Habari za Punde

Ziara ya Maendekleo ya Viwanda Yaendane na Hifadhi ya Mazingira - Waziri Mhe. JAFO

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo akitoa maelekezo Mkurugenzi wa Kiwanda cha Lodhia Steel Industry Ltd.  Bw. Sailesh Pandit mara baada ya kufanya ziara ya kikazi Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani.

Mkurugenzi wa Kiwanda cha Lodhia Steel Industry Ltd.  Bw. Sailesh Pandit akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo kuhusu shughuli za uendeshaji na hifadhi ya mazingira kiwandani hapo, Waziri Jafo hii leo amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Mkuranga kujionea uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo akiwasili katika Kiwanda cha Nondo cha Lodhia kilichopo katika Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mkurunga Bw. Filberto Sanga na Bw. Sailesh Pandit Mkurugenzi wa Kiwanda hicho.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo akitoa maelekezo kwa Meneja wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda ya Mashariki kusini Bw. Hamad Taimur (hayupo pichani) kuhusu Kiwanda cha Saruji cha Diamond ambacho kimekithiri kwa uchafuzi wa mazingira. Waziri Jafo amefanya ziara hiyo leo Mei 4, 2021. Watatu kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mkurunga Bw. Filberto Sanga.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.