Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza wakati akifungua Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, kilichofanyika katika ukumbi wa White House Jijini Dodoma leo.20/8/2020.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), na Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli amewasihi Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, kujadili
mapendekezo ya wagombea kwa kuweka mbele maslahi ya Chama na Taifa kwa jumla
kwani wanaCCM na Watazania wanaimani kubwa
na chama hicho.
Wito huo ameutoa leo katika Mkutano Mkuu wa
Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa CCM
(White House), Jijini Dodoma na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa chama
hicho akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambaye pia,
ni Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein.
Rais Magufuli alitoa wito huo wa kujadili
mapendekezo kwa umakini mkubwa kwa kumtanguliza Mwenyezi Mungu mbele na
kuyatuanguliza mbele maslahi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Taifa na kutoweka
mbele udugu, urafiki, ukanda ama dini bali uwezo wa mtu uongoze.
Alisema kuwa hivyo ndivyo walivyofunzwa na waasisi
wa chama hicho Hayati Mzee Abeid Amani karume na Hayati Mwalimu Julius Nyerere
na huo ndio msingi uliopelekea chama hicho kuendelea kuaminiwa na wananchi
tokea nchi hiyo kupata uhuru.
Aliwashukuru wajumbe wa NEC kwa kumpigia kura
nyingi na pale walipokwenda katika maeneeo yao walishiriki wka akiasi kikubwa
katika kumtafutia wadhamini ambapo alipata wadhamini zaidi ya Milioni 1.1 huku
akisema kuwa alipata wadhamini wengi sana katika Mikoa yote ya Tanzania Bara na
Zanzibar.
Alisema kuwa mkutano huo ulikuwa na ajenda moja
kubwa wa kufanya yteuzi wa kugombea Ugunbe na Uwakilishi, ambapo mchakato wake
ulizna mwezi mmoja uliopita ambapo wajumbe walipiga kura na kupendekeza majina
na baada ya kupitia ngazia mbalzai mbali waliwepza kufika katika kikao hicho.
Aliwapongeza wagombea wote wa CCM waliojitikeza
kugombea nafasi mbali mbali kwani walikuwa ni wengi sana hiyo ni kutokana na
kuwa chama hicho kinapendwa.
Alieleza kuwa wagobea walikuwa ni wengi sana
wakiwemo wafanyakazi, akinamama , wasomo, akibababa, viongozi wa NGOs, wavuvui
na walemavu wote waliomba CCM, hiyo ni kusipitishwa kuwa CCM inapenwa sana.
Alisema kuwa hapana chama waliojitokeza Wagombea wengi
hatua ambayo inayonesha ni kuvunja rekodi katika bara la Afrika kuwa ni chama
kinachopendwa na kinachoheshimika na kikubwa chenye mtandao mkubwa katika
kuleta ushindi.
Rais Dk. Mgufuli alisema kuwa hayo ni matokea
makubwa na kazi nzuri katika kusimamia
chama na Serikali katika utekelezaji wa Ilani, ambapo katika miaka mitano
wajumbe hao wamekuwa wakitembelea miradi mbali mbali na kutoa maelekezo pamoja
na kukemea kwa wale waliozembea, ambapo miradi mingi imeweza kukamilika katika
Majimbo yao.
“Huu ni ushahidi kwamba Wajumbe wa NEC wamesimamia
Chama na Utekelezaji wa Ilani ya CCM……….Hayo ni matunda mazuri ya uchapakazi
wenu na ndio maana mkaona watu wengi wamejitokeza katika kugombea nafasi mbali
mbali kupitia CCM”, alisema Dk. Magufuli.
Alisema kuwa vikao vilivyopita vilijadili vizuri
sana ndani ya siku mbili na kufanya uchambuzi wa kina ambapo walitumia vianzio
vingi na kuwahakikishia wajumbe kwua ameseoma majina yote 10367.
Alieleza kuwa hawakumpendelea mtu ama kumnyima mtu
haki yake na badala yake walitumia taarifa nyingi na kuwajadili wagombea kwa
muda mrefu ili watakaopitishwa wawe watu wenye uwezo wa kuipeperusha vyema
bendera ya CCM na hatimae kuleta ushindi na kukipelekea chama hicho kuendelea
kuongoza nchi.
Aliongeza kuwa kulikuwa na haja ya kufanya
uchambuzi wa kina kwani unyeti wa nafasi zinazogombewa za Ubunge na Uwakilishi
ni nyeti na muhimu sana kwani hao ni wasemaji wa wananchi kwani pia, wanajukumu
na kusimamia Serikali, hivyo ilikuwa ipo haja ya kufanywa mchakato huo mkubwa.
Alisema kuwa kwani ndani ya Wabunge na Wawakilishi
ndimo anakapopatikana Waziri Mkuu, Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mawaziri
na Manaibu Waziri, Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge na Baraza la Wawakilishi.
Hivyo, Mwenyekiti huyo wa CCM alisema kuwa ni
vyema kuwajadili kwa dhati kabisa kwani ili kudhiridhisha kuwa wale
watakaopitishwa wana sifa zinazostahili kuwa viongozi na wanaofahamu Dira za
nchi na Sera za CCM.
Rais Magufuli aliwashukuru Wajumbe wa Kamati Kuu
kwa kazi nzuri walizofanya siku mbili ambayo imerahisisha kufanya shughuli hiyo
na kusema kuwa Kamati ya Usalama na Maadili na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu
zimejitahidi kuchambua na kupata wagombea wawenye sifa zinazokubalika zikiwemo
kuwa wazalendo, kujitoa kwenye chama, wenye utayari kuwatumikia wananchi na
Watanzania wote na ambao wanokubalika na wananchi.
Alisema kuwa baada ya mchakato uliofanyika kuanzia
ngazi ya Jimbo hadi Kamati Kuu na kueleza kuwa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM
ndiyo iliyopewa jukumu la mwisho la kufanya uteuzi wa mwisho wa Ubunge na
Uwakilishi.
Mapema Katibu Mkuu wa CCM Bashiru Ali Kakurwa
alisema kuwa kikao hicho hakitajadili nafasi za Uwakilishi na badala yake
kitafanya zoezi hilo kwa nafasi ya
Ubunge pekee.
Aliongeza kuwa watakaoteuliwa na kikao hicho ndio
watakaopata nafasi ya kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment