ya fedha hizo,
TSh. 278,059,000/- ni kwa kazi za kawaida na TSh. 248,334,000/- zilitengwa kwa
matumizi ya mshahara. Hadi kufikia Aprili 2020, jumla ya TSh. 390,560,250/=
zilipatikana ambazo ni sawa na asilimia 74.
56.
Mheshimiwa Spika, maelezo yautekelezaji
halisi wa programu hii ni kama hivi ifuatavyo: -
i).
Sera ya TEHAMA katika Elimu
imekamilika na kuthibitishwa na Mamlaka husika. Hivi sasa, mpango mkakati wa utekelezaji
wa Sera unaaandaliwa.
ii).
Wizara kwa kushirikiana na
shirika la lisilio la Kiserikali la “Good neighbors” Tanzania imetayarisha
jumla ya vipindi 74 vya televisheni vya kujifunza kwa wepesi masomo ya
Kiingereza, Sayansi na Jiografia na Kiswahili. Vipindi hivi vinaendelea
kurushwa hewani na Shirika la ZBC. Aidha Wizara inaendelea kutayarisha na
kurusha hewani vipindi vya masomo ya Sayansi kwa ngazi ya Msingi kwa Darasa la
Tano na Sita. Lengo la programu hizi ni kuwasaidia walimu na wanafunzi katika
kurahisisha ufundishaji na kupunguza changamoto za mada ngumu katika
kuwafundisha wanafunzi wa ngazi ya msingi.
iii).
Jumla ya taasisi 127 za WEMA
zimefanyiwa upembuzi yakinifu kwa ajili ya kuziunganisha na mkonga wa Taifa.
Miongoni mwa taasisi hizo ni Skuli 83, Vituo vya Walimu 10, Vituo 20 vya
Ubunifu wa Kisayansi na Taasisi 14 za WEMA. Hadi sasa taasisi 13 za WEMA tayari
zimeunganishwa katika mkonga wa Taifa.
iv).
Jumla
ya watendaji 20 wamepatiwa mafunzo. Kati yao 18 walipatiwa mafunzo ya muda
mfupi na wawili walipatiwa mafunzo ya muda mrefu katika fani ya Usimamizi wa
TEHAMA na Mifumo pamoja na TEHAMA na Biashara. Aidha, Wizara iliendesha mafunzo ya TEHAMA kwa walimu wa
TEHAMA ngazi ya msingi ambapo jumla ya walimu 270 walifaidika na mafunzo hayo.
v).
Jumla
ya washiriki 150 kutoka mataifa mbalimbali ndani na nje ya nchi ya Zanzibar
walishiriki katika kongamano la kimataifa juu ya matumizi ya vyombo vya habari
katika uendeshaji wa programu za elimu.Washiriki hao ni kutoka Zanzibar, Tanzania Bara, Kenya, Uganda, Korea ya Kusini
na Rwanda.
vi).
Baada
ya kufungwa kwa skuli zote kutokana na maradhi ya Korona, Wizara imeandaa vipindi vya kufundishia kwa kutumia vyombo
vya habari vya Televisheni, Redio na mitandao ya kijamii.
Matokeo ya muda mfupi;
i)
Jumla
ya walimu 100 kutoka katika skuli 23 za Sekondari Unguja na Pemba wamepatiwa
mafunzo ya TEHAMA na matumizi ya mfumo wa Infoskuli kwa hatua ya majaribio.
Mfumo huu unalenga kurahisisha upatikanaji wa taarifa za maendeleo ya wanafunzi
kitaaluma (continuous assessment) zikiwemo mahudhurio, tathmini na utendaji wa
kazi za walimu. Aidha, mfumo huu unamuwezesha mzazi kupata taarifa hizo za
maendeleo ya mtoto wake wakati wowote na pahali popote alipo nchini kupitia
simu yake ya mkononi.
ii)
Jumla
ya vipindi 74 vya masomo vikiwemo vipindi tisa vya elimu ya maandalizi na 65
vya masomo ya elimu ya msingi. Vipindi hivyo vinaendelea kurushwa kupitia
Shirika la ZBC, Zanzibar Cable na mitandao ya kijamii.
Programu ndogo ya Elimu
Mjumuisho na Stadi za Maisha
57.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
jukumu la kuhakikisha upatikanaji wa elimu kwa watoto wote wakiwemo wenye mahitaji maalum. Programu hii
inatekelezwa na Kitengo cha Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha. Kwa mwaka
2019/20 programu hii ilitengewa jumla ya TSh. 77,610,000/- kwa kazi za kawaida.
Hadi kufikia Aprili, 2020 jumla ya TSh. 44,111,359/= sawa na asilimia 57
zilipatikana. Utekelezaji halisi wa shughuli za programu hii ndogo ni kama
ifuatavyo: -
i)
Matengenezo ya vyumba viwili vya
kufanyia upimaji wa kitaalamu wa wanafunzi wenye mahitaji maalumu “resource
rooms” katika skuli ya Kisiwandui Unguja na skuli ya Michakaini Pemba
umekamilika.
ii)
Rasimu ya Sera ya Elimu Mjumuisho imeshafanyiwa
mapitio na inatarajiwa kuwasilishwa katika vyombo vya ngazi za juu vya
Serikali.
iii)
Wanafunzi 21 wamelipiwa ada ya masomo ya
Stashahada ya Elimu Mjumuisho katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar
(SUZA).Aidha, wanafunzi wawili wasioona (1 mwanamme na 1 mwanamke) wamelipiwa
ada ya masomo katika ngazi ya Stashahada ya Ustawi wa Jamii (Social work)
katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA).
iv)
Mwongozo wa walimu juu uchunguzi wa
awali wa changamoto zinazowakwaza wanafunzi katika kujifunza umeandaliwa.Jumla
ya watendaji 15 (8 Wanaume na 7 wanawake) kutoka taasisi tafauti walishiriki.
v)
Mafunzo ya siku tatu kwa walimu 3,697
(2,512 kutoka Unguja na 1,185 Pemba) kutoka skuli 145 juu ya muongozo wa
uchunguzi wa awali na changamoto zinazowakwaza wanafunzi wakati wa kujifunza
yametolewa.
vi)
Skuli 50 zimejengewa miteremko (ramps),
kati yake 30 Unguja na 20 Pemba. Lengo la ujenzi huu ni kuyafanya mazingira ya
skuli kuwa rafiki na yanayofikika kwa wote.
vii)
Jumla ya walimu 137 kutoka katika skuli
8 za majaribio ya elimu mjumuisho Unguja na Pemba wamepatiwa mafunzo kuhusu
kuimarisha wa ujifunzaji makini darasani (active learning).
viii)
Watendaji watatu (wawili Unguja na mmoja
Pemba) wamepatiwa mafunzo ya matumizi ya mashine ya upimaji wa kiwango cha
usikivu (audiometer) pamoja na urekebishaji wa shime sikio (hearing aids
fixing) kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi viziwi waweze kujifunza kwa ufanisi.
ix)
Jumla ya walimu 1,777 kutoka skuli 145 wamepatiwa
mafunzo ya kuwatambua mapema wanafunzi wenye changamoto mbalimbali
zinazowakwaza katika kujifunza na hivyo kuzipatia ufumbuzi wa mapema.
