Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akimpongeza Msanii wa Filamu Bw. Ezekiel
Mwakipageme maarufu kama Soudblack (wa kwanza kushoto) anayefanya kazi za
filamu nchini China kwa mpango wake wa kushirikiana na wasanii wenzake
watanzania katika kukuza tasnia ya filamu nchini wakati msanii huyo
alipomtembelea ofisini kwake leo Jijini Dodoma.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akimsikiliza Msanii wa Filamu Bw. Ezekiel Mwakipageme
maarufu kama Soudblack (wa (kwanza kushoto) kuhusu mpango wake kuendeleza
tasnia ya filamu nchini wakati msanii huyo alipomtembelea ofisini kwake leo
Jijini Dodoma.
Mtayarishaji na Mwongozaji wa Filamu Tanzania
Bw. John Kalaghe (wa kwanza kushoto) akifafanua jambo kwa Mhe. Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani)
kuhusu kazi za filamu wanazotarajia kuzifanya kwa kushirikiana na Msanii
Bw.Ezekiel Mwakipageme maarufu kama Soudblack (wapili kushoto) ofisini kwa
Mhe.Waziri leo Jijini Dodoma.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Dkt. Harrison Mwakyembe (watatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Msanii
wa Filamu nchini China, Bw.Ezekiel Mwakipageme maarufu kama Soudblack (wa pili
kushoto) mara baada ya kufanya nae mazungumzo ofisini kwake leo Jijini Dodoma.
Na.Adeladius Makwega -WHUSM
Serikali imesisitiza kuendelea
kutoa ushirikiano kwa wasanii kupitia vyombo na idara zake zinazosimamia sekta
hiyo ili kusaidia kazi zao kufahamika zaidi ndani na nje ya nchi.
Hayo yamesemwa leo jijini Dodoma
na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe wakati
alipotembelewa na msanii Ezekiel Mwakipageme maarufu kama Sud Black ambaye ni
msanii wa sanaa ya maigizo.
Waziri
Mwakyembe amesema kuwa sanaa ya Tanzania inapofanyika sehemu yoyote ni vizuri
kuwa ya mfano na yenye motisha kwa wale wanaotaka kufanya kazi za sanaa pamoja
na wale wanaozifuatilia kazi hizo.
“Hongera kwa kucheza
picha nyingi, kuigiza na wasanii wengi wakubwa na kwa kufanya hivyo umeweza
kuibeba na kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania huko nchini China na
kimataifa.” Amesema Waziri Mwakyembe.
Kwa upande wake, msanii Ezekiel
Mwakipageme amesema kuwa anatarajia kuwakaribisha wawekezaji kutoka China kuja
kuwekeza katika ulimwengu wa filamu kwa kujenga studio ya kisasa, chuo cha
michezo na pia kufungua miradi mingine ya maendeleo ikiwemo huduma za afya.
“Nimecheza filamu nyingi na
wasanii wakubwa kama Jack Chain na wengine na hivi karibuni zitatoka filamu
zangu mpya mbili, Watanzania watarajie mengi makubwa katika tasnia hii ya
filamu”, Alisema msanii Sud Black.
Nae
Mtayarishaji wa Filamu, John Kalage ambaye ndiye Mkurugenzi wa msanii huyo hapa
nchini Tanzania ameishukuru Serikali kwa ushirikiano wanaoutoa katika masuala
yote ya Filamu na Sanaa. kufanya kazi zetu kwa kufuata miongozo yote ya
serikali na kuondoa migongano isiyo ya lazima”, Amesema Mkurugenzi Kalage.
Serikali
ya Awamu ya Tano kama ilivyotoa ahadi yake ya kukuza sanaa na wasanii kwa
kufanya kazi za sanaa kuwa ajira kwa vijana imeendelea kutekeleza ipasavyo huku
baadhi ya wasanii wakiendelea kuibuka na kazi zao kuvuka mipaka ya taifa letu.
No comments:
Post a Comment