Habari za Punde

Ufungaji wa Mafunzo ya kwanza ya Ndoa katika Wilaya ya Kaskazini B

Katibu Mkuu Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Seif Shaaban Mwinyi awataka wahitimu wa mafunzo ya ndoa Wilaya ya Kaskazini B kujenga subra, uvumilivu na kusamehe alipokuwa akiyafunga mafunzo hayo katika Ukumbi wa CCM Mahonda.
Naibu Mufti wa Zanzibnar Sheikh Mahmoud Mussa Wadi akizungumza na wahitimu wa mafunzo ya ndoa katika sherehe zilizofanyika Ukumbi wa CCM Mahonda
Baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya kwanza ya ndoa Wilaya ya Kaskazini B wakifuatilia ufungaji wa mafunzo hayo katika Ukumbi wa CCM Mahonda.

 Katibu Mkuu Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Seif Shaaban Mwinyi akimkabidhi cheti cha kumaliza mafunzo ya ndoa mshiriki wa mafunzo hayo Masoud Mohd Ali katika Ukumbi wa CCM Mahonda.

PICHA NA RAMADHANI ALI MAELEZO


Na Khadija Khamis- Maelezo Zanzibar 07/02/2021.

Katibu Mkuu Wizara ya Nchi  Ofisi ya Rais,Katiba, Sheria,Utumishi na Utawala Bora Seif Shaaban Mwinyi  amewataka wahitimu wa mafunzo ya ndoa kuwa na subira ustahamilivu na kusameheana katika kudumisha ndoa zao .

Hayo ameyaeleza  wakati wa Sherehe ya Ufungaji wa Mafunzo  ya kwanza ya Ndoa katika Wilaya ya Kaskazini B , ambapo jumla  ya Wananchi 201 walihitimu mafunzo hayo ya wiki 10 Huko Mkoa  ya Kaskazini, Mahonda.

Alifahamisha mafunzo ya ndoa yanajenga heshima na kila upande kujuwa haki yake ya msingi katika kuimarisha na kutunza familia .

Aidha alifahamisha kwamba mafunzo ya ndoa yatapunguza utitiri wa talaka ambao umeonesha kukidhiri kwa wingi hasa kwa vijana.

Naibu Mufti Mahmoud Mussa Wadi amewashauri wahitimu wa mafunzo hayo, ambao wengi wao ni watu wazima, kuyasambaza mafunzo hayo kwa vijana ambao hawajapata elimu ya ndoa.

Ameeleza matarajio makubwa kwa Mkoa wa Kaskazini unguja baada ya mafunzo hayo yatasaidia kupunguza mizozo ya ndoa ndani ya mkoa huo iwapo yatatumika kikamilifu.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B,

Katibu Tawala Makame Machano Haji aliiomba Ofisi ya Mufti kuendeleza elimu ya ndoa katika maeneo mengine ya Wilaya ya Kaskazini B, ikiwemo Bumbwini Mahonda na Kiwenga.

Alisema kutolewa mafunzo hayo kutaepusha utoaji wa talaka kiholela pamoja na vitendo vya udhalilishaji ambayo vinaongoza katika Mkoa huo .

Nao Wahitimu hao wameipongeza  Serikali kupitia Ofisi ya Mufti kwa kuwapatia elimu hiyo ambayo imewasaidia kuzijua haki zao.

Wametoa wito kwa vijana wenzao kushiriki katika mafunzo hayo ili kuweza kujuwa mambo mbali mbali ya sheria za kiislamu .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.