UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, Kwanza
kabisa naanza Hotuba hii kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mtukufu aliyetujaalia
afya njema na uzima tukaweza kukutana tena katika Baraza lako na kuendelea
kuwatumikia wananchi wetu ambao wametuamini na kutupa dhamana kubwa ya
kuwasemea na kutetea hoja zao mbali mbali kupitia chombo hichi. Aidha, nachukua
fursa hii kumpongeza Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. Ali Mohammed Shein
pamoja na Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar
kwa uongozi wao imara uliopelekea kudumu kwa amani na utulivu katika nchi yetu.
Kutokana na juhudi za viongozi wetu hawa pamoja na wasaidizi wao tumeshuhudia
maendeleo makubwa katika nyaja za kiuchumi, kisiasa na kijamii.
Mheshimiwa Spika,
natoa shukrani zangu za dhati kwako kwa namna unavyotuongoza katika Baraza letu
katika kipindi chote tulichotumikia pamoja na wasaidizi wako akiwemo Naibu
Spika na Wenyeviti wa Baraza. Aidha, nawashukuru watendaji wa Baraza hili
tukufu wakiongozwa na Katibu wa Baraza Ndg. Raya Issa Msellem.
Mheshimiwa Spika,
nikiri kuwa, kukamilika kwa hotuba hii kumetokana na ushirikiano mkubwa ambao
nimeupata kutoka kwa wajumbe wa Kamati katika kuibua hoja mbali mbali
zilizojadiliwa katika kikao cha majumuisho. Kwa kweli wamefanya kazi hii kwa
ufanisi mkubwa na napenda kuwatambua kwa kuwataja majina yao kama ifuatavyo:
1.
Mhe. Dkt. Mohamed Said
Mohamed Mwenyekiti
2.
Mhe. Bahati Khamis Kombo
M/Mwenyekiti
3.
Mhe. Abdalla Ali Kombo Mjumbe
4.
Mhe Ali Salum Haji Mjumbe
5.
Mhe. Asha Abdalla Mussa Mjumbe
6.
Mhe. Mohammedraza
Hassanali
Mjumbe
7.
Mhe. Salha Mohamed
Mwinjuma Mjumbe
Mheshimiwa
Spika, Kamati katika kutekeleza na kufanikisha majukumu
yake imekuwa ikisaidiwa na Sekretarieti iliyoundwa na makatibu watatu ambao
ni:-
1. Ndg. Abdalla Ali Shauri Katibu
2. Ndg. Shaib Fadhil Shaib Katibu
na
3.
Ndg. Asha Said Mohamed Katibu
Mheshimiwa Spika, Kanuni
ya 100(2) ya Kanuni za Baraza la
Wawakilishi (Toleo la 2016), inaitaka Kamati ya Bajeti kufanya majumuisho
kuhusu mijadala ya Bajeti za Wizara zote. Kwa kuzingatia Kanuni hii na kwa
ruhusa yako naomba kuwasilisha hotuba ya Kamati
ya Bajeti kuhusu Majumuisho ya Mijadala ya Bajeti za Wizara za Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2020/2021.
Mheshimiwa Spika, Kutokana na mijadala ya bajeti ilivyokwenda, Kamati ilikaa na baadhi ya Wizara ambazo hoja zao zilihitaji kujadiliwa katika kikao cha majumuisho. Kuna baadhi ya Wizara mijadala yake yote ilihitimishwa ndani ya baraza na hivyo kutokuwa na haja ya kujadiliwa tena hoja zao katika kikao cha majumuisho.
Mheshimiwa Spika, Kutokana na mijadala ya bajeti ilivyokwenda, Kamati ilikaa na baadhi ya Wizara ambazo hoja zao zilihitaji kujadiliwa katika kikao cha majumuisho. Kuna baadhi ya Wizara mijadala yake yote ilihitimishwa ndani ya baraza na hivyo kutokuwa na haja ya kujadiliwa tena hoja zao katika kikao cha majumuisho.