Programu ndogo ya Michezo
na Utamaduni katika Skuli
58.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kumuandaa mwanafunzi kimwili, kiafya na kiakili katika kujifunza
kwa kupitia michezo. Shughuli za programu hii zinatekelezwa na Idara ya Michezo
na Utamaduni katika elimu. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, programu hii imepangiwa
kutumia jumla ya TSh. 752,271,000/-. Kati ya fedha hizo, TSh. 579,611,000/- ni kwa
kazi za kawaida na TSh. 172,660,000/- ni kwa matumizi ya mishahara. Hadi
kufikia Aprili, 2020, jumla ya TSh. 515,472,291/= sawa na asilimia 69 zilipatikana.
59.
Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa
programu hii ni kama ifuatavyo: -
i).
Jumla ya matamasha matano ya utekelezaji
wa mpango mkakati unaolenga ushajihishaji wa uzalendo, nidhamu na kuwajenga
wanafunzi katika maadili mema pamoja na kuwafahamisha historia ya nchi ‘Nchi
yetu ni Urithi wetu’ yamefanyika katika kila mkoa.
ii).
Shughuli za ufuatiliaji wa utekelezaji
wa mpango wa “Sports 55” zimefanyika katika kila Wilaya na kwa kila skuli
husika. Ufuatiliaji huu wa kina umelenga kuhakikisha kwamba vifaa vilivyotolewa
vinatunzwa na kutumika vizuri na walimu waliopatiwa mafunzo wanawajibika
ipasavyo kutimiza lengo la mpango huu.
iii).
Wanafunzi 410 wa skuli za maandalizi,
msingi na sekondari Unguja na Pemba wameshiriki katika Tamasha la Utamaduni wa
Mzanzibari lililoratibiwa na Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
iv).
Jumla ya wanafunzi 187 kutoka skuli 33
za msingi Unguja na Pemba wameshiriki katika mashindano maalumu ya Sanaa ya
uigizaji na uchoraji yaliyoandaliwa na Baraza la Sanaa, Sensa ya Filamu na
Utamaduni Zanzibar (BASFU) yenye lengo la kuibua na kuendeleza vipaji vya Sanaa
hizo.
v).
Jumla ya walimu 210 wamepatiwa mafunzo
ya uendeshaji na usimamizi wa michezo ya riadha kwa watoto (Kids Atheletics). Mafunzo haya
yametolewa kwa mashirikiano na Chama cha Riadha Tanzania na yamelenga
kuwashajihisha walimu kutumia mazingira na vifaa vya kienyeji kufundishia
riadha.
vi).
Mashindano ya michezo na sanaa ya
Tamasha la Elimu bila Malipo kuanzia ngazi ya skuli, Wilaya, Mkoa hadi Taifa
yamefanyika kwa ufanisi na kuongeza hamasa na ushiriki wa wanafunzi katika
michezo pamoja na kuibua vipaji vipya vya michezo na sanaa.
vii).
Jumla ya timu tano za michezo za mpira
wa miguu, wavu, meza, mikono na riadha zimeshiriki mashindano ya michezo ya
skuli za sekondari za Afrika Mashariki yaliofanyika mjini Arusha. Mashindano
haya ni sehemu muhimu ya mpango wa kuendeleza vipaji vilivyotokana na
mashindano ya ndani.
PROGRAMU YA SITA: UTAWALA
NA UONGOZI
60.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina lengo
la kuhakikisha nyenzo zilizo bora zinapatikana na zinatumika ipasavyo kwa kuimarisha
utoaji na upatikanaji wa elimu nchini.
Programu hii ina programu ndogo tatu; Programu ya Uongozi kiujumla, Programu ya
Uratibu wa Shughuli za Mipango, Sera na Utafiti na Programu ya Uratibu wa
Shughuli za Elimu Pemba. Kwa mwaka wa fedha 2019/20 Programu hii ilipangiwa
jumla ya TSh. 14,599,201,000/-. Kati ya fedha hizo TSh. 7,573,176,000/- ni kwa
kazi za kawaida, TSh. 5,526,025,000/- kwa matumizi ya mshahara na TSh.
1,500,000,000/- kwa matumizi ya kazi za maendeleo kutoka Serikalini.
Utekelezaji halisi wa programu ya Utawala na Uongozi ni kama ifuatavyo: -
61.
Mheshimiwa Spika, programu hii ina
madhumuni ya kutoa ufanisi wa Uongozi na utawala wa rasilimali za Wizara.
Shughuli za programu hii ndogo zinatekelezwa na Idara ya Utumishi na
Uendeshaji. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, programu hii ilipangiwa jumla ya TSh.
6,091,971,000/-, kati ya fedha hizo TSh. 3,631,832,000/- kwa matumizi ya
kawaida na TSh. 2,460,139,000/- ni kwa matumizi ya mshahara. Hadi kufikia
Aprili, 2020, jumla ya TSh. 3,556,110,296/= zilipatikana sawa na asilimia 58. Utekelezaji wa kazi za programu hii ni kama ifuatavyo: -
i)
Jumla ya walimu 967 (638 Unguja
na 329 Pemba) na 65 nje ya kada ya ualimu waliajiriwa baada ya kupata kibali
cha uajiri kutoka Tume ya Utumishi Serikalini. Kati yao, kwa upande wa Unguja
walimu 83 ni wa Shahada ya Kwanza Sayansi, 450 Shahada ya kwanza Sanaa, 104
Stashahada ya Sayansi, 1 Stashahada ya Sanaa. Kwa upande wa Pemba, waliajiriwa
walimu 48 wa Shahada ya Kwanza Sayansi, 193 Shahada ya Kwanza Sanaa, 84
Stashahada Sayansi na 4 ni walimu wa Cheti.
ii)
Jumla ya wafanyakazi 463 Unguja
na 118 Pemba waliopewa likizo walilipwa posho la likizo la jumla ya TSh.
