Watumiaji wa
huduma za kibenki wameshauriwa kupata ushauri wa kitaalamu kabla ya kuingia katika mikopo kwa ajili ya
kutekeleza miradi ambayo haitakuwa na tija kwao wao na badala yake kuingia katika hasara.
Wakitowa
mada juu ya huduma na fursa mbali mbali zinazopatikana katika benki katika
semina elekezi kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi inayofanyika huko Baraza hilo Chukwani, wawakilishi kutoka Benki
za CRDB, NMB na PBZ wamesema baadhi ya wateja wa benki wamekua wakiingia katika hasara kwa kuchukua mikopo mikubwa kwa
ajili ya miradi ambayo hawakupata ushauri wa kitaalamu wa kifedha na miradi
hiyo.
Wamesema ili kujikinga na tatizo hilo, taasisi hizo za
kifedha zimejipanga kwa ajili ya kutoa taaluma kwa wateja na hatimae kuwapatia
mikopo mbali mbali itakayoleta tija kubwa kwao na hatimae kujikwamua na hali
ngumu ya maisha pamoja na kutengeneza ajira na kuondokana na umasikini miongoni
mwa jamii.
Wawakilishi
hao wa taasisi za fedha wamesema wako tayari kwenda sambamba na azma ya kasi
ya serikali ya kuwaletea maendeleo
wananchi kwa kuimarisha huduma zao mijini na vijijini.
Wakati huo
huo wawakilishi hao wa Mabenki wamewaomba wateja wao kuwatumia mawakala walio
mitaani ili kupunguza msongomano unajitokeza hasa mwisho wa mwezi katika benki
ziliopo hapa nchini.
Nao wajumbe
wa Baraza la Wawakilishi wamezishauri taasisi hizo za kifedha kuzitumia fursa ziliopo
ili kuongeza mitaji na Biashara kwani hivi sasa taasisi hizo zimekuwa ndio kimbilio
la wanyonge.
Mafunzo hayo
ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi yataendelea tena hapo kesho ambapo
kutawasilishwa mada mbali mbali ikiwemo mbinu za uwasilishaji na ushiriki
katika mijadala, Dhana ya uwajibikaji wa Serikali mbele ya Baraza la
Wawakilishi na Taratibu za Maswali na
Majibunkatika Baraza la Wawakilishi.
Imetolewa na
Divisheni ya Itifaki na Uhusiano, BLW
November 13,
2020
No comments:
Post a Comment