Habari za Punde

Hospitali ya Mnazi Mmoja Imetakiwa Kuondokana na Tabia ya Kupeleka Wagonjwa Nje ya Nchi.

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Afya Utawi wa Jamii Wazee Jinsia na Watoto Zanzibar, wakati wa kuwasilishwa kwa taarifa ya utekelezaji wa maagizo yake aliyoyatoa kwa Mawazi na Makatibu Wakuu wakati alipowaapisha Ikulu, mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar. 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema wakati umefika kwa Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto kuondokana na  utaratibu wa kupeleka wagonjwa nje ya nchi kwa matibabu, na badala yake fedha zinazotumika zielekezwe kuimarisha vitengo vya tiba katika Hospitali ya Rufaa Mnazi mmoja.

Dk. Mwinyi amesema hayo Ikulu Jijini hapa wakati alipozungumza na Viongozi na watendaji wa Wizara hiyo katika mkutano uliojadili utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa kwa Mawaziri na Makatibu wakuu wakati alipowaapisha.

Amesema kwa muda mrefu Wizara hiyo imekuwa na utaratibu wa kupeleka nje ya nchi idadi  kubwa ya wagonjwa kwa matibabu, wakiwemo wale wenye uwezekano wa kutibiwa nchini na hivyo kuilazimu Serikali kutumia fedha nyingi, ikiwemo posho la kujikimu wao na madaktari wanaowasindikiza.

Alieleza kuwa hatua ya kupeleka wagonjwa nje ikiwemo India ,inapaswa kufanyika pale pasipo budi na kubainisha kuwa wagonjwa watakaoshindikana kutibiwa katika Hospitali ya Rufaa Mnazi mmoja watapaswa kupelekwa Hospitali za Tanzania Bara.

Alisema fedha zinazotumika kupeleka wagonjwa hao zinapaswa kuelekezwa katika kuviimarisha vitengo vya tiba vilivyopo katika Hospitali ya Rufaa Mnazi mmoja.

Aidha, aliitaka Idara ya Kinga kutoa kipaumbele katika uimarishaji wa vitengo kwa kuvipatia vifaa,  akibainisha kuwepo madaktari wenye uwezo mkubwa kiutendaji.

 

AliwatakawataalamuwaWizarahiyokukaachininakuishauriserikalininikufanyikeilikuondokananachangamotoyakuwepokiwangokikubwa cha vifovyawatotowachanga, wakatiambapotakwimuzikizonyeshakuwepowastaniwawatotowachanga 23 wanaofarikikwakilavizazi 1,000.

 Katika hatua nyengine, Dk. Mwinyi alisema wakati umefika kwa serikali kutafuta njia za kuanzisha huduma za Bima ya Afya, kwa kuzingatia kuwa Bajeti ya Serikali haiwezi kukidhi mahitaji ya kila jambo.

“Hatuwezi kutoa huduma za Afya kwa ufanisi kwa kutegemea fedha za Serikali pekee”, alisema.

Alieleza kuwa pamoja na Sera ya Mapinduzi ya Zanzibar ya 1964 kubainisha upatikanaji bure wa huduma za Afya nchini, alisema hatua hiyo inapaswa kuendelezwa kwa ajili ya wananchi wasio na uwezo, sambamba na wale wenye uwezo kutumia huduma za Bima ya Afya, hivyo akawataka viongozi wa Wizara hiyo kukaa chini na kuanza kufikiria uanzishaji wa huduma hiyo.

Aidha, alisema ni jambo gumu kwa Serikali kumpatia mgonjwa kila aina ya dawa bure, hivyo akataka juhudi zaidi zifanyike ili kuwa na vyanzo zaidi vya mapato kusaidia utoaji wa huduma bora za afya.

Akizungumzia suala la upatikanaji wa dawa, Dk. Mwinyi alisema eneo hilo linamatatizo makubwa, hivyo akiitaka Bohari Kuu ya Dawa kubeba jukumu la ununuzi na usambazaji wa dawa hizo, kazi ambayo hivi sasa inafanywa na Wizara.