58,100,000.
iii)
Jumla ya wafanyakazi 474 (141
Unguja na 333 Pemba) walipatiwa fursa ya kujiunga na masomo katika vyuo mbali
mbali vya ndani na nje ya nchi katika ngazi tofauti baada ya kukamilisha
masharti ya kiutumishi na ya vyuo. Kati yao, wafanyakazi 23 wamepatiwa mafunzo
ya muda mfupi na 118 ni wa mafunzo ya muda mrefu.
iv)
Jumla ya walimu 1,231
walipatiwa huduma ya likizo, walimu 84 walistaafu, 6 waliacha kazi na walimu 10 walifariki
dunia. Mwenyezi Mungu awalaze mahali pema peponi Amin.
v)
Jumla ya wafanyakazi 21
walistaafu kazi kwa mujibu wa sheria. Wafanyakazi watano walifariki dunia,
Mwenyezi Mungu awalaze mahali pema peponi (Amin). Aidha mfanyakazi mmoja alipewa
uhamisho kwenda kuendelea na kazi katika Wizara ya Fedha na Mipango na
mfanyakazi mmoja amechukua likizo bila ya malipo.
vi)
Jumla ya wafanyakazi 350 Unguja
na 259 Pemba wamedhaminiwa kupata mikopo ya Benki na Saccos mbalimbali nchini.
Wafanyakazi hao wamepata mikopo ya fedha taslim, vifaa vya ujenzi, vipando na
vifaa vya matumizi ya nyumbani. Mikopo iliyotolewa ina thamani ya
TSh.1,227,284,338/- kwa Unguja na TSh 1,363,264,310/- kwa Pemba.
Matokeo
ya muda mfupi;
Hadi kufikia Aprili 2020, Wizara
ya Elimu na Mafunzo ya Amali ilikuwa na jumla ya wafanyakazi 7,758. Kati yao,
3,877 ni wanawake na 3,881 wanaume. Wafanyakazi 5,967 wapo Unguja (3,193wanawake
na 2,774 wanaume) na kwa upande wa Pemba wapo wafanyakazi 1,791 (wanawake 684
na wanaume ni 1,107). Kati ya wafanyakazi wote hawa 5,704 ni wa kada ya ualimu
na 1,664 ni wafanyakazi wasiokuwa wa kada ya ualimu.
Programu
ndogo ya Uratibu wa Shughuli za Mipango, Sera na Utafiti
62.
Mheshimiwa Spika, programu hii ina
madhumuni ya kufanikisha na kuratibu Mipango, Sera na Utafiti katika Wizara.
Programu hii ndogo inatekelezwa na Idara ya Mipango, Sera na Utafiti. Kwa mwaka
2019/20 programu hii ilipangiwa kutumia jumla ya TSh. 5,233,552,000/-. Kati ya
fedha hizo, TSh. 3,238,099,000/- ni kwa kazi za kawaida, TSh. 495,453,000/- kwa
matumizi ya mshahara na TSh. 1,500,000,000/- ni kwa kazi za maendeleo. Hadi
kufikia Aprili, 2020, jumla ya TSh. 2,367,449,619/= za kazi za kawaida
zilipatikana ambazo ni sawa na asilimia 45.2.
63.
Mheshimiwa Spika, utekelezaji halisi wa
programu hii ni kama hivi ifuatavyo: -
i.
Rasimu ya mapitio ya Sera ya Elimu ya
mwaka 2006 imewasilishwa kwa wadau 1,200 kwa ajili ya kutoa michango yao ya
kuiimarisha. Washiriki katika mijadala ilijumuisha walimu, wazee, maafisa
kutoka taasisi za serikali na binafsi pamoja na viongozi mbalimbali wa Wilaya
na Mikoa yote ya Unguja na Pemba. Rasimu hiyo itawasilishwa kwenye vikao vya
juu vya Serikali kwa ushauri zaidi.
ii.
Ufuatiliaji wa utekelezaji wa Mpango
Mkuu wa Elimu umeendelea kwa kila robo mwaka na ripoti za utekelezaji
zimetayarishwa. Aidha, Wizara imeendelea kufuatilia na kusimamia utekelezaji wa
miradi ya elimu iliyokamilika na inayoendelea. Miongoni mwa Miradi hiyo ni
ujenzi wa Skuli Tisa za Sekondari (ZATEP), Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya
Sekondari (ZISP), Mradi wa Uimarishaji
wa Elimu ya Maandalizi na Utekelezaji wa Mradi wa Elimu Mbadala na Amali (ALSD
II). Miradi hiyo inatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa
Maendeleo wa ndani na nje ya nchi.
iii.
Mkutano mkuu wa tatu wa mwaka wa tathmini
ya elimu (3rd AJESR) uliowashirikisha wadau 150 wa elimu wa ndani na
nje ya Zanzibar wakiwemo wahisani, wazee, wanafunzi, kamati za skuli, taasisi
za serikali na za watu binafsi umefanyika. Mkutano huo ulifanyika kwa muda wa
siku tatu kuanzia tarehe 9 - 11/03/2020 katika ukumbi wa Madinat Albahr.
iv.
Matokeo ya utafiti wa kutathmini
upatikanaji, utumiaji na usimamizi wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa
skuli za sekondari Zanzibar yamewasilishwa kwa wadau wa elimu katika Mkoa wa
Mjini Magharibi. Uwasilishaji pia utaendelea katika mikoa mingine.
v.
Zoezi la utafiti wa SEACMEQ V limeanza
kwa hatua ya kutayarisha na kuhariri dodoso za kukusanyia taarifa. Hatua
inayofuata ni kamati ya utafiti ya SEACMEQ kupitisha maswali ya utafiti mkuu na
kuanza zoezi la utafiti. Kikao cha pamoja cha nchi wanachama kilichopangwa
kufanyika mwanzoni mwa mwezi wa Aprili 2020 nchini Afrika ya Kusini
kiliahirishwa kutokana na ugonjwa wa virusi vya Korona (COVID 19).
vi.