Mheshimiwa Spika, Mbali na hoja zilizoibuka katika majadiliano ya Bajeti
za Wizara ambazo zimewasilishwa katika taarifa hii, kuna maeneo ambayo yalijadiliwa
sana na wajumbe na ambayo kutokana na umuhimu wake Kamati yangu imeona ni
busara kuyatolea ushauri. Miongoni mwa maeneo hayo ni pamoja na uimarishaji
miundombinu ya barabara. Kwa vipindi tofauti, wajumbe wamekuwa wakichangia
suala la ubovu wa barabara za ndani katika majimbo yao. Pamoja na jitihada
kubwa inayochukuliwa na Serikali katika kuendeleza ujenzi wa barabara, bado kuna
baadhi ya barabara za ndani ambazo ni mbovu na nyengine zipo katika maeneo ya
utalii ambayo ni Sekta tunayoitegemea sana katika uchumi wetu. Kamati
inaishauri Serikali kusimamia marekebisho ya barabara za ndani hususan zile ambazo zipo katika maeneo ya utalii
ili kuyafanya maeneo hayo yawe mazuri na kuvutia wawekezaji.
Mheshimiwa
Spika, Eneo jengine ambalo Kamati yangu imeona ni busara
kulisisitiza ni kuchelewa kutumika kwa baadhi ya fedha za Programu za Miradi,
hali ambayo inapelekea fedha hizo kuombwa tena katika bajeti za mbele kama
ambavyo imejitokeza kwa Bajeti ya Wizara ya Vijana katika Programu ya
Kuendeleza Ajira kwa Vijana. Mheshimiwa
Spika, Kamati inaendelea kusisistiza kuwa ni muhimu sana kujipanga vizuri
katika kuendesha miradi ya maendeleo, kwani haileti taswira nzuri kwa bajeti ya
mwaka wa nyuma kuitumia miaka ya mbele. Hali hii sio tu inaathiri ufanisi wa
miradi lakini pia inatoa taswira ya uwezo mdogo wa Wizara katika kutumia fedha
wanazoidhinishiwa.
MAENEO
YALIYOCHANGIWA NA WAJUMBE WENGI
Mheshimiwa Spika, baadhi ya maeneo yaliyochangiwa na Wajumbe
wengi na kwa hisia zaidi ni pamoja na haya yafuatayo:
· Pongezi
kwa Mhe. Rais wa Zanzibar kwa maendeleo makubwa yaliyofikiwa na kuridhishwa na
utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi.
- Kuzifanyia
matengenezo barabara katika maeneo mbali mbali pamoja na kuzikarabati
sehemu zilizoharibika kutokana na mvua.
- Changamoto
ya migogoro ya ardhi.
- Ajira za
waalimu ambapo wajumbe wengi walichangia kuhusu umuhimu wa kuajiriwa
waalimu hasa wale waliokuwa hawajaajiriwa siku nyingi.
- Umuhimu wa
kuimarisha Sekta ya Uvuvi, Wajumbe wameishauri Serikali iimarishe Sekta ya
Uvuvi ili isaidiane na sekta nyengine hususan wakati sekta nyengine
zinapoyumba.
- Umuhimu wa
kuondolewa vikwazo vya biashara baina ya Zanzibar na Tanzania bara.
- Changamoto
za Mradi wa Pilipili.
- Ufanisi wa
Mradi wa Ujenzi wa Viwanja vya Michezo vya Wilaya.
· Umuhimu
wa kuzitafutia ufumbuzi changamoto za ubora wa majengo ya mahkama ikiwemo
majengo ya Mahkama za Wilaya na Mikoa.
· Ofisi
ya Mufti kupatiwa fungu la kibajeti (vote) ili iweze kutekeleza majukumu yake
kwa ufanisi.
· Utaratibu
wa kisheria unaotumika katika kuitishwa zabuni (tender).
