Picha na Maryam Kidiko / Maelezo Zanzibar
Pili Ali - Maelezo
Idara ya Ustawi wa Jamii Zanzibar imemkamata Mama Mzazi wa mtoto aliyetelekeza mwenye umri wa miezi minane kwa kumuacha nyumbani bila ya kumpa huduma yoyote huko maeneo ya Kianga Wilaya Magharibi “A” Unguja.
Mama huyo anaejulikana kwa jina la Dorice Moses Mazigu mwenye umri wa miaka 27 alikamatwa leo huko Mbuzini Wilaya ya Magharibi A katika kumbi za starehe na Idara ya Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na masheha wa shehia ya Kianga na Mbuzini.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupatikana mama huyo huko Welezo Mkurugenzi wa Idara ya Ustawi wa Jamiii na Wazee Abdalla Saleh Omar huko Ofisini kwake, amesema Mama huyo yuko chini ya uangalizi wa vyombo vya sheria kwa ajili ya hatua za kisheria.
Nae Afisa Ustawi wa Jamii katika kitengo cha Hifadhi ya Mtoto Ramadhan Mohamed Ramadhan amesema hali ya mtoto huyo imedhoofika kutokana na kukosa huduma za mama na uangalizi mazuri.
Ameeleza kuwa mtoto huyo anapatiwa huduma katika hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja kwa matibabu ambae anasumbuliwa na vidonda pamoja na tatizo la utapia mlo yuko chini Idara ya Ustawi wa Jamii kwa huduma.
No comments:
Post a Comment