Mfumo wa kielektroniki wa kukusanya
taarifa za skuli unaendelea kutumika kwa majaribio. Mfumo huu umesaidia kuinua
usimamizi wa skuli zetu katika utoaji na upatikanaji wa elimu. Aidha, Wizara
imewajengea uwezo wataalamu wa ndani ili waweze kuusimamia mfumo huo. Kwa sasa
kazi inayoendelea ni kuhamisha mfumo kutoka katika SERVER za kampuni ya FHI 360
kwenda katika SERVER za WEMA.
vii.
Wizara imeandaa mpango wa kukabiliana na
athari za ugonjwa wa virusi vya Korona (COVID 19) katika elimu. Mpango huo una
lengo la kuhakikisha mawasiliano ya karibu kati ya uongozi, walimu na wanafunzi
katika kuhakikisha watoto wanaendelea kusoma hasa kipindi hiki ambacho watoto
wapo majumbani. Aidha, mpango umezingatia pia kuendeleza ubunifu na mikakati
mbalimbali iliyoibuliwa katika kujifunza na kufundisha hata baada ya COVID 19,
hasa katika matumizi ya Teknolojia katika elimu, uimarishaji wa miundombinu na
uhamasishaji wa jamii katika kusaidia elimu ya mtoto.
Programu ndogo ya Uratibu
shughuli za elimu Pemba
64.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ndogo ina
madhumuni ya kuratibu na kusimamia shughuli zote za elimu kwa upande wa Pemba.
Msimamizi Mkuu wa shughuli za programu hii ni Afisa Mdhamini wa Wizara yangu
kupitia katika Divisheni ya Idara ya Uendeshaji na Utumishi Pemba. Programu hii ndogo ilipangiwa jumla
ya TSh. 3,273,678,000/-, kati ya fedha hizo TSh. 703,245,000/-kwa kazi za
kawaida na TSh. 2,570,433,000/- ni kwa matumizi ya mshahara. Hadi kufikia
Aprili, 2020, jumla ya TSh. 2,799,615,809/= zilipatikana sawa na asilimia 86.
65.
Mheshimiwa Spika, Fedha za programu hii
zilitumika katika kusimamia na kufuatilia shughuli na programu za elimu
Pemba.
MAPATO
66.
Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea
kukusanya mapato kupitia usajili wa Skuli za binafsi na malipo ya leseni za
walimu. Hadi kufikia Aprili 2020, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali imekusanya
jumla ya TSh. 104,063,190/= kati ya TSh. 195,655,000/= zilizopangwa kukusanywa.
Hii ni sawa ya asilimia 53 ya makadirio. Kati ya Mapato yaliyokusanywa TSh.
58,596,850/= zinatokana na malipo ya leseni za walimu na TSh. 34,569,560/= ni
za usajili wa skuli za binafsi.
MPANGO WA UTEKELEZAJI KWA
MWAKA 2020/2021 KWA MFUMO WA PROGRAMU
67.
Mheshimiwa Spika, baada ya taarifa hiyo
ya utekelezaji wa bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa mwaka wa
fedha 2019/20 naomba sasa niwasilishe vipaumbele vya Wizara yangu na kisha
makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2020/2021.
Vipaumbele vya Wizara
68.
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha
2020/2021,vipaumbele vya Sekta ya Elimu vitakuwa kama ifuatavyo: -
i.
Kuendelea kuzipatia skuli za sekondari
fedha za ruzuku kufidia michango ya wazee kwa kuwapatia wanafunzi mabuku ya
kuandikia na vifaa vyengine vya kusomeshea na kujifunzia vikiwemo chaki, vitabu
vya kiada na ziada na vifaa vya maabara.
ii.
Kuimarisha miundombinu na mazingira ya
kufundishia na kujifunzia kwa kukamilisha ujenzi wa madarasa 50 yaliyoanzishwa kwa
nguvu za wananchi, kuanza ujenzi wa skuli tatu mpya katika maeneo ya Mfenesini,
Gamba kwa Unguja na Kifundi kwa Pemba, kujenga maabara katika skuli 11 za
Sekondari pamoja na kukamilisha ujenzi wa skuli ya sekondari ya Kibuteni.
iii.
Kukamilisha ukarabati wa Skuli ya
Sekondari ya Lumumba na kuanza ukarabati mkubwa wa Skuli za sekondari za
Benbella, Hailesselasie na Pajemtule kwa Unguja na Skuli ya Sekondari ya Chwaka
Tumbe Pemba
iv.
Kufanya ukarabati mdogo katika Skuli 20
za Sekondari Unguja na Pemba.
v.
Kuimarisha mapambano dhidi ya ugonjwa wa
virusi vya Korona (COVID 19) na kuwawezesha wanafunzi wa ngazi zote kuendelea
kupata elimu kupitia Teknolojia.
vi.
Kuendelea na matumizi ya TEHAMA katika
kuinua ubora wa elimu.
vii.
Kuzipatia fedha za zawadi skuli za
sekondari na msingi zitakazoongeza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi katika
katika masomo ya Sayansi, Hisabati na Kiingereza.
viii.
Kufanya utafiti wa tathmini ya ubora wa
elimu ya msingi (SEACMEQ V).
ix.
Kuendelea kutoa mikopo kwa wanafunzi wa
elimu ya juu na kukusanya marejesho ya mikopo kutoka kwa wahitimu wa ngazi
hiyo.
x.
Kuwajengea uwezo walimu wanaofundisha
masomo ya Sayansi, Hisabati na Kiingereza.
xi.
Kuandaa Mitaala ya Elimu ya Maandalizi
na Msingi, kuandika mihitasari ya masomo, kuandika na kuchapisha vitabu pamoja
na miongozo ya walimu kwa ngazi ya elimu ya maandalizi.
xii.
Kuwawezesha watoto wenye mahitaji
maalumu kupata elimu kwa kuimarisha mazingira ya skuli kujali mahitaji ya
watoto kuendana na hali zao.
xiii.
Kutoa elimu ya ushauri nasaha juu ya
udhalilishaji (ndoa za mapema na mimba za utotoni). Kuratibu mapambano dhidi ya
liwati, dawa ya kulevya, UKIMWI na COVID 19 kwa kushirikiana na taasisi husika.
xiv.
Kuimarisha huduma za dahalia kwa
kuzipatia usafiri (basi moja) na chakula kwa wanafunzi 2,000.
xv.
Kuandaa mkutano mkuu wa nne wa pamoja na
wadau wa elimu kutathmini mafanikio ya Sekta ya Elimu Zanzibar (4th AJESR).
xvi.