· Upatikanaji
wa kampuni ambayo inafanya ukaguzi katika Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali.
· Kusimamiwa
vyema wamiliki wa vyombo vya baharini pamoja na kuepuka kupanda kwa bei za
tiketi bila ya utaratibu maalum.
· Umuhimu
wa kuratibiwa vyema usafiri wa boda boda na kutatua changamoto za ajali
zinazotokana na usafiri huo.
· Kuimarishwa
kwa utunzaji wa kumbukumbu za mahkama katika mfumo wa kielektroniki na mfumo wa
kawaida.
UFAFANUZI WA HOJA ZILIZOTOKANA NA MAJADILIANO YA MAJUMUISHO YA
MIJADALA YA BAJETI BAINA YA SERIKALI NA KAMATI YA BAJETI
Mheshimiwa
Spika, Kikao cha
majumuisho kilijadili jumla ya hoja nane (8) kutoka katika Wizara (5) ambazo
hazikupata ufafanuzi wa kina wakati wa mijadala ya upitishaji wa Bajeti za
Wizara. Hoja hizo, zimetoka katika mafungu tofauti katika bajeti za Wizara zikiwemo
hoja zinazohusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hoja za kutaka ufafanuzi wa
baadhi ya mafungu ya bajeti ambayo hayakufafanuliwa kwa kina na hoja za ulipaji
fidia kwa wananchi ambao wameathirika na ujenzi wa barabara.
Mheshimiwa Spika, ili kutowa urahisi wa ufafanuzi wa hoja zilizofanyiwa kazi na Kamati, Kamati yangu inaomba iwasilishe hoja hizo kwa njia ya Jadweli (Table) ambalo limegawika sehemu tatu; Sehemu ya Kwanza inahusu Hoja zilizoibuliwa, Sehemu ya Pili inahusu, Majibu ya Wizara na Sehemu ya Tatu ni Ushauri wa Kamati ya Bajeti.
Nam.
|
HOJA
|
MAJIBU YA
WIZARA
|
MAONI YA KAMATI
|
|
Wizara
ya Biashara na Viwanda
|
||||
1
|
Hoja ya kwanza ilikua inahusu Mradi wa Pilipili, ambapo kutokana na
changamoto zinazoukabili mradi huo, Serikali iliamua Mradi huo usimamiwe na
Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi pamoja na
Shirika la Biashara la Taifa (ZSTC).
Aidha, fedha zilizobakia za Mradi huo Tsh 376,462,104 ziliamuliwa kurejeshwa Wizara ya Vijana. Baadhi ya
Wajumbe waliochangia walitaka kupatiwa
ufafanuzi kama ifutavyo:-
a. Jee fedha hizo
tayari zimesharejeshwa Wizara ya Vijana?
b. Iwapo fedha hizo
tayari zimesharejeshwa kwanini hazikuonyeshwa katika Bajeti ya Wizara ya
Vijana?
c. Iwapo fedha hizo bado hazijarejeshwa Wizara ya Vijana,
lini zinatarajiwa kurejeshwa na
zitatumika kwa bajeti ya mwaka gani?
|
Fedha za Mradi wa Pilipili ambazo
ziliamuliwa kurejeshwa Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo bado
hazijarejeshwa kwakuwa ni muda mfupi tokea kutolewa maamuzi ya mradi huo
kurejeshwa Wizara ya Vijana. Hatua inayoendelea sasa ni kufanya uchambuzi wa
mapendekezo yaliyotolewa. Kwa hiyo, fedha
hizo hazikuonekana katika Bajeti za Wizara zote mbili kwa sababu ni fedha
zinazotokana na bajeti ya mwaka 2018/2019. Aidha, kwakuwa fedha hizo, zina
ahadi “Commitment” ya Serikali zitaingizwa katika Bajeti ya Wizara ya Vijana
mara baada ya taratibu za uchambuzi kukamilika.
