Habari za Punde

Dk. Shein Amewataka WanaCCM Pamoja na Wananchi Kisiwani Pemba Kumchagua Dk Hussein Mwinyi


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia katika Uwanja wa Gombani  ya Kale Chakechake Pemba wakati wa Ufunguzi wa Kampeni za CCM Pemba kuwatambulisha Wagombea wake. na kumptambulisha Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Hussein Mwinyi.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambaye pia ni Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein amewataka wanaCCM pamoja na wananchi kiswani Pemba kumchagua Dk. Hussein Ali Hassan Mwinyi kuwa Rais wa Zanzibar kwani ndie pekee anaeweza kuyalinda Mapinduzi ya Januari 12, 1964 pamoja na kuutunza Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Dk. Shein aliyasema hayo leo katika mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kisiwani Pemba, uliofanyika katika viwanja vya Gomnani ya Kale, Chake Chake Pemba katika Mkoa wa Kusini Pemba ambao ulihudhuriwa na mamia ya wanaCCM.

Katika maelezo yake, Makamo Mwenyekiti huyo wa CCM Zanzibar alisema kuwa
Dk. Hussein Mwinyi ndie pekee anaeweza kuyalinda na kuyatunza Mapindzi ya Januari 12.1964 pamoja na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na hakuna kiongozi mwengine anaeweza kutekeleza hayo miongoni mwa wale wanaogombea nafasi hiyo.

Makamao Mwenyekiti  huyo wa CCM alieleza kuwa Zanzibar imepata uhuru wake kupitia Mapinduzi Matukufu yaliyofanyika mwaka 1964 ambapo kipindi chote hicho hadi hivi leo CCM ndio inayoongoza dola hivyo, chama hicho kinatambua mahitaji na maisha ya wananchi hasa wanyonge.

Rais Dk. Shein alisema kuwa Dk. Hussein Mwinyi anaiweza kazi ya kuyalida Mapinduzi na kuuimarisha Muungano kwani ameshaifanya kwa kipindi kirefu kupitia nafasi za uongozi alizoitumikia ndani ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwemo kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa kipindi kirefu sambamba na kuwa Waziri katika Ofisi ya Makamo wa Rais anayeshughulikia masuala ya Muungano.

Aidha, Makamo huyo Mwenyekiti wa CCM alisema kuwa siku zote chama hicho hakibahatishi kuwachagua viongozi wake katika nafasi za Urais na ndio maana katika chaguzi zote wamekuwa wakipata ushindi mkubwa, hivyo kuchaguliwa kwa Dk. Hussein Mwinyi kunaonesha wazi usshindi w akishindo kwa CCM unakuja.

Rais Dk. Shein alisema kuwa CCM imemchagua Dk. Hussein Mwinyi kuwa mgombea nafasi ya Urais kutokana na sifa zote za kuwa Rais hasa ikizingatiwa kuwa yeye anapenda haki na anaichukua rushwa kwani ni mtu safi.

Pia, Rais Dk. Shein alisema kuwa Dk. Hussein Mwinyi ni mtu mwenye maadili na kiongozi mchapa kazi mahiri na mwenye elimu kubwa na mwenye utaalamu wa afya  na aliyebobea katika fani hiyo kwani ni mtu anayejituma sana.

Rais Dk. Shein alisema kuwa yeye mwenyewe binafsi anamfahamu sana Dk. Hussein Mwinyi kutokana na kuwa ameshawahi kufanya nae kazi wakati Rais Dk. Shein akiwa Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Dk. Hussein Miwnyi akiwa Waziri katika Ofisi hiyo anayeshughulikia Muungano.

Aliongeza kuwa Dk. Hussein Mwinyi ni kiongozi mwenye maadili, heshima na nidhamu ya hali ya juu na hawezi kufananishwa na wagombea wengine wa nafasi hiyo ya Urais wa Zanzibar.

“Dk. Hussein ataongoza ushindi wa CCM kwani aliyepewa kapewa na wala hapokonyeki kwnai uwezo wake mkubwa sana”alisisitiza Makamo Mwenyekiti huyo wa CCM Zanzibar.

Hivyo, Rais Dk. Shein aliwataka wananchi wa kisiwa cha Pemba kutokubali kubabaishwa wala kulazimishwa kumchagua mtu asie kuwa na sifa za kuiongoza Zanzibar na badala yake wamchague kiongozi kutoka CCM.

Aidha, Rais Dk. Shein alieleza matumaini yake makubwa aliyonayo kwa Dk. Hussein Mwinyi katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi mpya ya mwaka 2020-2025 kama alivyosimamia yeye Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2010-2015 na ile ya 2015-2020.

Makamo Mwenyekiti huyo alitumia fursa hiyo kumuombea kura Dk. Hussein Mwinyi pamoja na  wagombea wengine wote wa CCM wa kisiwani Pemba huku akitumia fursa hiyo kuwanadi wagombea Ubunge, Uwakilishi na Udiwani wa CCM wa Mikoa Miwili ya Pemba pamoja na kuwakabidhi Ilani ya chama hicho ili waende wakainadi kwa wananchi.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.