Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi Amekutana na Kuzungumza na Balozi wa Uturuki Nchini Tanzania leo Ikulu Zanzibar.

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na mgeni wake Balozi wa Uturuki Nchini Tanzania Mhe.Mehmet Gulluoglu, alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza mgeni wake Balozi wa Uturuki Nchini Tanzania Mhe. Mahmet Gulluoglu alipofika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na mgeni wake Balozo wa Uturiki Nchini Tanzania Mhe. Mehmet Gulluoglu, akimshindikiza baaba ya kumaliza mazungumzo yao yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi alikutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania Dk. Mehmet Gulluoglu.

Dk. Mwinyi alisema kutokana na mashirikiano yaliopo kati ya nchi mbili hizo, ana imani kubwa kuwa Wawekezaji  kutoka Uturuki watashajihika na kuja nchini kwa ajili ya kuwekeza katika nyanja  tofauti, pale hali ya ugonjwa ya Covid -19 itakapopungua.

Nae, Balozi Mehmet aliahidi kuendeleza uhusiano na ushirikiano ulipo kati ya nchi mbili hizo, sambamba na   kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuimarisha sekta za Uwekezaji , Utalii, Uvuvi pamoja na Mafuta na Gesi.

Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822      

 E-mail: abdya062@gmail.com

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.