|
Kimsingi Kamati imeridhika na majibu
ya Serikali. Hasa kwa kuzingatia kuwa msingi wa pendekezo hilo ni Wajumbe wa
Baraza na Kamati husika ya Kisekta. Kamati inaendelea kusisitiza kuwa mara baada
ya kukamilika kwa taratibu za uchambuzi fedha hizo ziingizwe na zitumike kwa
mujibu wa malengo. Aidha, Wizara ihakikishe inasimamia vyema Mradi huo ili
uwe na tija na malengo ya kuwasaidia vijana yaweze kufikiwa kwa kuzingatia
maoni ya wataalamu.
|
|
Wizara
ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo
|
||||
1
|
Hoja ya pili inahusu matumizi ya fedha za Programu
ya kuendeleza vijana ambapo, kwa
mujibu wa Hotuba ya Mhe. Waziri wa Vijana, Utamaduni Sanaa na Michezo, Mnamo
mwezi wa Julai 2019/2020, Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo iliingiziwa jumla ya shilingi
2,000,000,000/= kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali, fedha ambazo zinatokana na
bajeti ya mwaka 2018/2019, fedha hizo
zote zimetumika kwa shughuli mbali mbali za kuendeleza vijana. Aidha, kwa
bajeti ya mwaka 2019/2020 Programu hii
pia ilipangiwa tena Tsh 2,000,000,000. Kamati iliomba kupatiwe ufafanuzi
ufuatao?
Kwakuwa fedha za bajeti ya mwaka 2018/2019 zimetumika katika mwaka wa
fedha 2019/2020. Jee fedha za bajeti ya 2019/2020 zimepatikana ngapi na
zimetumika vipi. Hasa ikizingatiwa kuwa fedha hizo hazikuonyeshwa matumizi
yake katika bajeti ya 2020/2021.
|
Ni kweli fedha za bajeti ya mwaka
2019/2020 bado hazijatumika kutokana na kuchelewa kukamilika taratibu. Hata
hivyo, mikataba ya fedha hizo tayari imeshakamilika na tayari zimeshaombwa na
pia zina ahadi ya Serikali “Commitment”. Hivyo, fedha hizo zitapatikana na
zitatumika kama ilivyopangwa.
|
Kamati imeridhika na maelezo ya
Wizara kwa msingi kwamba, fedha hizo zina ahadi ya Serikali “Commitment” na
pia mikataba ya matumizi yake imeshakamilika. Aidha, ili kujiridhisha na
ukweli huo Kamati imeiagiza Wizara kuwasilisha nakala za mikataba hiyo kabla
mjadala wa Bajeti kuu kuanza. Kamati inaendelea kusisitiza wajibu wa Taasisi
za Serikali kufanya matumizi ya fedha kama zinavyoidhinishwa na kwa wakati.
|
|
Wizara ya Kazi,
Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto
|
||||
1
|
Programu ya Uwezeshaji Wananchi
Kiuchumi (PQ 0101) ilikadiriwa kutumia jumla ya TZS 1,849,399,000 kwa mwaka
wa fedha 2019/2020. Aidha, katika Hotuba ya Wizara, umetolewa uchanganuzi wa
matumizi wa fedha hizo kama ifuatavyo:
Jumla ya TZS 789,348,000 zimetumika
kwa kutoa mikopo 811 Unguja na Pemba. Jumla ya TZS 872,818,764 zilipatikana.
Kwa kuangalia kiasi cha fedha kilichopatikana na kilichotumika, kunaonekana
kuna tofauti ya TZS 83,470,764 milioni. Kamati ilihoji kwa nini ufafanuzi wa
matumizi ya fedha uliotolewa, haulingani na makadirio ya programu ya
uwezeshaji Wananchi kiuchumi (PQ0101).
