Habari za Punde

Kumbukizi ya Hayati Benjamin Mkapa · Uwanja wa Mkapa: Zawadi ya Umoja na Mshikamanowa Kitaifa

Na:Lillian Shirima – MAELEZO.

Wadau ya wanamichezo wataendelea kumkumbuka aliyekuwa rais wa Awamu ya Tatu Hayati Benjamin William Mkapa kwa zawadi ya ujenzi wa Uwanja wa Taifa, sasa Uwanja wa Mkapa,ambao umeleta hamasa katika tasnia ya michezo.

Akiongea na Idara ya Habari-MAELEZO Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Miundombinu ya Michezo Makoye Alex Nkenyenge amesema, wakati taifa linaadhimisha mwaka mmoja wa kumbukizi ya aliyekuwa rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Tatu, Hayati Benjamin William Mkapa wadau wa michezo wataendelea kumkumbuka kutokanaujenzi wa Uwanja wa Michezo ulioanza kujengwa ulianza kujengwa mwaka 2003 wakati wa uongozi wake.

‘Tangu kujengwa kwa uwanja huu viwanja vingine vidogo zaidi ya 9vimejengwa na watu binafsi pamoja na Taasisi.Hii imewatia moyo wadau mbalimbali kama Azam’.

Aidha amesema, Hayati Mkapa alikuwa kiongozi mwanamapinduzi,mwenye njozi ya kuona watanzania wanatumia michezo si kwa ajili ya burudani au kuimarisha afya  pekee bali kuimarisha mshikamano, kuleta umoja wa kitaifa lakini pia michezo itanyike kwa maendeleo ya taifa, pengine hiyo ilikuwa zawadi ya ndoto yake kwa watanzania;Ujenzi wa Uwanja wa Michezo.

Akielezea tija itokanayo na uwanja huo amesema, serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imekuwa ikishughulika na ustawi wa wananchi hivyo shughuli kubwa zinazofanyika uwanjani hapo hukusanya watu wenye itikadi tofauti za kisiasa, dini na utaifa ambao kwahufurahi na kuburudika pamoja.

Hata hivyo amesema, mbali na masuala ya burudani mechi kubwa au matukio makubwa yanapofanyikahutoafursa kwa vikundi zaidi ya sita vya vijana vinavyojiandikisha mapema kabla ya tukio kutoa huduma ya vyakula na vinywaji ndani ya uwanja hukuwajasiriamali wengine wengiwakipata nafasi ya kufanya biashara mbalimbali nje ya uwanja ambapowatu zaidi ya 5,000 wanakadiriwa kuwepo.

‘Wajasiriamali wengi wanaoishi maeneo yanayozunguka uwanja na wale waishio jirani hutegemea kujipatia kipato kutokana na kuwepo kwa Uwanja wa Mkapa hivyo, tunapozungumzia Mkapa tunazungumzia maisha ya makundi ya watu wanaonufaika na kujishirikisha na masuala ya biashara ndogo hasa wakazi wa temeke na maeneo mengine’.  

Akielezea mabadiliko ya jina la uwanja huo Nkenyenge amesema, maamuzi aliyofanya Hayati John Pombe Magufuli, rais wa awamu ya tanokuamua uwanja wa taifa uitwe Uwanja wa Mkapa ilikuwa ni faraja kubwa kwa wadau wa michezo kutokana na ukweli kwamba siku zote wananchi watakapoingia uwanjani au kuangalia matukio yanayoendelea uwanjani hapo kupitia luninga wataendelea kumkumbuka Mkapa.

Jina la Uwanja wa Mkapalilitangazwa na Hayati John Pombe Magufuli wakati wa hafla ya kitaifa ya kuuaga mwili wa Mkapa aliyefariki usiku wa kuamkia Julai 24, 2020 Jijini Dar es Salaam.

Uwanja huu wa Mkapa upo katika wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam ulianza kujengwa mwaka 2003 ikiwa ni muhula wa pili wa hayati Benjamin Mkapa madarakani na kumalizika mwaka 2007 ambapo ujenzi wake ulifanyikakwa ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na China kama sehemu za programu za kidiplomasia kwa gharama ya dola za kimarekani Milioni 57.

Wataalam wanatafsiri kuwa, uwanja ni eneo kubwa lililojengwa kwa wachezaji kucheza na kwa watazamaji kuangalia michezo mbalimbali, matamasha, na matukio mengine mengi yanayoendelea uwanjani hapo na kwamba usanifu wa ujenzi wa uwanja unafanywa kwa namna ambayo watazamaji wanaweza kuona chochote bila kujali upande waliokaa.

Kutokana na kukidhi viwango vyamahitaji yote ya michezo kimataifa, Uwanja wa Mkapa       umethibitishwa na FIFA pamoja na Shirikisho la Riadha Dunianina unatumika kwa shughuli nyingi tofauti zikiwemo za kitaifa ingawa mpira wa miguu ni mchezo unaotumia zaidi uwanja huu.

Ukiwa na uwezo wa kuchukua mashabiki elfu 60, uwanja wa Mkapa ni miongoni mwa viwanja vikubwa Afrika na mkubwa kuliko yote nchini. Tangu kukamilika kwake michezo mbalimbali imefanyika, mechi za kirafiki, kitaifa na kimataifa zimefanyika.

Kadhalika, uwanja unatakadiriwa kuchukua miaka 30 kabla ya kufanyika kwa matengeneza makubwa, hii inatokana na ujenzi wake kutumia teknolojia ya juu.

Baadhi ya timu kubwa za kimataifa zilizowahi kucheza katika uwanja huu ni Evaton, Ivorycost, na Brazil na kupitia timu hizi nchi yetu inajitangaza. 

Itakumbukwa kuwa mwaka 2019 Tanzania ilikuwa mwenyeji wa finali ya mashindano ya mpira wa miguu kwa vijana chini ya umri wa miaka 19na hata ile ya AFCON chini ya 17 ilifanyika ndani ya uwanja wa Mkapa.

Katika kuenzi mchango wa Hayati Benjamin Mzee aliyesimamia dhana ya uwajibikaji,watanzania tutaendelea kumkumbuka kwa kutujengea uwanja wa michezo wenye miundombinu ambayo haitofautiani na ile iliyojengwa katika nchi zilizoendelea duniani na kupitia michezo tunaimarisha upendo, umoja na mshikamano wa taifa letu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.