Habari za Punde

Taasisi ya Al Falasi kuisaidia Zanzibar kwenye huduma za Afya

Mkuu wa Taasisi ya Al falasi kutoka (UAE) Ahmad Al-falasi akizungumza na waandishi wa habari kuhusu dhamira yake yakutaka kusaidia katika sekta ya afya Zanzibar Mkutano uliofanyika Hoteli ya Park Hyatt Shangani Mjini Zanzibar.
Mkuu wa Taasisi ya Al falasi kutoka (UAE) Ahmad Al-falasi akisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu dhamira yake ya kutaka kusaidia katika sekta ya afya Zanzibar Mkutano uliofanyika Hoteli ya Park Hyatt Shangani Mjini Zanzibar.
Mwandishi wa habari wa ITV Farouk Karim akiuliza maswali katika Mkutano na Mkuu wa taasisi ya Al falasi uliofanyika Hoteli ya Park Hyatt Shangani Mjini Zanzibar.

 Mtoto wa Mkuu wa Taasisi ya Al falasi Shaima Ahmad Alfalasi akijibu maswali mbalimbali yaliyoulizwa na wandishi wa habari (kushoto) ni Mke wa Ahmad Al-falasi.

Picha na Makame Mshenga.


Issa Mzee    Maelezo 09/07/2021

Wizara ya Afya Ustawi wa Jamii,Wazee Jinsia na Watoto inaendelea kushirikiana na wahisani wa maendeleo katika kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana Nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari katika majumuisho ya ziara ya kutembelea katika maeneo mbalimbali ikiwemo vituo vya afya, mkuu wa Taasisi ya Alfalasi Ahmed Alfalasi amesema taasisi yake itahakikisha inaisaidia Serikali ya Zanzibar katika kuhakikisha huduma bora za afya zinatolewa Mjini na Vijijini.

Alisema kuwa katika ziara hiyo wamebaini uhitaji wa matengenezo ya mashine mbalimbali kwa Hospitali za Zanzibar nakuahidi kuzikarabati ili ziweze kufanya kazi vizuri.

Alieleza kuwa tasisi hiyo imepanga mkakati wa kuwaleta mafundi kutoka Nchini Dubai ili kuzitengeneza mashine hizo pamoja na kuwapa ujuzi mafundi waliopo Zanzibar ili kuwajengea uwezo wa kuzitengeneza mashine hizo jambo ambalo litasaidia katika kuleta ufanisi hospitalini.

Aidha alisema  miongoni mwa maeneo yanayohitaji msaaada ni pamoja na  Benki ya Damu pamoja na wodi ya wazazi ambayo inatarajiwa kupata msaada hivi karibuni.

Akizungumzia kuhusu suala la msaada wa dawa mkuu huyo alisema  atafanya mazungumzo na Wizara ya afya Nchini Dubai ili kuona namna nzuri ya kuipatia Zanzibar  msaada huo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.