Habari za Punde

Mafunzo kwa wakulima wa mwani yaliyotolewa na taasisi ya REPOA Tanzania yafanyika kisiwani Pemba

BAADHI ya wakufunzi wa ukulima wa mwani Kisiwani Pemba, wakifuatilia kwa makini mafunzo ya ukulima wa mwani kisasa yaliyotolewa na taasisi ya REPOA na kufanyika kiwanja cha Makonyo Wawi Chake Chake.(PICHA NA ABDI SUELIMAN, PEMBA)

KATIBU Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Juma Hassan Reli, akitoa maelezo ya kitaalamu kuhusu mwani wakati wamafunzo ya ukulima wa mwani kisasa yanayotolewa na taasisi ya REPOA kwa wakulima 30 watakaoweza kuwafundisha wakulima wenzao vijijini.(PICHA NA ABDI SUELIMAN, PEMBA)

MKURUGENZI Mtendaji wa Taasisi ya utafiti wa sera za maendeleo na umasikini Tanzania (REPOA)Dkt.Donald Mmari, akitoa maelezo mafupi juu ya malengo ya taasisi hiyo katika kuwasaidia wakulima wa mwani nchini na kuinua kipato chao, mafunzo yaliofanyika mjini chake chake.(PICHA NA ABDI SUELIMAN, PEMBA)

WAZIRI wa Kilimo Umwagiliaji na Mifugo Zanzibar Soud Nahoda Hassan, akifungua mafunzo kwa wakulima wa mwani 30 juu ya kulima kisasa wataoweza kuwenda kuwafundisha wakulima wenzao vijijini, yaliyoandaliwa na taasisi ya REPOA na kufanyika mjini Chake Chake.(PICHA NA ABDI SUELIMAN, PEMBA)



MKULIMA wa mwani maarufu Kisiwani Pemba na mbunifu wa vitu mbali mbali kwa kutumia zao la mwani aliyejulikana kwa jina la Fatma kutoka Makangale, akitoa neno la shukuran kwa niaba ya wakulima wenzake wa mwani, katika mafunzo ya ukulima kisasa wa zao hilo yaliyotolewa na taasisi ya REPOA Tanzania.(PICHA NA ABDI SUELIMAN, PEMBA)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.