Habari za Punde

ZURA Yakabidhi Kamati ya Zanzibar Marathon.

Na Mwashungi Tahir   Maelezo  Zanzibar. 15-7-2021

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Maji, Nishati ZURA  Bihindi Nassor Khatib  wamekabidhi hundi ya Millioni ishirini kwa waandaaji wa mbio za marathon yanayotarajiwa kufanyika tarehe 18-7 -2021.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari huko katika Ukumbi wa ZURA amesema fedha hizo lengo lake kuwazidisha nguvu mashindano hayo ambayo yatahamasisha wazanzibar  na kuweza kuibua vipaji kwa washiriki hao.

Amesema mashindano hayo yatawaimarisha mamlaka hiyo kwa kuitangaza na kuboresha huduma zao ikiwemo mafuta, nishati na gesi  pamoja na kukuza sekta ya utalii ambapo utazidi kuimarika kwa vile  inaingiza pato kubwa kwa Serikali.

Pia amesema ZURA  ina kawaida ya kuwasaidia watu wenye mazingira magumu, walemavu wa viungo na wa akili kwa lengo la kuwapa misaada hiyo ili na wao waweze kufarijika kwa kujikimu maisha yao.

Bihindu amesema kwa vile Serikali  inathamini michezo  ndani ya wao ZURA  wana timu ya michezo wa mpira wa miguu na ndani ya mashindano hayo wafanyakazi  18  watashiriki katika mbio hizo za marathon kwa kilomita 5 na 10.

“Michezo ni afya, mashirikiano na kupata kuweza kujuana hivyo na sisi hatuna budi kuunga mkono suala hili na ZURA ipate kujitangaza kwa huduma zao wanazozitoa kwa wananchi”, alisema  Mkurugenzi huyo.

Nao waandaaji wa mashindani hayo  ya marathon  wamefurahishwa sana kwa kupatiwa kiasi cha fedha hizo na wamesema wamepata matumaini  makubwa   kwa kupata wafadhili na kutokana na nguvu waliyopata wanatarajia na mwakani kuandaa tena mashindano hayo.


Mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika tarehe 18-7-2021 yatafunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi huko Forodhani na washiriki watakimbia kilomita 5 ,10  na zaidi  hadi kumalizikia katika Uwanja wa Amani Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.