|
Wizara ilieleza kuwa, ni kweli Programu Kuu
ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (PQ0101) ilikadiriwa kutumia jumla ya TZS
1,849,399,000 kwa mwaka wa fedha 2019/2020. Fedha hizo ziliidhinishwa kwa
ajili ya matumizi mengineyo na Mishahara kwa Programu ndogo 3 ambazo ni
Programu Ndogo ya Mfuko wa Uwezeshaji, Programu Ndogo ya Usimamizi na
Uimarishaji wa Vyama vya Ushirika na Programu Ndogo ya Uratibu na Uendelezaji
wa Programu za Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi. TZS 789,348,000 ni fedha ambazo
zilitumika kwa utolewaji wa mikopo na hazihusiani na fedha zilizoidhinishwa
katika Kitabu cha Makadirio ya Bajeti. Programu Ndogo ya Mfuko wa Uwezeshaji
kwa mwaka wa fedha 2019/2020 iliidhinishiwa jumla ya TZS 269,470,080 na
kufanikiwa kupata TZS 168,793,576. Uchambuzi wa matumizi ya fedha hizo
unapatikana katika Kiambatanisho Nambari 1 cha Kitabu cha Hotuba ya Waziri.
|
Kamati imeridhika baada ya kupatiwa
ufafanuzi wa kuridhisha.
|
|
Wizara
ya Katiba na Sheria
|
||||
|
Hoja ya nyengine iliyoibuka ni
matumizi yaliyopangwa katika Programu ya Uendeshaji na Uratibu wa Wizara ya
Katiba na Sheria kifungu SG100302 ya Jumla ya TZS 2,344,079,000 kwa mwaka wa
fedha wa 2020/2021. Wakati wa mjadala wa Wizara hii, matumizi hayo
hayakutolewa ufafanuzi wa kina.
|
Idara ya Mipango
Sera na Utafiti ilipanga jumla ya Tsh 2,344,079,000 kwa ajili ya shughuli kuu
3 kwa mchanganuo ufuatao:
i.
Mradi wa Ujenzi wa Skuli ya
Sheria Tsh 1,500,000,000
ii.
Ruzuku Skuli ya Sheria Tsh
520,000,000
iii.
Matumizi ya Kawaida Tsh
324,079,320
Jumla
Tsh 2,344,079,000
|
Kamati iliridhika na uchanganuzi
uliotolewa
|
|
Wizara ya
Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji
|
||||
1
|
Katika mjadala wa bajeti ya 2020/2021,
Mheshimiwa Mjumbe alitoa hoja katika Kifungu P010103 kuhusu Miundombinu ya
Usafirishaji. Mjumbe hakuridhika na majibu ya Mhe. Waziri kuhusiana na
ulipaji wa fidia kwa wananchi walioathirika na utengenezaji wa barabara ya
Wete – Gando. Mheshimiwa Mjumbe alisisitiza kwamba, mbali na wale ambao
waliothirika wakati ujenzi ukiendelea lakini hata wale ambao nyumba zao
zimebomolewa kwa ajili ya kupisha ujenzi bado hawajalipwa. Ametoa mfano,
Bwana Hamad Iddi Hamad ambaye Mheshimiwa Mjumbe alishuhudia kwa macho yake
nyumba inatiwa grader, na mpaka
sasa hajalipwa fidia yake. Hoja ya Mjumbe hapa ambayo bado Wizara haijaijibu
ni kuelezwa lini wananchi hawa watapatiwa fidia zao ukizingatia kwamba
tathmini zimeshafanyika. Aidha katika hoja hii, Mheshimiwa Spika aliitaka
Serikali ilipe fidia kwa thamani ya sasa kwani ni muda mrefu umepita.
|
Wizara imekiri kuwepo kwa tatizo la
malalamiko ya ulipaji fidia kwa wananchi waliothirika na utengenezaji wa
barabara ya Wete – Gando licha ya kwamba Serikali imeshatoa fedha zote kwa
ajili ya malipo ya fidia za nyumba zilizobomolewa wakati wa ujenzi wa
barabara hiyo. Kinachodaiwa kwa sasa ni fidia za vipando tu.
