Habari za Punde

Wanawake wahimizwa kupima afya na kushiriki mazoezi

 Mwashungi Tahir    Maelezo    15/3/2021.

Wanawake nchini wametakiwa kuwa na tabia ya kupima afya zao na kushiriki kufanya mazoezi ili kujilinda na maradhi  yasiyo ambukiza. 

Akizungumza na wanachama wa chama hicho  Daktari wa maradhi bingwa yasioambukiza Salama Asaa Ali kutoka Mnazi Mmoja  katika Ukumbi wa Tamwa ulioko Tunguu wakati wa mkutano mkuu wa waandishi wa habari wanawake  na kutoa  elimu ya afya kwa lengo la kujitambua mapema afya zao na  kupatiwa matibabu haraka.

Amesema baadhi ya akinamama wengi hawana tabia ya kufika vituoni kupima afya zao kwani inasaidia unapogundilika unaanza kuwa na maradhi yataweza kutibika kwa haraka  kabla hayajakithiri ndani ya miili yao.

Hivyo amesema hivi sasa kuna maradhi mengi duniani ikiwemo kisukari, kensa, presha  na kuwaomba kula vyakula vya matunda , kunywa maji kwa wingi na kuepuka kula vyakula vya  mafuta mara kwa mara ili kuepukana na maradhi hayo.

Nae Mkurugenzi wa waandishi wanawake  Tamwa, Dr Mzuri Issa amesema ametaka wanawake kupatiwa elimu hiyo kwa lengo la kupima ili kujitambua mapema na kufanyiwa matibabu.

Nao wanachama wa mkutano huo wa Tamwa wameishukuru jumuiya hiyo kwa kuwapatia elimu hiyo ambayo itawafanya kuhamasika kupima afya zao  pale mtu akiona zile dalili zilizotajwa anazo ili kupatiwa matibabu.

Aidha elimu nyengine iliyotolewa hapo ni pamoja na changamoto za uzazi,shingo ya kizazi, tezi dume,  matatizo yanayosababisha kukosekana kwa hedhi, figo na mengi mengineo.

Mkutano huo hufanyika kila mwaka kwa lengo la kujadili mikakati na maendeleo ya chama hicho cha waandishi wa habari wanawake Tamwa  ambao ulifanyika siku mbili huko Tunguu Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.