Kuimarisha programu za masomo katika
Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar, Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia
na Mamlaka ya Mafunzo ya Amali.
69.
MheshimiwaSpika, Naomba sasa,
kuwasilisha mpango wa maendeleo ya elimu kwa mwaka wa fedha wa 2020/2021 kwa
mfumo wa programu kama hivi ifuatavyo: -
70.
Mheshimiwa Spika, Kwa mwaka wa fedha wa
2020/2021 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali itaendelea kutekeleza malengo
yake yaliyozingatia Dira 2020, MKUZA III, Sera ya Elimu, Mpango Mkuu wa Elimu
(2017 – 2021), vipaumbele vya Wizara kwa mwaka 2020/21 pamoja na mikakati
mengine ya Kitaifa na Kimataifa yenye lengo la kuimarisha upatikanaji wa huduma
ya elimu nchini. Wizara pia, itaendelea kushirikiana na sekta nyengine
zinazotoa huduma za jamii na kuimarisha uchumi ikiwemo Wizara ya Afya, Wizara
ya Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira, Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Maendeleo ya
Wazee, Wanawake na Watoto, Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa,
Serikali za Mitaa na Idara Maalumu, Washirika wa Maendeleo na Mashirika yasiyo
ya kiserikali na wananchi.
71.
Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha
wa 2020/2021, Wizara yangu itatekeleza miradi mitano ya maendeleo kupitia
programu zake sita kama ilivyokuwa mwaka 2019/2020. Programu ya Maandalizi na
Msingi itatekelezwa kwa pamoja na Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za
Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ kupitia mfumo wa Ugatuzi.
72.
Mheshimiwa Spika, Jumla ya TSh.
138,145,584,000/= zimetengwa. Kati ya hizo TSh. 123,183,500,000/= ni za SMZ,
TShs. 14,962,084,000/= ni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo na TSh.
4,500,000,000/= ni mchango wa SMZ kwa miradi ya maendeleo. Fedha za Washirika
wa Maendeleo zinajumuisha TSh. 6,327,084,000/= ni ruzuku kutoka GPE, Table for
Two (TfT), Shirika la “Good Neighbors” la Korea na “Milele Zanzibar Foundation”
na TSh. 8,635,000,000/= ni mkopo kutoka Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya
Afrika (AfDB) na Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA). Jadweli Nam.
49 linatoa ufafanuzi zaidi.
Mheshimiwa Spika, Miradi mitano itakayotekelezwa na Wizara ni hii ifuatavyo: -
i).
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya
Maandalizi
ii).
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Msingi
iii).
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Lazima
iv).
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu Mbadala na
Amali.
v).
Mradi wa Uimarishaji wa Miundombinu
katika elimu
MAELEZO YA
PROGRAMU ZA ELIMU
73.
Mheshimiwa Spika, yafuatayo ni maelezo
ya programu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali yanayohusisha Madhumuni,
Matokeo ya muda mfupi, Viashiria na Shabaha za utekelezaji kwa kila programu.
PROGRAMU YA
KWANZA:
ELIMU YA
MAANDALIZI NA MSINGI
74.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kumuandaa mtoto kimwili na kiakili kwa ajili ya kupata elimu ya
maandalizi na msingi na kumuwezesha mwanafunzi kujua kusoma, kuandika na
kuhesabu na kumtayarisha kwa elimu ya sekondari.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Kumtayarisha mtoto kwa ajili ya
elimu ya msingi.
·
Kutoa elimu ya msingi
Viashiria vya matokeo;
·
Uwiano wa uandikishaji wa
wanafunzi katika ngazi ya maandalizi na msingi.
·
Uwiano wa idadi ya walimu kwa
wanafunzi.
·
Uwiano wa wanafunzi kwa darasa.
·
Uwiano wa ufaulu wa wanafunzi.
Shabaha za utekelezaji;
·
Kuongeza kiwango cha uandikishaji
wanafunzi wa maandalizi kutoka asilimia 86.0 kwa mwaka 2020 hadi kufikia
asilimia 88 ifikapo mwaka 2021.
·
Kuongeza kiwango halisi cha
uandikishaji wanafunzi wa msingi kutoka asilimia 86 kwa mwaka 2019 hadi kufikia
asilimia 90 ifikapo mwaka 2021.
PROGRAMU YA PILI: ELIMU YA SEKONDARI
75.
Mheshimiwa Spika, Programu ya Elimu ya
Sekondari madhumuni yake makubwa ni kumtayarisha mwanafunzi aweze kuendelea na
masomo katika ngazi za juu zaidi.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Kutoa Elimu ya Sekondari.
Viashiria vya matokeo;
·
Uwiano wa wanafunzi wanaomaliza
elimu ya lazima,
·
Uwiano halisi wa uandikishaji
wa wanafunzi katika ngazi ya kidato cha nne na cha sita,
·
Uwiano wa idadi ya walimu kwa
nyumba za wafanyakazi katika maeneo yasiyofikika kirahisi
·
Uwiano wa wanafunzi kwa
madarasa.
Shabaha za utekelezaji;
·
Kuongeza kiwango halisi cha uandikishaji
wanafunzi wa sekondari ya awali (Kidato cha 1 – 4) kutoka asilimia 79.5 mwaka
2020 hadi kufikia asilimia 83 ifikapo mwaka 2021.
·
Kiwango cha ufaulu cha mpito kutoka kidato cha pili kwenda cha tatu
kuongezeka kutoka asilimia 76.8 mwaka 2019 hadi kufikia asilimia 78.8 ifikapo
mwaka 2020.
PROGRAMU YA TATU: ELIMU YA
JUU
76.
Mheshimiwa Spika, programu hii madhumuni
yake ni kutoa elimu itakayomuwezesha muhitimu kujiajiri au kuajiriwa. Programu hii ina programu ndogo moja
na maeneo madogo manne ambayo ni: -
Programu ndogo ya Mafunzo ya Ualimu
77.
Mheshimiwa Spika, programu hii ina
madhumuni ya kuwawezesha walimu kuwa wabunifu, wataalamu na wenye uwezo wa
kuongoza ili kukuza ubora wa elimu.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Elimu ya Diploma ya Ualimu
kutolewa
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya wanafunzi wote
walioandikishwa vyuo vya ualimu.
Shabaha za Utekelezaji;
·
Kuongeza kiwango cha asilimia
ya walimu wenye sifa kutoka 99.2 mwaka 2018 hadi kufikia asilimia 99.6 mwaka
2020.