Alisema kuna umuhimu wa kutizama matatizo yaliopo na kuyapatia ufumbuzi, akibainisha kuwa Hospitali ndio yenye taarifa sahihi za kuelewa matatizo waliyonayo na sio Wizara,  akatoa mfano wa tenda ya ununuzi wa vifaa (vyuma) kwa ajili ya tiba ya wagonjwa wa mifupa iliochukuwa miezi kutokana na utaratibu huo.

Aliitaka Bohari ya Dawa ipewe jukumu la kuagiza na kusambaza dawa zote na kusema huo ndio mfumo ulio kamilika, hata hivyo alishangazwa na taarifa za kuwa Bohari hiyo hain amfumo wa kumbukumbuku pitia Komputa.

Aidha, alieleza umuhimu wa kuangalia mahitaji yaliopo wakati wa kufanya ajira ili kuondokana na tatizo la upungufu wa wafanyakazi linaloonekana kujitokeza katika baadhi ya vitengo na Idara zake.

Aliitaka Wizara hiyo kufanya juhudi za ziada ili kupata fedha zitakazowezesha kuondokana na changamoto ya Ofisi Kuu Pemba ya kukosa huduma za uchomaji taka (incinerator) katika Hospitali za Abdalla Mzee, Wete pamoja na Vitongoji, ili kuondokana na taka hatarishi.

 Akigusia changamoto zinazozikabili Idara mbalimbali za Wizara hiyo, Dk. MwinyialiitakaWizarahiyokuwanamifumoyapamojakwakuzingatiakuwatayariSerikaliilitoafedhanyingiilikufanikishakazihiyoambayohaikufanyikaipasavyo.

 

AliutakaUongoziwaWizarahiyokuliangaliasualahilokwa kinailikubainiusahihiwamatumiziyafedhahizonajinsizilivyotumika, wakatihuumitandaoikiwahaifanyikazi.

 

Vile vile, Dk. MwinyiakautakaUongozihuokufikiriauwezekanowakuziungnishataasisizaWakalawaChakula, DawanaVipodozinaileyaMkemiaMkuuwaSerikaliilikuwataasisimojakwadhamirayakuletaufanisinakuondoaurasimu.

KuhusiananamiradiyamaendeleoyaWizarahiyo, alitakajuhudizifanyikekutafutamikopokutokamashirikayaKimataifailikupatafedhazitakazowezeshakufanikishamiradihiyokwakuzingatiaukubwawagharama, hukuakitakafedhazaBajetizitumikekulipiamikopohiyo.

AliwatakaviongozihaokutathminuamuziwaSerikaliwakuifanyiaugatuzisektayaAfyakatikaManispaazaWilaya, iwapoumeletaufanisi, akibainishaumuhimuwakufanyaugatuziwenyekuletatija, sambambanakuwatakakuendeleeakuvutiawahisaniilikuimarishahudumazaAfyanchini.

Mapema, KatibuMkuuWizarayaAfya, UstawiwaJamii, Wazee, JinsianaWatoto Dk. Omar DadiShajakalisemakatikakufanikishautatuziwachangamotoziliopo, Wizarahiyoimeandaamipangokadhaakwalengo lakuimarishamazingirayautendajikazi, ikiwemokuwekautaratibuwakuanzishamifumoya TEHAMA itakayounganishamifumoiliopoilikupunguzagharamayakuwepomifumomingi.

AlisemaWizarainalengakupunguzamsongamanowawagonjwakatikaHospitaliyaRufaa, MkoanaWilaya, ambapokwakushirikiananaOfisiyaRais, TawalazaMikoa, SerikalizamitaanaIdaramaalumza SMZ itavijengeauwezovituovyaAfyavyamsingipamojanavituovyamadarajaya kwanza napiliilikutoahudumakwasaa 24.

AlisemaWizaraitaifanyiaukarabatimkubwaWodiyaMifupa, chumba cha upasuajipamojanakufanyamarekebishoyamiundombinuyaHospitali, sambambanakununuamashinenasamani.

WizarayaAfya, UstawiwaJamii, Wazee, JinsianaWatotoinajumlayawafanyakaziwakadambalimbali5,062 Ungujana Pemba, ambapo kw amujibu w atakwimuzamwaka 2020 ianjumlayamadaktari 345, wauguzi 1,328. 

AbdiShamna, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822 

 E-mail: abdya062@gmail.com

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.