Habari za Punde

Sherehe ya kuwaaga wahitimu wa kada ya Uuguzi na Ukunga yafanyika SUZA Kampasi ya Vuga

Mkuu wa kada ya Uuuguzi na Ukunga wa skuli ya Afya  na Sayansi za Tiba SUZA  Mwanaisha Juma Fakih akimkaribisha mgeni Rasmi katika sherhe ya kuwaaga wahitimu wa kada ya ukunga na uuguzi Skuli ya Afya na Sayansi za tiba huko Suza Kampasi ya Vuga.

Wahitimu wa kada ya Uuguzi na Ukunga wakiimba wimbo maalum uitwao (I'M PROUD TO BE A NURSE)  katika sherehe ya kuwaaga wahitimu wa kada ya Ukunga na Uuguzi huko SUZA Kampasi ya Vuga. 
 

Mwenyekiti wa Wakunga na Wauguzi Prof. Amina Abdulqadir akizungumza na Wakunga na Wauuguzi( hawamo pichani)katika sherehe ya kuwaaga wahitimu wa kada ya Ukunga na Uuguzi huko SUZA Kampasi ya Vuga.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar ( SUZA akizungumza na wahitimu wa  kada ya Uuguzi na Ukunga  katika sherehe ya kuwaaga wahitimu wa kada ya ukunga na uuguzi huko Suza Kampasi ya Vuga

Waziri wa  Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto Maudeline Cyrus Castico akimkabidhi zawadi Mhadhiri mkuu Idara ya Uuguzi na Ukunga (SUZA) Rukia Rajab Bakar kufatia kuhitimu Uzamivu wa Afya ya Jamii katika chuo cha Kilimanjaro Christian Medical University College (KCMUCo) Moshi Tanzania hafla iliyopfanyika Ukumbi wa SUZAKampasi ya Vuga.


 Waziri wa Wizara ya Kazi Uwezeshaji Wazee Wanawake na Watoto Maudeline Cyrus Castico akizungumza na wakunga na Wauuguzi( hawamo pichani)katika sherehe ya kuwaaga wahitimu wa kada ya Ukunga na Uuguzi huko Suza Kampasi ya Vuga

PICHA NA FAUZIA MUSSA /MAELEZO ZANZIBAR.


NA MIZA KONA MAELEZO/ZANZIBAR    

WAZIRI WA Elimu na Mafunzo ya Amali Mhe. Riziki Pembe Juma amewataka wanafunzi waliomaliza kada ya Uuguzi na Ukunga kuyatekeleza kwa vitendo mafunzo waliyoyapata kwa lengo la kutoa huduma bora kwa jamii.

Akizungumza kwa niaba, Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto Maudline Syrus Castico katika hafla ya Kuwaaga wanafuzi walinaomaliza Kada ya Uuguzi na Ukunga wa Skuli ya Afya na Sayansi za Tiba huko Ukumbi wa SUZA Vuga,

Amesema wauguzi na wakunga wana umuhimu mkubwa kwa jamii katika kutoa huduma ya Afya na kuwa watetezi wakuu kwa wanawake na watoto katika kupinga vitendo vya udhalilishaji.

Amewasisitiza kufuata kanuni za maadili ya uuguzi na Ukunga kwa kutumia lugha nzuri kwa wagonjwa na kutoa mashirikiano na upendo katika utoaji wa huduma kwa wagonjwa ili kuweza kutoa huduma nzuri na kupata mafanikio katika fani yao  hiyo.

Waziri Castico amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein kwa kukiunganisha na kukipa hadhi Chuo cha Afya kuwa na hadhi ya chuo Kikuu cha Taifa pamoja na kutekeleza kwa vitendo shabaha ya Mapinduzi ya kutoa elimu kwa wananchi wote bila ya ubaguzi.

aidha Waziri huyo alimkabidhi zawadi maalum Mhadhiri Mkuu Idara ya Ukunga na Uuguzi Dk.Rukia Rajab Bakar mara baada ya kuhitimu  masomo yake katika ngazi ya uzamivu wa Afya ya jamii.

Nae Makamu Mkuu wa Chuo wa  hicho Dk. Zakia Mohamed Abubakar amesema fani ya uuguzi na ukunga ni sekta inayohitajika sana katika kuboresha maisha ya wananchi na kupata Taifa bora na lililoimara.

Mapema Mwenyekiti wa Baraza la Wakunga na Wauguzi Profesa Amina Abdulkadir amewahimiza wahitimu hao  kufuata sheria na maadili ya fani hiyo katika kutekeleza majukumu yao ili kupata mafaniko na maendeleo zaidi.

Ameeleza mashirikiano ya pamoja baina ya wauguzi wa zamani na waliopata eluimu ya sasa ndio yatayoweza kusaidia kukuza taaluma hiyo na kuboresha utoaji mzuri wa  hudunma

“Tunawapima wanafunzi wetu kwa kutumia H 3, H ya kwanza ni kichwa na H ya pili ni Mikono na H ya tatu ni moyo. Hizi H tatu mkizitumia vizuri mtafanikiwa katika kuwahudumia wagonjwa na kutoa huduma kwa upendo na uadilifu”, alifahamisha Bi Amina.

Bi Amina amewasisitiza wahitimu hao kujiendeleza kielimu kwa dhamira ya kupata ujuzi zaidi ili kuweza kufanyakazi kwa ufanisi mkubwa katika kuimarisha huduma ya afya nchini.

Akisoma risala mwanafunzi Rashid Hilal Mohamed amesema wanakabiliwa na changamoto ya kukosa wasimazi kutoka chuoni  wanapokwenda kujifunza kwa  vitendo katika vituo vya afya kwani wafanyakazi wa vituo hivyo hukabiliwa na majukumu yao mengine jambo linalopelekea kukosa maelekezo mazuri ya vitendo.

Aidha wameupongeza uongozi wa Chuo hicho kwa kuwafundisha na kuwapa mafunzo mazuri na kupata mafanikio katika fani yao hiyo na kuweza kufaulu bila ya usumbufu. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.