Huduma ya Elimu ya Juu, Ushauri na Utafiti
78.
Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina
madhumuni ya kumtayarisha mwanafunzi kuingia katika fani za kitaalamu na ajira.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Kiwango cha elimu ya
Stashahada, Shahada ya kwanza, Shahada ya pili na Shahada ya tatu kutolewa.
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya wanafunzi wanaomaliza
ngazi ya Astashahada na Stashahada.
·
Idadi ya wanafunzi wanaomaliza
ngazi ya Shahada ya kwanza ya Uzamili na Uzamivu.
·
Idadi ya tafiti zinazofanywa.
Shabaha za Utekelezaji;
·
Kuongeza idadi ya wanafunzi wa
Chuo Kikuu kutoka 7,303 mwaka 2019 hadi kufikia 8,000 mwaka 2021.
Huduma ya Elimu ya Sayansi
na Teknolojia
79.
Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina
madhumuni ya kuimarisha elimu ya sayansi na teknolojia.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Kuimarisha ufundishaji na
kujifunza Sayansi, Hisabati na Teknolojia
·
Elimu ya Ufundi kuimarishwa.
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya wanafunzi wahitimu
katika Taasisi,
·
Uwiyano wa wanafunzi kwa
madarasa.
Huduma ya Mikopo ya Elimu ya Juu
80.
Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina
madhumuni ya kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya Juu.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Mikopo kwa wanafunzi wa elimu
ya juu kutolewa.
·
Fedha zilizokopeshwa kwa
wanafunzi kurejeshwa.
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya wanafunzi wanaopokea
mikopo
·
Idadi ya wanafunzi wanaorudisha
mikopo.
Shabaha za Utekelezaji;
·
Kuongeza utoaji wa mikopo kwa
wanafunzi kutoka asilimia 36 ya waombaji mwaka 2018/19 hadi kufikia asilimia 45
ifikapo mwaka 2020/21.
·
Kuongeza makusanyo ya marejesho
ya mikopo kutoka TSh. 1,970,000,000/=
ya mwaka 2019/20 na kufikia TSh. 3,000,000,000/= mwaka 2020/21.
Huduma ya Uratibu wa Elimu ya Juu
81.
Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina
madhumuni ya usimamizi na tathmini ya elimu ya juu.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Tathmini katika vyuo vinavyotoa
elimu ya juu kufanyika.
·
Wahitimu waliomaliza masomo ya
elimu ya juu kuratibiwa.
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya wanafunzi wanaoendelea
na masomo ya elimu ya juu kijinsia.
·
Idadi ya wahitimu wa elimu ya
juu kijinsia.
PROGRAMU YA NNE: ELIMU MBADALA NA MAFUNZO YA AMALI
82.
Mheshimiwa Spika, Programu hii madhumuni
yake ni kutoa elimu ya mafunzo ya amali kwa mwanafuzi kulingana na mahitaji ya
soko la ajira. Programu hii ina programu ndogo ndogo mbili kama ifuatavyo;
Programu ndogo ya Mafunzo ya Amali
83.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kutoa elimu itakayowawezesha vijana kujiajiri ili kujikwamua na
umasikini.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Mafunzo ya Amali na ufundi
kutolewa.
Viashiria vya matokeo;
·
Ukosefu wa ajira kwa vijana
kupungua
·
Idadi ya wanafunzi wanaomaliza
mafunzo ya amali kuongezeka.
Programu ndogo ya Elimu Mbadala na Watu Wazima
84.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kupunguza kiwango cha kutojua kusoma, kuandika na kuhesabu miongoni
mwa wanajamii.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Elimu mbadala na ya watu wazima
kutolewa.
Viashiria vya matokeo;
·
Kiwango cha kujua kusoma,
kuandika na kuhesabu kwa watu wazima,
·
Idadi ya watu wazima
wanaoshiriki katika madarasa ya wanakisomo,
·
Idadi ya vijana waliojiunga na
madarasa na vituo vya elimu mbadala,
·
Idadi ya wanakisomo
walioanzisha vikundi vya ushirika
Shabaha za Utekelezaji;
·
Kuongeza kiwango cha kujua
kusoma na kuandika kutoka asilimia 84.2 mwaka 2012 hadi kufikia asilimia 90
ifikapo mwaka 2022.
PROGRAMU YA TANO: UBORA WA ELIMU
85.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kutoa elimu bora kwa ngazi zote za elimu. Ina programu ndogo tatu
na maeneo matano ya kutoa huduma kama yafuatayo;
Huduma ya Mitaala na Vifaa vya Kufundishia
86.
Mheshimiwa Spika, Huduma hii ina
madhumuni ya kutayarisha mitaala ya elimu na vifaa vya kufundishia na
kujifunzia kwa ngazi za elimu ya maandalizi, msingi, sekondari na mafunzo ya
Ualimu.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Mitaala ya Elimu na vifaa vya
kufundishia na kujifunzia kwa ngazi zote kutayarishwa.
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya Mitaala na vifaa vya
kufundishia na kujifunzia vilivyotayarishwa na kusambazwa katika skuli.
Huduma ya Upimaji na Tathmini ya Elimu
87.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kupima na kutathmini utekelezaji wa utoaji wa elimu.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Malengo ya elimu kupimwa.
Viashiria vya matokeo;
·
Asilimia ya wanafunzi na
kiwango cha mpito katika ngazi za darasa la nne, darasa la sita, kidato cha
pili, kidato cha nne na cha sita.
·
Asilimia ya ufaulu wa walimu na
wanafunzi
Huduma ya Ukaguzi wa Elimu
88.
Mheshimiwa Spika, utoaji wa huduma hii
una madhumuni ya kusimamia utoaji wa elimu unaofuata mtaala na kuhakikisha
ufanisi na ubora wa elimu inayotolewa.
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya skuli zilizokaguliwa
·
Idadi ya ripoti za ukaguzi
zilizowasilishwa
Huduma za Maktaba
89.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kutoa fursa ya kutumia vitabu na vyanzo vyengine vya taaluma kwa
wananchi.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Kutoa nafasi kwa wanafunzi na
watu wengine ya kupata taarifa mbalimbali kupitia maktaba.
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya watu wanaotumia
maktaba
·
Idadi ya vitabu, CDs, magazeti
na majarida yaliyopo katika maktaba.
