Baraza la Wawakilishi linatarajiwa kuanza
kutumia mfumo wa baraza mtandao kupitia tablet katika shughuli za uendeshaji wa
vikao vya baraza na kazi za kamati kuanzia mkutano wa nne wa baraza
la kumi unaotarajiwa kuanza mwezi Septemba.
Hatua hiyo imekuja baada ya kukamilika taratibu
zote za makabidhiano ya Tablet hizo yaliyoambatana na mafunzo ya utumiaji
wake yaliyofanyika Chukwani.
Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo Spika
wa Baraza la Wawakilishi Mhe Zubeir Ali Maulid amefahamisha kuwa matumizi ya mtandao
katika kuongoza Baraza yatasaidia kuokoa gharama kubwa ambayo ilikua ikitumika
katika matumizi ya nyaraka za karatasi.
Akikabidhi Tablets hizo Katibu wa Baraza la Wawakilishi
Raya Issa Msellem amesema kuwa hatua hiyo itasaidia kuondoa matumizi ya
karatasi katika shughuli za Baraza na kuwarahishia Waheshimiwa Wawakilishi
kupata nyaraka zote mbali mbali kwa njia ya mtandao kupitia tablets zao.
Nao Waheshimiwa wameipongeza hatua ya ofisi ya Baraza
la Wawakilishi kuwapatia Tablets huku wakisema kuwa hatua hiyo ni utekelezaji
wa vitendo maelekezo ya Mhe Rais katika kuimarisha mifumo ya kisasa ya
kidigitali wakati akizindua Baraza la kumi la Wawakilishi ambapo unalenga
kurahisisha shughuli zao.
No comments:
Post a Comment