Habari za Punde

Wagombea Urais walio Pemba walivyopiga kura leo

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia chama cha ADC Taifa Hamad Rashid Mohamed, akitumbukiza kura yake katika moja ya masanduku ya kura yaliyowekwa na tume ya uchaguzi Zanzibar ZEC, katika kituo cha kupigia kura Fidel Casro Wawi jimbo la Wawi.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia chama cha ADC Taifa Hamad Rashid Mohamed, akitumbukiza kura yake katika moja ya masanduku ya kura yaliyowekwa na tume ya uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania NEC, katika kituo cha kupigia kura Fidel Casro Wawi jimbo la Wawi.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia chama cha wananchi CUF Mussa Haji Kombo, akitumbukiza kura yake katika moja ya masanduku ya kupigia kura yaliyowekwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC)katika kituo cha Wara kilimo Mchaomanne jimbo la Wawi. (PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia chama cha wananchi CUF Mussa Haji Kombo, akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya habari Tanzania, mara baada ya kupiga kura kituo cha Wara kilimo Mchaomanne jimbo la Wawi.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

BAADHI ya wananchi wa jimbo Wawi Wilaya ya Chake Chake, wakitumbukiza karatasi zao za kupigia kura baada ya kuchagua kiongozi anaye mtaka, katika kituo cha kupigia kura wawi B jimbo la Wawi.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia chama cha Wakulima Tanzania (AFP) Said Soud Said, akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya habari Tanzania, mara baada ya kupiga kura kituo cha Skuli ya Wawi Jimbo la Wawi Wilaya ya Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

BAADHI ya akinamama wa jimbo la kojani Wilaya ya Wete wakiwa katika foleni kusubiri kupiga kura katika kituo cha kupigia kura skuli ya Kangagani Jimbo la Kojani Wilaya ya Wete.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia chama cha NRA Zanzibar Khamis Faki Mgau, akitumbukiza kura yake katika moja ya masanduku yaliyowekwa na Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC) katika moja ya vituo vya kupigia kura skuli ya Kangagani jimbo la Kojani.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MGOMBEA Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha NRA Taifa Khamis Ali Hassan, akitumbukiza karatasi yake ya kupigia kura katika moja ya masanduku ya upigaji wakura yaliyowekwa na Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika moja ya vituo vya kupigia kura skuli ya Kangagani jimbo la Kojani.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)


 

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia chama cha AFP Said Soud Said, akitumbukiza karatasi yake ya kupigia kura katika sanduku maalumu la kupigia kura lililowekwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kituo cha kupigia kura Skuli ya Wawi jimbo la Wawi.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.