Habari za Punde

Wasanii Wanogesha Mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Hussein Mwinyi Viwanja vya Gando Wilaya ya Wete Pemba leo.Wanacha

Msanii wa muzi wa Kizazi Kipya Bongo Flava Mabawa na Msanii Mkongwe wa Zanzibar muziki wa Taraab Bi. Fatma Issa wakitowa burudani ya wimbo maalum wa kampeni wakati wa kutambulisha Mgombea Urais wa Zanzibar Mhe.Dk. Hussein Mwinyi kwa Wananchi wa Wilaya ya Wete Pemba, mkutano uliofanyika katika uwanja wa mpira Gando leo.


Manju wa Mkota Ngoma Othman Ali Hatib akitowa  burudani wakati wa mkutano wa Kampeni ya Chama Cha Mapinduzi kumnadi mgombea wa Urais wa Zanzibar Mhe.Dk. Hussein  Mwinyi katika uwanja wa mpira Gando Wilaya ya Wete Pemba  kumuombea kufra kwa Wananchi wa Pemba. 


Wasanii wa Kikundi cha Ngoma ya Msewe kutoka Mchangamdodo Kijiji cha Kambini Kichokocho wakionesha umahiri wa kucheza msewe wakati wa mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Mhe.Dk. Hussein Mwinyi uliofanyika katika Uwanja wa Mpira Gando Wilaya ya Wete Pemba.  



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.