Msanii wa muzi wa Kizazi Kipya Bongo Flava Mabawa na Msanii Mkongwe wa Zanzibar muziki wa Taraab Bi. Fatma Issa wakitowa burudani ya wimbo maalum wa kampeni wakati wa kutambulisha Mgombea Urais wa Zanzibar Mhe.Dk. Hussein Mwinyi kwa Wananchi wa Wilaya ya Wete Pemba, mkutano uliofanyika katika uwanja wa mpira Gando leo.
Manju wa Mkota Ngoma Othman Ali Hatib akitowa burudani wakati wa mkutano wa Kampeni ya Chama Cha Mapinduzi kumnadi mgombea wa Urais wa Zanzibar Mhe.Dk. Hussein Mwinyi katika uwanja wa mpira Gando Wilaya ya Wete Pemba kumuombea kufra kwa Wananchi wa Pemba.
Wasanii wa Kikundi cha Ngoma ya Msewe kutoka Mchangamdodo Kijiji cha Kambini Kichokocho wakionesha umahiri wa kucheza msewe wakati wa mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Mhe.Dk. Hussein Mwinyi uliofanyika katika Uwanja wa Mpira Gando Wilaya ya Wete Pemba.
No comments:
Post a Comment