|
Kamati imegundua kwamba, kuna matatizo
katika ulipaji fidia, kuna uwezekano mkubwa wahusika hawakupata fidia zao licha
ya Serikali kutoa fedha za fidia hizo. Hali hii imesababishwa na watendaji
wasio waaminifu pamoja na kutofuata taratibu za malipo kwa usahihi. Mfano,
kumejitokeza kasoro ya baadhi ya watu kusainiwa na watu wengine wakati wa
kuchukua malipo. Kutokana na hivyo, Kamati inaishauri Wizara, ifanye uhakiki
wa malipo ya fidia yaliyofanyika je waliolipwa ndio waliostahiki. Pia, iwapo
Wizara itabaini kama kuna watendaji wameshiriki katika vitendo vya
kuwadhulumu wananchi fidia zao, iwachukulie hatua za kisheria haraka
iwezekavyo. Ni matumaini ya Kamati kwamba, jambo hili litamalizwa kwa haki
ili kila mwenye haki apate haki yake na kuepusha malalamiko na masononeko ya
mara kwa mara.
|
|
2
|
Katika barabara ya Ole - Kengeja kuna wananchi ambao bado
hawajalipwa fidia zao licha ya kwamba wameshafanyiwa tathmini ya kulipwa
lakini mpaka leo hii hawajalipwa. Mheshimiwa Mjumbe alipokuwa anajenga hoja
yake alisema kwamba, Mhe. Rais wa Zanzibar aliwahi kutamka kwamba
atakapoondoka atahakikisha kwamba kwa kila alichokianzisha kisiwe na doa,
anahitaji asiache madeni. Jee fedha hizi lini zitapatikana?
|
Wizara imeahidi kulifanyia kazi suala hili.
|
Kama ilivyo katika hoja ya ulipaji fidia kwa
walioathirika na ujenzi wa barabara ya Wete – Gando, Kamati inaishauri Wizara
kufanya uhakiki na tathmini na iwapo kama itabaini kwamba kuna wananchi bado
wanadai fidia zao, basi taratibu za kuwalipa zitekelezwe haraka. Na
ikibainika kwamba, malamiko haya yamejitokeza kutokana na watendaji wasio
waaminifu, basi wachukuliwe hatua za kisheria haraka sana. Tusiwe na muhali
katika haki za wananchi wetu.
|
|
HITIMISHO
Mheshimiwa Spika, Kamati
kwa vipindi tofauti ambavyo ilifanya vikao vya majumuisho baina yake na Wizara
za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imefarijika kwa hatua mbali mbali za
utekelezaji ambazo Serikali imechukuwa. Kwa kweli hatua hizo zimesaidia sana
katika kufikia malengo ya utekelezaji wa bajeti zetu pamoja na kupata ufumbuzi
wa mambo. Kwa kumalizia, Kamati inazishukuru sana Wizara zote ambazo
zimeshirikiana na Kamati katika kufanikisha kazi zake mbali mbali. Aidha, kwa
kuwa Kamati hii itakuwa ni mara yake ya mwisho kuwasilisha taarifa ya aina hii,
ni matumaini yangu kuwa, wajumbe wengine wa Kamati ya Bajeti wataokuja katika
Baraza lijalo wataendelea kusimamia na kuishauri Serikali katika kusimamia
utekelezaji wa hoja mbali mbali za Bajeti zilizoibuliwa.
Mheshimiwa Spika, namalizia
hotuba hii kwa kukushukuru wewe kwa kunipatia nafasi hii na pia nawashukuru Wajumbe
wa Baraza lako kwa utulivu na usikivu wao kwa muda wote ambao niliwasilisha
hotuba hii. Nawatakia kheri na mafanikio nyote na naomba kuwasilisha.
Ahsante,
Dkt. Mohamed Said Mohamed,
Mwenyekiti,
Kamati ya Bajeti,
Baraza la Wawakilishi,
Zanzibar.
No comments:
Post a Comment