·
Idadi ya skuli zenye maktaba
kamili.
90.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kuhakikisha Sheria, Sera na taratibu za Wizara zinafuatwa. Pia
kutoa leseni kwa walimu na kusajili skuli za Serikali na za binafsi.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Skuli za Serikali na binafsi
zenye viwango bora kusajiliwa
·
Leseni za walimu kutolewa.
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya leseni za walimu
zilizotolewa.
·
Idadi ya skuli zilizosajiliwa.
·
Sheria ya Elimu iliyopitiwa na
kurekebishwa.
·
Idadi ya wanafunzi waliopata
ujauzito na kurejea masomoni baada ya kujifungua kuratibiwa.
·
Idadi ya kesi za ndoa kwa
wanafunzi zilizofuatiliwa na kutolewa uamuzi.
Programu ndogo ya Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha
91.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kutoa elimu kwa wote wakiwemo watoto wenye mahitaji maalum.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Vifaa vya kufundishia na
kujifunzia kwa watoto wenye mahitaji maalum kutolewa
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya wanafunzi na walimu
katika Elimu Mjumuisho.
Programu ndogo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
92.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kuifanya teknolojia ya habari na mawasiliano itumike katika
kujifunza, kufundisha, ngazi ya utawala na katika maisha ya kila siku.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Walimu na wanafunzi wanapatiwa
mafunzo juu ya matumizi ya Teknolojia ya kisasa.
Viashiria vya utekelezaji;
·
Idadi ya walimu wenye ujuzi wa
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,
·
Idadi ya vifaa vya Teknolojia
ya Habari na mawasiliano katika skuli na Wizara
·
Idadi ya Taasisi za elimu
zilizounganishwa na mkonga wa Taifa.
·
Mafunzo ya matumizi ya kompyuta
kutolewa kuanzia katika skuli za msingi.
Programu ndogo ya Michezo na Utamaduni katika Skuli
93.
Mheshimiwa Spika, Programu hii ina
madhumuni ya kumuandaa mwanafunzi kimwili, kiafya na kiakili katika kujifunza
kwa kupitia michezo.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Kuinua taaluma ya michezo
katika skuli.
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya walimu wenye taaluma
ya michezo
·
Idadi ya skuli zenye viwanja
vya michezo
·
Idadi ya skuli zenye vifaa vya
michezo
·
Idadi ya wanafunzi wenye vipaji
vya michezo
PROGRAMU YA SITA: UTAWALA NA UONGOZI
94.
Mheshimiwa Spika, Programu hii madhumuni
yake makubwa ni kuhakikisha nyenzo zilizo bora zinapatikana na zinatumika kwa
kuimarisha utoaji wa elimu. Programu
hii ina programu ndogo tatu kama zifuatavyo: -
Programu ndogo ya Uongozi kiujumla
95.
Mheshimiwa Spika, programu hii ina
madhumuni ya kuratibu usimamizi na ufanisi wa Uongozi na Utawala wa rasilimali
za Wizara.
Matokeo ya muda mfupi;
·
Kupatikana kwa ufanisi katika utoaji
wa huduma, uongozi na utawala wa rasilimali za Wizara.
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi ya wafanyakazi
wanaoajiriwa na kustaafu,
·
Mafunzo yanayotolewa kwa
wafanyakazi.
Shabaha za Utekelezaji;
·
Kuongeza ufanisi katika kutoa
huduma kwa wafanyakazi na upatikanaji wa nyenzo za kufanyia kazi.
Programu
ndogo ya Uratibu wa Shughuli za Mipango, Sera na Utafiti
96.
Mheshimiwa Spika, programu hii ina
madhumuni ya kufanikisha na kuratibu Mipango, Sera na Utafiti katika Wizara.
Matokeo ya muda mfupi;
Kupatikana kwa sera na mipango ya
Wizara, kufanya utafiti na kufanya ufuatiliaji na tathmini.
Viashiria vya matokeo;
·
Idadi za tafiti zilizofanywa
·
Ripoti za utekelezaji na ripoti
za tathmini.
Programu ndogo ya kuratibu
shughuli za Elimu Pemba
97.
Mheshimiwa Spika, programu hii ina
madhumuni ya kuratibu na kusimamia shughuli zote za elimu kwa upande wa Pemba.
Matokeo ya muda mfupi na shabaha za utekelezaji zinazotumika ni kama zile
zilizoelezwa katika programu za Uongozi kiujumla na Uratibu wa shughuli za
Mipango, Sera na Utafiti.
98.
Mheshimiwa Spika, msimamizi wa shughuli
za programu hii ni Afisa Mdhamini wa Wizara yangu kupitia katika Divisheni ya
Idara ya Uendeshaji na Utumishi Pemba.
MGAWANYO WA FEDHA KWA
PROGRAMU
99.
Mheshimiwa Spika, Sehemu hii inaonesha
mgawanyo wa fedha kwa Programu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali yenye
kuzingatia gharama za Idara/ Vitengo/Taasisi zilizomo katika programu husika.
PROGRAMU YA KWANZA:
ELIMU YA MAANDALIZI NA
MSINGI
Idara Husika: Idara ya Elimu ya
Maandalizi na Msingi
Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 5,135,232,000/= zimepangwa kwa ajili ya kufanikisha
programu hii. Kati ya fedha hizo, TSh. 1,479,669,000/= ni kwa kazi za kawaida
na TSh. 3,655,563,000/= kwa kazi za maendeleo.
PROGRAMU YA PILI: ELIMU YA SEKONDARI
Idara Husika: Idara ya Elimu ya
Sekondari
Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 66,478,525,000/= zimepangwa kwa ajili ya kufanikisha
programu hii. Kati ya hizo TSh. 53,062,304,000/= kwa kazi za kawaida na TSh.
13,416,221,000/= kwa kazi za maendeleo.
PROGRAMU YA TATU: ELIMU YA JUU
Taasisi Husika: Idara ya
Mafunzo ya Ualimu, Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar, Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia, Bodi ya Mikopo ya Elimu
ya Juu na Kitengo cha Uratibu wa Elimu wa Juu.
Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 30,480,366,000/= zimepangwa kwa kufanikisha programu
hii kwa kazi za kawaida.
PROGRAMU YA NNE: ELIMU
MBADALA NA MAFUNZO YA AMALI
Idara Husika: Mamlaka ya Mafunzo ya Amali pamoja na Idara ya Elimu Mbadala na Watu
Wazima.
Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 9,403,674,000/= zimepangwa kwa ajili ya kufanikisha
programu hii kwa kazi za kawaida.
PROGRAMU YA TANO: UBORA WA ELIMU
Idara Husika: Taasisi ya Elimu ya Zanzibar, Baraza la Mitihani la Zanzibar, Ofisi
ya Mkaguzi Mkuu wa Elimu, Kitengo cha Elimu Mjumuisho na Stadi za Maisha,
Shirika la Huduma za Maktaba Zanzibar, Idara ya Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano Katika Elimu, Ofisi ya Mrajisi wa Elimu, Idara ya Michezo na
Utamaduni Katika Skuli.
Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 10,201,204,000/= zimepangwa kwa ajili ya kufanikisha
programu hii kwa kazi za kawaida.
PROGRAMU YA SITA: UONGOZI NA UTAWALA
Idara Husika: Idara ya Utumishi na Uendeshaji, Idara ya Mipango, Sera na Utafiti
na Ofisi ya Elimu Pemba.
Gharama za Programu: Jumla ya TSh. 16,446,583,000/= zimepangwa kwa ajili ya kufanikisha
programu hii. Kati ya hizo, TSh. 14,056,283,000ni kwa kazi za kawaida na TSh.
2,390,300,000/= kwa kazi za maendeleo.
100.
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2020/21
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali imekadiriwa kukusanya mapato ya jumla ya
TSh. 215,700,000/=. Mapato hayo yatatokana na usajili wa skuli na leseni za
kufundishia walimu.
JUMLA YA GHARAMA ZA WIZARA
YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI
101.
Mheshimiwa Spika, gharama kwa programu
zote sita za Wizara ni TSh. 138,145,584,000/= sawa na bajeti yote ya Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Amali inayotumia programu iliyoainishwa Barazani. Kati ya
fedha hizo, TSh. 118,683,500,000/= zimetengwa kwa kazi za kawaida na TSh.
19,462,084,000/= kwa kazi za maendeleo. Kati ya fedha za maendeleo, TSh.
4,500,000,000/= ni mchango wa SMZ na TSh. 14,962,084,000/= ni mchango wa Washirika
wa Maendeleo.
102.
Mheshimiwa Spika, Utekelezaji wabajeti
hii utategemea kupungua au kuondoka kabisa kwa janga la ugonjwa wa virusi vya
Korona (COVID 19). Tunamuomba Mwenyezi Mungu atujaalie ugonjwa huo umalizike.
Ikiwa hivyo, wanafunzi wataendelea na masomo yao kama kawaida wakiwa skuli.
Kama dhana yetu itakuwa sahihi bajeti yetu haitaathirika sana kwa yale
tuliyopanga kuyatekeleza. Aidha, Ugonjwa huu ukiendelea (tunamuomba Mwenyezi
Mungu asijaalie hivyo) na wanafunzi wakaendelea kuwa nyumbani, bajeti yetu
itaathirika na fedha nyingi zitatumika katika utekelezaji wa mpango wa
kukabiliana na COVID 19 katika kutoa elimu.
SHUKURANI
103.
Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa
hii kutoa shukurani za dhati kwa washirika wote wa sekta ya elimu wakiwemo
wananchi, washirika wa maendeleo na mashirika ya misaada ya kimataifa kwa
kutuunga mkono katika jitihada zetu za kuendeleza elimu. Tunatoa shukurani zetu za pekee kwa Serikali
ya Sweden, Marekani, Oman na Serikali ya Watu wa China, Serikali ya India na
Iran. Pia, napenda kuyashukuru mashirika mbalimbali ya kimataifa yakiwemo,
Sida, USAID, KOICA, UNESCO, UNICEF, ILO, VSO, GPE, Good Neighbours, Table for
Two na Patnership for Child Development.
Shukurani zetu za dhati ziende kwa Benki ya Dunia, Benki ya Kiarabu kwa
Maendeleo ya Afrika, Benki ya Maendeleo ya Afrika na Mfuko wa OPEC. Napenda
pia, kuyashukuru mashirika yasio ya kiserikali yakiwemo Milele Zanzibar
Foundation, Jumuiya ya Madrasa Early Childhood Education, NFU, FAWE, Save the
Children Fund, Book Aid International na ZAPDD. Vile Vile napenda kuyashukuru
makampuni na mashirika mbalimbali ya kifedha ya kiwemo ZTE, Benki ya watu wa
Zanzibar, CRDB, Barclays, NBC, NMB, Postal Bank Tanzania, ZANTEL, kampuni ya
SHA na ndugu Bakhresa. Aidha, napenda pia kuzishukuru Kampuni ya Bopar
Interprise, SACCOSS mbalimbali na kampuni Tigo kwa misaada yao katika sekta
yetu ya elimu na kwa wafanyakazi kwa ujumla. Shukurani za pekee ziendekwa Kamati
zetu za Skuli na Halmashauri zetu za Wilaya kwa kazi kubwa wanayoifanya katika
kusimamia maendeleo ya elimu Zanzibar.
104.
Mheshimiwa Spika, Shukurani za pekee
Chama change cha Mapinduzi kuanzia taifa hadi shina. Niushukuru uongozi mzima
wa Mkoa wa Kaskazini Unguja na wananchi wenzangu wote hasa kina mama kwa
kuendelea kuniamini na kushirikiana nami katika kuendelea kusimamia maendeleo
kwa taifa letu.
105.
Mheshimiwa Spika, shukurani kwa familia
yangu kwa ushirikiano wanaonipatia.
106.
Mheshimiwa Spika, mwisho, napenda kutoa
shukrani zangu za dhati kwa viongozi wenzangu kuanzia wewe Mheshimiwa Spika na
Wajumbe wa Baraza lako Tukufu kwa ushirikiano mkubwa walionipa na kwa namna
watakavyoichangia hotuba yangu hii. Nasema ahsanteni sana.
107. Mheshimiwa Spika, sasa naliomba Baraza lako Tukufu liidhinishe makadirio ya matumizi
ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ya jumla ya TSh. 138,145,584,000/= kwa
mwaka wa fedha 2020/21, ili kuiwezesha Wizara yangu kutekeleza majukumu yake.
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.
KIAMBATISHO
(Takwimu
za Maendeleo ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali
Kwa Kipindi cha 2015/16- 2019/20 na Hali
Halisi ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa Mwaka 2019/20)
No comments:
Post a Comment